STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 25, 2014

Mbwa Mwitu wa Kajala azinduliwa, Lamata alalamika

BAADHI ya picha za matukio katika shughuli hiyo ya usiku wa jana
FILAMU ya Mbwa Mwitu ya msanii Kajala Masanja imezinduliwa kwa kishindo usiku wa jana kwenye ukumbi wa Sinema wa Mlimani City, huku mtunzi na muongozaji wake, Leah Richard 'Lamata' akilalamika ukiritimba unaofanywa na wasimamizi wa tasnia ya filamu nchini.
Lamata aliidokeza MICHARAZO mapema kuwa, kabla ya kuzindua filamu hiyo iliyotengenezwa na Kay Entertainment wakikumbana na vikwazo wakipigwa namna simulizi la filamu hiyo ya dakika 15 iliyogusa matukio ya kweli yaliyoikumba jamii hivi karibuni kutoka makundi ya wahalifu yaitwayo 'Mbwa Mwitu', 'Boda kwa Boda', 'Bad Face' na 'Watoto wa Mbwa'.
"Hii inkatisha tamaa lengo letu kuifundisha jamii juu ya kuepuka uhalifu kwani mwisho wake huwa siyo mwema, lakini 'mabosi' wanaosimamia fani hii wanadhani sisi tunaelimisha vibaya katika matukio yaliyopo ndani ya filamu hii ya 'Mbwa Mwitu'.
Lamata alisema bado wataendelea kutunga filamu zinazoigusa jamii sambamba na kuielimisha, kuionya na kuiburudisha kama sifa za fasihi ilivyo.
Ndani ya filamu hiyo wamo Kajala, Hemed Suleiman, Mama Kawele, Quick Racca na Mwinjuma Muumin 'Kocha wa Dunia'.
Nyota mbali walihudhuria onyesho hilo wakiwamo waigizaji Rich Richie, mtoto wa Kajala, Paula, Sandra, Odama na wengineo kibao waliompiga tafu Kajala.

No comments:

Post a Comment