STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 31, 2014

Nguvu ya Umma yamng'oa Rais Compaore

http://api.ning.com/files/TgHj0KqUN*sX9e*LQOoFNFdBmjR8AKGdAHVfrhLq-iDc3HuWmmMQ4Q1Jdxmu6-BA0j*RTstgln8BgRdlbBGnikzEAvgB0z8g/traore.jpg
Kiongozi wa Mpito wa Burkina Faso
http://www.dw.de/image/0,,18025612_303,00.jpg
Rais aliyeondoka madarakani kwa nguvu ya umma
NGUVU ya umma nchini Burkina Faso zimemng'oa Rais Blaise Compaore. 
Taarifa zinasema Rais huyo amejiuzulu katika kiti hicho licha ya msimamo wake wa awali kwamba asingejiuzulu kama shinikizo la wapinzani. Maandamano ya siku kadhaa ya kupinga mpango wa rais huyo kujiongezea muhula wa madarakani yamesababisha vifo vya watu kadhaa na inaelezwa kuwa Rais Compaore ametoweka na haijulikani alipo.
Kwa sasa nafasi yake inashikiliwa na Mkuu wa Majeshi wa nchi hiyo, Honore Traore ili kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.
Hatua bya Rais huyo anayedaiwa kuiongoza Burkina Faso kwa Mkono wa Chuma imekuja baaada ya vurugu zilizosababisha uchomaji moto wa Bunge la nchi hiyo na ofisi za chama tawala.

No comments:

Post a Comment