STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 31, 2014

Alex Song achekelea Ligi ya England

http://estaticos.marca.com/imagenes/2012/08/19/en/football/barcelona/1345394833_extras_mosaico_noticia_1_g_0.jpg
KIUNGO Alex Song, 27 anapanga kubaki kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kuanza vyema muda wake wa kucheza kwa mkopo wa muda mfupi katika klabu ya West Ham ambayo ameisaidia kukwea hadi nafasi ya nne katika msimamo baada ya kuwazamisha mabingwa Man City Jumamosi iliyopita.
"Nadhani hatma yangu iko hapa (England)," aliiambia Sky Sports. "Familia yangu, kila mmoja ana furaha hapa. Nina furaha sana kurejea England.
"Daima nimekuwa nikisema kama nitaondoka Barcelona , nitakuja England na hatma yangu iko hapa hata hivyo.
"Nataka kufurahia kucheza soka kwa sasa na tutaona nini kitatokea mwisho wa msimu."  

No comments:

Post a Comment