STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 31, 2014

Polisi yakana kunaswa kwa wauaji wa Meyiwa

http://citizen.co.za/wp-content/uploads/sites/18/2013/10/TL_1081310-602x400.jpgJESHI la Polisi nchini Afrika Kusini wamekanusha taarifa kuwa watuhumiwa wa mauaji ya nahodha wa timu ya taifa ya Afrika Kusini, Bafana Bafana, Senzo Meyiwa wamekamatwa katika daraja la Beit lililopo katika mkapa na Zimbabwe. 
Msemaji wa jeshi hilo Neville Malila amesema tetesi hizo kuwa kuna mtu amekamatwa sio za kweli ila uchunguzi kuhusiana na tukio hilo bado unaendelea. 
Awali kulizuka taarifa kuwa mtuhumiwa mmojawapo wa katika mauaji hayo alikamatwa katika daraja hilo lililopo mpakani na Zimbabwe na kuwa alipelekwa Vosloorus mahali ambako alitenda kosa hilo. 
Meyiwa aliuawa siku ya Jumapili kwa kupigwa risasi wakati akiwa katika harakati za kumuokoa mpenzi wake Kelly Khumalo nyumbani kwake wakati majambazi walipovamia na kutaka kuwapora vitu vyao vya thamani.
Kipa na nahodha huyo wa timu ya Orlando Pirates na Bafana Bafana anatarajiwa kuzikwa siku ya Jumapili.

No comments:

Post a Comment