STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 31, 2014

'Lionel Messi ni zaidi ya Cristiano Ronaldo'

http://gms.cachefly.net/images/9332f7310262fe4012a93d5aa2ec54f2/650.jpgKOCHA wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza, Fabio Capello amedai kuwa nyota wa Barcelona Lionel Messi ana kipaji zaidi ya mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo. 
Messi, 27 anatarajiwa kuwa mfungaji mwenye mabao mengi La Liga kama akifunga mabao mawili katika mchezo wa nyumbani dhidi ya Celta Vigo hapo kesho. 
Ronaldo mwenye umri wa miaka 29 anashikilia nafasi ya 10 katika orodha hiyo. Capello amesema Ronaldo ni mchezaji mwenye nguvu mbinu nzuri lakini huwezi kulinganisha ujuzi wa kiufundi halisi alionao Messi. 
Messi ameshafunga mabao 250 katika mechi 284 alizoichezea Barcelona akiwa amebakisha bao moja kufikia rekodi ya nyota wa zamani wa Atletico Madrid Telmo Zarra aliyoweka kati ya mwaka 1940 na 1950.

No comments:

Post a Comment