STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 6, 2014

Rais JK, mkewe washiriki kumuangaMeja Jen. Msemwa


 Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe mama Salma Kikwete wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa  aliyekuwa Kamishna wa Utafiti na maendeleo ya Jeshi katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa  marehemu Meja Jenerali Kevin Gerald Msemwa wakati wa hafla ya kuaga mwili wake iliyofanyika katika uwanja wa makao makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Upanga jijini Dar es salaam leo April 6, 2014. Meja Jenerali Msemwa alifariki April 3, 2014 katika hospitali ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es salaam. 
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe mama Salma Kikwete wakitoa mkono wa pole kwa wanafamilia baada ya kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Kamishna wa Utafiti na maendeleo ya Jeshi katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa  marehemu Kevin Gerald Msemwa wakati wa hafla ya kuaga mwili wake iliyofanyika katika uwanja wa makao makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Upanga jijini Dar es salaam leo April 6, 2014. Meja Jenerali Msemwa alifariki April 3, 2014 katika hospitali ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment