STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 11, 2013

Hatma ya Milovan Simba leo

Kocha wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic


HATMA ya aliyekuwa kocha wa Simba, Mserbia Milovan Cirkovic, kulipwa fidia yake ya kusitisha mkataba wa kuifundisha timu hiyo huenda ikajulikana leo wakati atakapokutana na viongozi wa klabu hiyo kabla ya kurejea kwao baada ya kupata haki yake.
Hata hivyo, Milovan ambaye ameumizwa na sare ambazo Simba imeendelea kuzipata, alisema jana kwamba yuko tayari kurejea kwenye timu hiyo endapo uongozi utamrejesha.
Milovan anaidai Simba dola za Marekani 24,000 (Sh. milioni 36), ambazo ni malimbikizo ya mishahara yake ya miezi mitatu.
Akizungumza jana, Milovan, alisema kwamba  hadi sasa anafahamu kuwa yeye bado ni kocha halali wa timu hiyo kwani mkataba wake unamalizika Julai Mosi mwaka huu.
Mserbia huyo alisema kwamba ndiyo maana, baada ya kuona viongozi wa klabu hiyo wakikaa kimya, aliamua kuja nchini kufuatilia haki yake na kwamba, hata hoteli anayoishi jijini Dar es Salaam gharama zake zitalipwa na Simba.
"Mimi najua bado ni kocha wa Simba kwa sababu mkataba wangu haujamalizika. Na kama watakuwa tayari kuzungumza na mimi, naweza kurejea kazini. Bila shaka mnajua uwezo wangu na nini nilikifanya katika ligi na mshindano ya kimataifa mwaka jana," alisema kocha huyo.
Aliongeza kwamba kabla ya kukutana leo na Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, alitarajiwa kukutana jana na katibu mkuu wa timu hiyo, Evodius Mtawala; ambaye ndiye huwasiliana naye mara kwa mara.
"Hata hivyo, naye aliahidi tutakutana leo (jana) asubuhi, lakini sijamuona na alisema kwamba anamsubiri Rage na Kaburu,"  aliongeza Milovan.
Akihojiwa juzi katika kipindi cha michezo cha Radio One, Rage alikiri kocha huyo kuidai Simba lakini akashangazwa na maamuzi yake (Milovan) kufuata malipo yake jijini Dar es Salaam wakati wao walimueleza kuwa watamtumia kwa njia salama za kibenki.
Milovan alitua jijini Jumatano wiki iliyopita na kulieleza gazeti hili kwamba amechukua maamuzi ya kufuata haki yake baada ya kuona ahadi alizopewa kwa njia ya simu hazitekelezwi na kwamba sasa, anafahamu kuwa klabu hiyo inazo fedha baada ya kumuuza kwa klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia aliyekuwa mshambuliaji wao wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi.
 

CHANZO:NIPASHE

MAN UNITED YAZIDI KUPAA ENGLAND, MAN CITY WAKATA TAMAA


VINARA wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Manchester United imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo baada ya kuendeleza wimbo lake la ushindi kwa kuilaza Everton mabao 2-0, huku wakishuhudiwa na kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho ambao watakutana na kikosi chake katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Timu hizo mbili zitakutana Jumatano katika mechi hizo za kuwania kutinga robo fainali za Ulaya, ambapo Mourinho ambao vijana wao jana walipata ushindi mnono wa mabao 4-1 dhidi ya Sevilla 
ipashia vema misuli Real Madrid na Cristiano Ronaldo wao kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Everton na kuzidi kupaa kileleni mwa Ligi Kuu England kwa pointi 12 zaidi.
Pamoja na Jose Mourinho kuushuhudia mchezo huo, Real Madrid inaonekana haitakuwa na kazi nyepesi mbele ya United ambayo leo ushindi wake umetokana na mabao ya Ryan Giggs na Robin van Persie.
Gap: Manchester United moved 12 points clear of rivals City at the top of the table
Wachezaji wa Manchester United wakishangilia

AZAM YAIKAMATA YANGA, WAISHINDILIA MTIBWA 4-1




Kikosi cha Azam  ambacho jana kiliendelea kushinda mechi zake kwa asilimia 100

TIMU ya soka ya Azam jana ilifanikiwa kuikamata Yanga kileleni baada ya kuizabua Mtibwa Sugar kwa mabao 4-1 katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara, huku mshambuliaji wake wa kimataifa, Kipre Tchetche akirejea dimbani kwa kishindo akifua mabao mawili kati ya hayo.
Azam ilipata ushindi huo katika mechi pekee iliyochezwa jana kwenye uwanja wa Manungu, Morogoro na kurejea rekodi kama hiyo waliyoipata mbele ya Mtibwa katika uwanja huo misimu miwili iliyopita.
Kipre Tchetche aliyekuwa majeruihi alirejea kwa kishindo katika kiosi cha Azam kwa kufunga mabao mawili, baada ya kushuhudiwa dakika 45 za kwanza zikiisha kwa sare ya baoa 1-1.
Bao la Azam la kwanza lilifungwa na Humphrey Aturdo kabla ya Vincent Barnabas wa Mtibwa kusawazisha na walipoanza kipindi cha pili, Mganda Brian Umony  alifunga bao la pili kabla ya Tchetche kutupia mengine mawili moja dakika za lala salama.
Kwa ushindi huo, Azam sasa wameikamta Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ya Bara baada ya kufikisha pointi 33, lakini wakiendelea kukamata nafasi ya pili kwa tofauti ya magoli. Yanga imefunga mabao 29 na kufungwa 12 wakati Azam wamefunga goli 27 na kufungwa 14.
Wenyewe Yanga watashuika dimbani siku ya Jumatano kuvaana na African Lyon katika pambano litakalochezwa uwanja wa Taifa, jijini Dar ambapo tayari wachezaji wa Yanga jana usiku waliingia kambini tayari kwa mchezo huo wakipania kupata ushindi.
Kwa mabao mawili ya jana Kipre Tchetche amefikisha jumla ya mabao 10 na kumzidi Mrundi wa Yanga, Didier Kavumbangu aliyesaliwa na mabao yake nane tangu duru lililopita.
Ligi hiyo itaendelea Jumatano kwa michezo mingine kadhaa mbali na huo wa Yanga na Lyon ambayo imeendelea kugawa pointi kwa wapinzani wao tangu duru la pili lianze.

NIGERIA BINGWA MPYA WA AFRIKA YAIZIMA BURKINA FASO


Cup of joy: A jubilant Nigeria squad hoist the Africa Cup of Nations trophy aloft for the third time
Wachezaji wa Nigeria wakishangilia Kombe lao la Mataifa ya Afrika baada ya kuifunga Burkina Faso kwenye Fainali nchini Afrika Kusini jana.Fancy seeing you again: Nigeria coach Stephen Keshi grabs the Africa Cup of Nations trophy after winning the competition as a player in 1994
Kocha wa Nigeria, Stephen Keshi akiwa ameshika Kombe ambalo awali alitwaa akiwa mchezaji mwaka 1994Warm welcome: FIFA president Sepp Blatter was made to feel at home in Johannesburg
Rais wa FIFA, Sepp Blatter wa pili kutoka kulia alikuwepo Johannesbug jana, chini mashabiki wakiwa na bango na kuonyesha upendo wa Waafrika kwake
Warm welcome: FIFA president Sepp Blatter was made to feel at home in South Africa
Winner: Sunday Mba is congratulated by Nigeria team-mates after firing the only goal of the game
Sunday Mba akipongezwa na wenzake kwa kufunga bao la ubingwa
No holds barred: Burkina Faso's Mady Panandetiguiri clashes with Nigeria keeper Vincent Enyeama
Mchezaji wa Burkina Faso, Mady Panandetiguiri akivaana na kipa wa Nigeria, Vincent Enyeama
Outnumbered: Nigeria's Victor Moses scraps for possession with Burkina Faso's Bakary Kone (centre), Mohamed Koffi (back) and Djakaridja Kone (right)
Mchezaji wa Nigeria, Victor Moses akipambana na ukuta Burkina Faso, Bakary Kone (katikati), Mohamed Koffi (nyuma) na Djakaridja Kone (kulia)

NCHI ya Nigeria jana usiku ilifanikiwa kutwaa ubingwa wa Afrika ikiwa ni kwa mara ya kwanza tangu miaka 19 na taji la tatu kwa nchi hiyo baada ya kuifunga Burkina Faso bao 1-0 katika fainali kali iliyopigwa kwenye Uwanja wa FNB(Soccer City), Johannesburg, Afrika Kusini.
Shujaa wa Nigeria kwa mechi ya jana alikuwa ni Sunday Mba aliyefunga bao hilo pekee la ushindi dakika ya 40, baada ya kutokea purukushani kwenye lango la Burkina Faso.
Burkina Faso ambayo hiyo ndiyo fainali yake ya kwanza kucheza tangu ilipoanza kushiriki michuano hiyo, ilipigana kutaka kurudisha bao hilo, lakini bahati haikuwa yao na hivyo kujikuta wakijifuta machozi kwa kushika nafasi ya pili.
Nigeria ilitwaa taji la michuano hiyo mwaka 1980 na 1994 na baada ya hapo ilikuwa ikishuhudia mataifa mengine yakinyakua kabla ya mwaka huu ikiwa chini ya kocha mzawa Stephen Keshi aliyenyakua taji la mwisho mwaka 1994, kuibebesha taji hilo akiweka rekodi ya kuwa kocha wa 15 mzawa kubebea taji hilo dhidi ya 14 ya makocha wa kigeni wa nchi mbalimbali katika michuano hiyo ya Afrika.

NJIKU KUWANIA TAJI LA PST SIKU YA WAPENDANAO



Mabondia Omary Ramadhani kushoto na Deo Njiku wakitunishiana misuri baada ya kusaini mkataba kupigania ubingwa wa Tanzania PST siku ya February 14 katika ukumbi wa Friends Corner Hotel Manzese picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
MABONDIA Deo Njiku wa Morogoro na Omary Ramadhani wataingia uringoni  February 14 katika ukumbi wa Friends Corner Hotel Manzese 14 kuwania Ubingwa wa Tanzania PST 


Mpambano huo wa aina yake unatarajiwa kuwa wa kusisimua kutokana kila mtu kuwa na rekodi nzuri mpambano uho utakaosindikizwa na mpambano mwingine wa ubingwa kati ya  Godfrey Silver na Adam Yahya ambapo mipambano hiyo itakuwa ya raundi kumi
Huku kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Nchini, Rajabu Mhamila 'Super D' atampandisha kwa mara ya kwanza bondia wake mpya Iddy Mnyeke kuvaana na Sadiki Momba mpambano utakaopigwa kwa raundi nne

Mgeni rasmi siku hiyo anatsrahjiwa kuwa ni Kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi wa kinondoni Charles Kenyela atakaewafisha mikanda ya ubingwa

Super D, alisema katika mpambano huo atasambaza DVD zake mpya tofauti na kanda yake ya awali iliyokwenda kwa SUPER D BOXING COACH, DVD za sasa zimeandaliwa kisasa na zikiwa na mchanganyiko wa ‘clips’ za michezo ya nyota wa Dunia katika kuwafunza watu namna ya kupigana ngumi.Super D, alisema mbali na michezo ya nyota hao wa Dunia akiwemo Manny Pacquio,Juan Emanuel Marquez, Floyd Maywether, Roy Jones na wakali wengine DVD hizo zina.  michezo
ya tamasha lao la ngumi wanaloendesha kwa kushirikiana na kocha mkongwe Habibi Kinyogoli.”katika muendelezo wa kuwafunza watu ngumi kwa njia rahisi, nimetoa dvd pamoja na CD nyingine tofauti zilizokusanya michezo ya mabingwa wa dunia na mafunzo ya ngumi tunayoendesha kupitia tamasha letu na Kinyogoli Foundition ” alisema.
 Super D ambae ni kocha wa timu ya ngumi ya Ashanti pamoja na timu ya mkoa wa Ilala kimichezo alisema anamini kupitia njia  hii watu wengi wenye kupenda kujifunza mchezo wa ngumi kwa kuangalia mbinu na ufundi katika mchezo huo kupitia michezo ya mabondia waliopo kwenye dvd hizo.   
Aliongeza kuwa, mbali na dvd hizo bado wanaitajika vijana wenye vipaji kujitokeza kuja kushiriki katika mazoezi ya ngumi ili wajiunge na wenzao wa
timu ya Ashanti na Amana kujifunza ‘live’ chini ya makocha Habibu Kinyogoli, Kondo Nassoro, na yeye mwenyewe Super D na wengine wanaowanoa vijana