STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 31, 2014

Steven Gerrard kuhama Liverpool iwapo...

http://img.thesun.co.uk/aidemitlum/archive/01567/gerrards_1567523a.jpg
Steven Gerrard
NAHODHA wa klabu ya Liverpool, Steven Gerrard amebainisha kuwa atajiunga na klabu nyingine kama timu hiyo ikishindwa kumpatia mkataba mpya. 
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 34 ambaye alijiunga katika shule ya soka ya Liverpool akiwa na umri wa miaka tisa, ameondoa uwezekano wa kustaafu soka wkati mkataba wake utakapomalizika Mei mwaka huu. 
Kiungo huyo amesema hana mpango wa kutundika daruga majira ya kiangazi kwani amepanga kuendelea kucheza soka zaidi. 
Gerrard aliendelea kudai kuwa kwasasa anasubiria kuona kama itakuwa ni Liverpool au mahali pengine, huo utakuwa uamuzi wa klabu hiyo. 
Nahodha huyo wa zamani wa Uingereza ambaye alitangaza kustaafu soka la kimataifa Julai mwaka huu ameichezea Liverpool karibu mechi 700, huku akicheza na washambuliaji mahiri wa zamani Robbie Fowler na Michael Owen.

No comments:

Post a Comment