STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 6, 2013

HII NDIYO ORODHA YA WANAOWANIA TUZO ZA TASWA 2012

Majina ya wanaowania kwa mwaka 2012:
MPIRA WA MAGONGO-WANAUME
1    Sylvester Kigodi
2.   Casto Mayuma
3.   Gurtej Bilu Singh
4.   Vendri Bhamra
5.  Elias Samala
Gofu ya Kulipwa 
1 Hassani Kadio 
   2 Yassin Salehe
  3 Fadhili Nkya
  4 Salimu Mwanyenza
  5 Rajabu Iddy
GOFU YA RIDHAA WANAWAKE:
1:MADINA IDDI
2:ANGEL EATON
3. HAWA WANYECHE
4.AYNE MAGOMBE
GOFU YA RIDHAA WANAUME
Jimmy Mollel
Frank Roman
Nuru Mollel
Martin MacDonald
John Said
NGUMI ZA RIDHAA-WANAUME
  1. Ismail Isack Galiatano
  2. Said Hofu
  3. Selemani Kidunda
  4. Victor Njaiti
  5. Mohamed Chibumbui
NGUMI ZA RIDHAA WANAWAKE:-
1.   Sara Andrew
2.   Irene Kimaro
3.   Easter Kimbe.
4.   Mather George
5.   Mariam Nyerere.
Ngumi za Kulipwa
1.      Francis Miyeyusho
2.     Ramadhan Shauri
3.     Thomas Mashali
4.     Said Mbelwa
5.     Francis Cheka
JUDO-TANZANIA BARA-WANAUME
1)     AHMED MAGOGO
2)    ADREW THOMAS MLUGU
3)    GEOPHREY EDWARD MTAWA
4)    GERVAS LEONARD CHILIPWELI
5)    ABUU SELEMANI MCHETEKO
6)   ABUUBAKAR NZIGE
JUDO TANZANIA BARA WANAWAKE
                             
1.     MATRIDA .H. TEMBA
2.     AMINA MOHAMED
JUDO ZANZIBAR-WANAUME
1.    MOHAMMED KHAMIS JUMA
2.   MASOUD AMOUR KOMBO
3.   MBAROUK SULEIMANI SULEIMAN
JUDO ZANZIBAR-WANAWAKE
1.     GRACE ALPHONCE
2.     LAYLATI MOHAMMED
TENISI-WANAWAKE
 [1] Rehema Athumani
[2] Vailety Petar
 [3] Mkunde iddi
 [4] Edna John
 [5] Zuhura Baraka
TENISI  Wanaume
 [1] Omary Abdalah
 [2] Yassini Shabani
 [3] Hassan Kasimu
 [4] Kiango Kipingu
 [5] Lebric Jacobu
MPIRA WA MIKONO-WANAUME
Faraji Shaibu
Nyuki ZANZIBAR
Hemedi Salehe
JKT
Abinery  Kusena
JKT
Ally Khamis
Ngome
Hassani  Yusufu
Magereza
MPIRA WA MIKONO-WANAWAKE
Catherine    Mapua
Ngome
Dorisi        Mangara
Magereza
Zakia        Mohamed
Ngome
Happy      Mahinya
JKT
Mary       Kimiti
Magereza
RIADHA-WANAWAKE
1.Zakia Mrisho
2. Mary Naali
 3.Jacklin Sakilu
4.Sarah Ramadhani  
 5.Anjelin Tsere
6. Sara Maja
RIADHA-WANAUME
1. Dickson Marwa
 2. Faustine Musa
3. Augstino Sule
4. Bazil John
5. Samson Ramadhan
KRIKETI-WANAUME
1.   Abhik Patwa.
2.     Benson Mwita.
3.     Sefu Khalifa.
4.     Issa Kikasi.
5.   Riziki Kiseto
KRIKETI-WANAWAKE
Monica Pascal.
Mwanaiddi Ibrahim.
Hadija Nasibu
Esther Wales
Mwanaidi Ammy
SOKA-WANAWAKE
FATUMA MUSTAPHA
ASHA RASHID
MWANAHAMISI OMARY
SOPHIA MWASIKILI
ESTER CHABRUMA
SOKA-WANAUME
JOHN BOCCO-AZAM
KELVIN YONDANI-YANGA
SHOMARI KAPOMBE-SIMBA
MCHA KHAMISI-AZAM
MBWANA SAMATTA-TP MAZEMBE
Thomas Ulimwengu-TP Mazembe
WACHEZAJI WA NJE WANAOCHEZA TANZANIA
EMMANUEL OKWI-SIMBA(SASA ETOILE DU SAHEL)-SOKA
KIPRE TCHETCHE-AZAM-SOKA
HARUNA NIYONZIMA-YANGA-SOKA
HAMISI KIIZA-YANGA-SOKA
MARY WAYA-FILBERT BAYI –NETIBOLI (ALIKUWA KOCHA MCHEZAJI)
KIKAPU-WANAWAKE
Faraja Malaki- Jeshi
Evodia Kazinja-JKT Stars
            Sajida Ahmed-Don Bosco
           Rehema Kilomba-Donbosco
        Tukusubira David-Vijana Queens
KIKAPU-WANAUME
Mussa Chacha-Savio
Lusajo Samuel Mwakipunda-Oilers
Salim Mchemba-ABC
Filbert Mwaipungu-ABC
Steven Atanasio-ABC
NETIBOLI
Lilian Sylidion-Filbert Bayi
Mwanaidi Hassan-JKT
Irene Elias Kanile-Filbert Bayi
Jacqueline Sikozi-Filbert Bayi
Faraja Malaki-Jeshi Stars
WACHEZAJI BORA CHIPUKIZI
Salum Abubakari-Azam-soka
Frank Domayo-Yanga-soka
Edward Cristopher-Simba-soka
Emmanuel Malya-Tenisi Gymkhana Arusha
Tambwe Juma-Kriketi
WATANZANIA WANAOCHEZA NJE
Mbwana Samatta-TP Mazembe
Ivo Mapunda-Gor Mahia
Hasheem Thabeet-Oklahoma
Thomas Ulimwengu-TP Mazembe
Soud Abdulrazak-Uganda (kikapu)
Mohammed Abdallah ‘dulah’-Uganda (kikapu)
TUZO YA HESHIMA--- ITATANGAZWA UKUMBINI
TUZO YA MWANAMICHEZO BORA MWAKA 2012- ATAPATIKANA MIONGONI MWA WASHINDI WA KILA MCHEZO
Imetolewa na
Haji Manara
Mwenyekiti Kamati ya Tuzo TASWA
05/05/2013

Azam warejea, Hall ajifariji

Azam Fc

WAKATI kikosi cha timu ya soka ya Azam kilichokuwa kinashiriki mashindano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho kikirejea leo mchana kutoka Morocco, kocha wa timu hiyo, Stewart Hall amesema kwamba wachezaji wake walipambana kusaka ushindi wa ugenini lakini bahati haikuwa yao.
Azam iliyotoka suluhu katika mechi ya ya kwanza hapa nyumbani, juzi ilifungwa magoli 2-1 na AS FAR Rabat ya Morocco katika mechi ya marudiano ya raundi ya pili ya michuano hiyo na kutolewa.
Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Morocco jana mchana, Hall alisema kwamba wanaheshimu matokeo hayo na wanaamini kwamba mwakani wakipata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa watafanya vizuri zaidi ya msimu huu.
Hall alisema kwamba mchezo ulikuwa mgumu katika vipindi vyote na timu zote zilitengeneza nafasi lakini washambuliaji hawakuwa makini na kushindwa kutumia nafasi hizo.
"Tulipambana na tulijitahidi kuwakabili lakini matokeo hayakuwa mazuri katika upande wetu, ila wachezaji na mimi mwenyewe kuna mambo tumejifunza yatakayotusaidia kwa ligi ya nyumbani na mashindano mengine ya kimataifa tutakayoshiriki," alisema Muingereza huyo.
Afisa Habari wa timu hiyo, Jaffer Idd, alisema kuwa kikosi cha timu hiyo kitatua nchini saa 9:00 mchana kwa ndege ya Shirika la Ndege la Emirates ambapo jana usiku walilala Dubai.
Alisema wachezaji na viongozi wote waliokuwa kwenye safari hiyo wako salama na wanarejea nchini na nguvu mpya kuhakikisha wanashinda mechi za Ligi Kuu ya Tanzania Bara zilizobaki.
Azam iliyoshiriki kwa mara ya kwanza michuano hiyo inayoandaliwa na Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) ilifika raundi ya pili baada ya kuzitoa Al Nasri ya Sudan Kusini na baadaye Barrack Young Controllers ya Liberia.
Chanzo: NIPASHE

Floyd Mayweather Jr akata ngebe za Robert “The Ghost” Guerrero

Bondia Floyd Mayweather Jr kushoto akimrushia ngumi mfululizo Robert “The Ghost” Guerrero wakati wa mpambano wao uliofanyika alfajiri ya leo
Bondia Robert “The Ghost” Guerreroakiwa chini baada ya kupata konde zito kutoka kwa Floyd Mayweather Jr  wakati wa mbambano wao uliofanyika alfajiri ya leo maywether alishinda mpambano uho kwa point
Bondia Floyd Mayweather Jr kushotoakioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Robert “The Ghost” Guerrero wakati wa mpambano wao maywether alishinda kwa point

Warembo 28 kuchuana Miss Utalii Tanzania jijini Tanga

Warembo wa Miss Utalii Tanzania wakiwa katika pozi

JUMLA ya warembo 28 wanatarajiwa kuchuana kwenye shindano la kuwania taji la urembo la taifa la utalii, 'Miss Utalii Tanzania', litakalofanyika Jumapili ijayo (Mei 12) mkoani Tanga.
Warembo tayari wameshatua mkoani Tanga kujiandaa na fainali hizo ambazo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Khamis Kagasheki.
Akizungumza kwa simu kutoka Tanga, Rais wa Miss Utalii Tanzania, Gideon Chipungahelo alisema kuwa maandalizi ya shindano hilo yamekamilika na kwamba warembo watakaochuana wanaendelea vyema na maandalizi.
Chipungahelo maarufu kama 'Chipps' alisema walishatuma barua ya mualiko katika ofisi ya Waziri wa Maliasili na Utalii kwa ajili ya kumuomba waziri awe mgeni rasmi na wakati wanasubiri majibu, ni matarajio yao kwamba atawakubalia ombi lao.
"Tunatarajia Waziri Dk Kagasheki ndiye atakayekuwa mgeni rasmi wa fainali zetu kwani tumeshatuma ombi na barua ya mualiko katika ofisi yake na kwa sasa tunasubiri majibu," alisema.
Chipps alipoulizwa sababu ya kupungua kwa idadi ya washiriki wa shindano hilo kutoka 40 hadi 28, alisema imetokana na baadhi ya warembo kukatishwa tamaa na danadana za kufanyika kwa fainali hizo kulikosababishwa na ahadi zilizoyeyuka za wadhamini wao.
"Idadi imepungua kwa vile wengine walikata tamaa walipoona fainali zikibadilika tarehe kila mara baada ya wadhamini na wafadhili tuliokuwa tukiwategemea kutuacha solemba kabla ya kupigwa tafu na kulihamishia Tanga badala ya kufanyika jijini Dar es Salaam," alisema.

Kalapina halingani na zogo la mtaa

Kalapina katika pozi

MSANII nyota wa miondoko ya Hip Hop nchini, Karama Masoud 'Kalapina' ameachia nyimbo mbili mpya ambazo alitarajiwa kuzitambulisha rasmi jana kwa mashabiki wake katika tamasha lililofanyika jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO juzi, Kalapina anayeliongoza kundi la Kikosi cha Mizinga, alisema nyimbo mpya ni 'Zogo la Mtaa' na 'Hawalingani na Sisi', alizorekodia katika studio za Kikosi Records.
Kalapina alisema wimbo wa 'Zogo la Mtaa' ameuimba kwa kushirikiana na Suma Labu na Gwalu wakati ule wa 'Hawalingani na Sisi' ameimba kwa kushirikisha wasanii walioibuliwa na kukuzwa na familia ya Kikosi yenye  maskani yake maeneo ya Kinondoni kama Sam Flezy, Zimwi na Abuu Gaidi.
Mkali huyo aliyewahi kutamba na nyimbo kadhaa kama 'Harakati', 'Kufa na Kupona', 'Lawama', 'Maisha Yangu Muziki Tosha' na nyingine, alisema nyimbo hizo ni salamu kwa mashabiki wake kwa mwaka 2013 akiwa amepania kuwapa burudani zaidi pamoja na uhamasishaji katika harakati za kujikomboa.
Kalapina pia alisisitiza juu ya mipango yake ya kutaka kuwania kiti cha ubunge Jimbo la Kinondoni ambalo kwa sasa linashikiliwa na Idd Azan wa CCM.
Katika uchaguzi uliopita msanii na mwanaharakati huyo aliwania kiti cha udiwani Kata ya Kinondoni kupitia Chama cha CUF na kushindwa kwa kura chache na mpinzani wake kupitia CCM

Stars kuanza kibarua COSAFA Julai 6

 
Taifa Stars
Na Boniface Wambura
TIMU ya taifa ya soka, Taifa Stars imepangwa kundi A la michuano ya Kombe la COSAFA ambapo itacheza mechi yake ya kwanza Julai 6 mwaka huu jijini Lusaka, Zambia dhidi ya Shelisheli.

Upangaji ratiba (draw) wa mashindano hayo ulifanyika juzi (Mei 3 mwaka huu) jijini Lusaka ambapo timu nyingine zilizo na Taifa Stars katika kundi hilo ni Namibia na Mauritius. Kundi la Taifa Stars litachezea mechi zake jijini Lusaka.

Mechi ya pili ya Taifa Stars katika hatua ya makundi itakuwa Julai 8 mwaka huu dhidi ya Mauritius. Mechi ya mwisho katika hatua hiyo itakuwa Julai 10 mwaka huu dhidi ya Namibia.

Kundi B lina timu za Kenya (Harambee Stars), Botswana (Zebras), Lesotho na Swaziland. Hatua itakayofuata baada ya hapo ni ya mtoano (knockout) na kila kundi litatoa timu moja tu.

Iwapo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itafuzu kwa hatua itakayofuata itacheza Julai 13 mwaka huu na Afrika Kusini (Bafana Bafana) ambayo pamoja na timu nyingine tano zimekwenda moja kwa moja katika hatua ya mtoano.

Nyingine zilizokwenda moja kwa moja hatua ya mtoano ni wenyeji Zambia, Angola, Zimbabwe, Msumbiji na Malawi ambazo kwenye viwango vya ubora vya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ziko juu ya zile zilizoanzia hatua ya makundi.

Kwa mujibu wa ratiba hiyo, fainali ya michuano ya Kombe la COSAFA itafanyika Julai 20 mwaka huu.

Ratiba Ligi ya Mabingwa wa Mikoa kupangwa kesho, kivumbi kuanza J2

 
Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura

Na Boniface Wambura
UPANGAJI wa ratiba ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) uliokuwa ufanyike juzi (Mei 3 mwaka huu), sasa utafanyika Jumanne (Mei 7 mwaka huu) na ligi hiyo itaanza Mei 12 mwaka huu kama ilivyopangwa.

Uamuzi huo umefanya na Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana leo (Mei 5 mwaka huu) kujadili maandalizi ya ligi hiyo, yakiwemo maombi ya baadhi ya mikoa ambayo haijamaliza yao kutaka RCL isogezwe mbele.

Kamati ya Mashindano chini ya Uenyekiti wa Blassy Kiondo ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF ilipitia maombi hayo na kuangalia athari ambazo zinaweza kujitokeza huko mbele iwapo RCL itasogezwa mbele.

Baadhi ya athari iwapo RCL itasogezwa mbele ni timu zitakazopanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kutopata muda wa kufanya usajili wa wachezaji kwa msimu mpya.

Hivyo draw hiyo itakayofanyika saa 6 mchana itahusisha mikoa ambayo tayari imemaliza ligi na kuwasilisha majina ya mabingwa wao. Mabingwa ambao wamewasilishwa na mikoa yao kwenye mabano ni Abajalo SC (Dar es Salaam 2), Biharamulo FC (Kagera), Flamingo SC (Arusha), Friends Rangers (Dar es Salaam 3), Katavi Warriors (Katavi), Kiluvya United (Pwani), Kimondo FC (Mbeya) na Machava FC (Kilimanjaro).

Mingine ni Magic Pressure FC (Singida), Mbinga United (Ruvuma), Mji Njombe (Njombe), Polisi Jamii Bunda FC (Mara), Red Coast FC (Dar es Salaam 1), Rukwa United (Rukwa), Saigon FC (Kigoma), TECKFOLT FC ya Kilombero ambayo ni Shule ya Sekondari (Morogoro) na UDC FC ya Ukerewe (Mwanza).

Ada ya ushiriki ni sh. 100,000 wakati usajili wa wachezaji wa timu hizo ni uleule uliofanyika katika Ligi ya Mkoa na unatakiwa kuwasilishwa TFF kwa ajili ya uthibitisho. TFF inapenda kusisitiza kuwa hakuna usajili mpya wa wachezaji kwa ajili ya ligi hiyo.

Mikoa iliyoshindwa kuwasilisha mabingwa wake ni Dodoma, Geita, Iringa, Lindi, Manyara, Mtwara, Shinyanga, Simiyu, Tabora na Tanga.

Tuzo za Taswa zafikia patamu majina yatangazwa

John Bocco 'Adabayor' anayawania tuzo ya Mwanasoka Bora

Emmanuel Okwi anayewania tuzo ya mwanasoka bora kutoka nje ya nchi


WASHAMBULIAJI Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wa klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na John Bocco wa Azam ni miongoni mwa nyota sita walioteuliwa kuwania "Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka 2012" inayoandaliwa ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) itakayotolewa mwezi ujao, imefahamika.
Taarifa iliyotolewa jana na mwenyekiti wa kamati ya TASWA kusimamia tuzo za wanamichezo bora wa Tanzania mwaka 2012, Haji Manara, iliwataja nyota wengine waliong'ara katika kipengele cha kuwania tuzo ya mwanasoka bora kuwa ni mshambuliaji Mcha Khamis wa Azam, beki Kelvin Yondani (Yanga) na beki kisiki wa Simba, Shomari Kapombe ambaye atakuwa akiiwania tuzo hiyo kwa mara ya pili mfululizo.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa majina ya nyota hao wa soka wanaume yamependekezwa na kamati ya tuzo baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutowapatia majina hayo. Nyota wa michezo mingine waliopendekezwa kuwania tuzo (isipokuwa mpira wa kikapu), wote  wamependekezwa na vyama vyao na hafla ya kutangaza washindi na kuwapa zawadi itafanyika mwanzoni mwa Juni.
Kwa soka la wanawake, walioteuliwa kuwania tuzo ni Fatuma Mustafa, Asha Rashid,
Mwanahamisi Omar, Sophia Mwasikili na Ester Chabruma 'Lunyamila'.
Nyota wanaowania tuzo katika kipengele cha wachezaji wa nje wanaocheza Tanzania ni Emmanuel Okwi aliyekuwa Simba (sasa Etoile du Sahel ya Tunisia), Kipre Tchetche(Azam),
Haruna Niyonzima (Yanga), Hamis Kiiza (Yanga) na mcheza netiboli Mary Waya wa klabu ya Filbert Bayi.
Wachezaji wanaowania "Tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi wa Mwaka 2012" ni
Salum Abubakar 'Sure Boy' (Azam), Frank Domayo (Yanga), Edward Cristopher (Simba), mcheza tenis Emmanuel Malya wa klabu ya Gymkhana ya Arusha na mcheza kriketi Tambwe Juma.
Majina ya Samatta na Ulimwengu yamejitokeza pia katika kipengele cha wanaowania tuzo ya mchezaji bora Mtanzania anayecheza nje ya nchi. Wengine wanaowania tuzo hiyo ni kipa Ivo Mapunda-wa klabu ya soka ya Gor Mahia inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya, nyota wa mpira wa kikapu Hasheem Thabeet anayecheza Oklahoma City Thunder inayoshiriki Ligi Kuu ya Marekani (NBA), mchezaji wa mpira wa kikapu Soud Abdulrazak (Uganda) na Mohamed Abdallah ‘Dulah’ ambaye pia anacheza mpira wa kikapu nchini Uganda.
Wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa mpira wa magongo (wanaume) ni Sylvester Kigodi, Casto Mayuma, Gurtej Bilu Singh, Vendri Bhamra na Elias Samala wakati nyota wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa gofu ya kulipwa ni Hassan Kadio, Yassin Salehe, Fadhili Nkya, Salim Mwanyenza na Rajabu Iddy.
Walioteuliwa kuwania tuzo ya mchezaji bora wa ridhaa wa gofu (wanawake) ni Madina Iddi, Angel Eaton, Hawa Wanyanche na Ayne Magombe. Nyota wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa gofu ya ridhaa wanaume ni Jimmy Mollel, Frank Roman, Nuru Mollel,
Martin MacDonald na John Said.
Katika ngumi za ridhaa (wanaume), walioteuliwa kuwania tuzo ni Ismail Isack Galiatano, Said Hofu, Selemani Kidunda, Victor Njaiti na  Mohamed Chibumbui wakati ngumi za ridhaa wanawake ni Sara Andrew, Irene Kimaro, Easter Kimbe, Mather George na Mariam Nyerere.
Nyota wanaowania tuzo ya mwanamichezo bora wa ngumi za kulipwa ni Francis Miyeyusho, Ramadhan Shauri, Thomas Mashali, Said Mbelwa na Francis Cheka.
Katika mchezo wa judo (wanaume), wanaowania tuzo ni Ahmed Magogo, Andrew Thomas Mlugu,  Geofrey Edward Mtawa, Gervas Leonard Chilipweli, Abuu Selemani Mcheteko na Aboubakar Nzige. Judo wanawake Tanzania Bara ni Matrida Temba, Amina Mohamed wakati judo wanaume Zanzibar ni Mohamed Khamis Juma, Masoud Amour Kombo, Mbarouk Suleiman Suleiman. Judo wanawake Zanzibar ni Grace Alphonce na Laylat  Mohamed.
Wanaowania tuzo ya mcheza tenis bora (wanawake) ni Rehema Athumani, Vailety Petar, Mkunde iddi, Edna John na Zuhura Baraka huku tenis wanaume wakiwa ni Omary Abdallah, Yassin Shaaban, Hassan Kassim, Kiango Kipingu na Lebric Jacobu.
Ushindani mkali unatarajiwa kuonekana katika kumpata mshindi wa tuzo ya mwanariadha bora wa kike ambayo watakaochuana ni Zakia Mrisho, Mary Naali, Jacklin Sakilu, Sarah Ramadhani, Sara Maja na Anjelin Tsere. Wanariadha wa kiume wanaowania tuzo ni Dickson Marwa, Faustine Mussa, Augstino Sule, Bazil John na Samson Ramadhan.
Michezo mingine ambayo tuzo zake zitawaniwa ni mpira wa mikono, kriketi, mpira wa kikapu na netiboli ambayo itawaniwa na Lilian Sylidion wa Filbert Bayi, Mwanaidi Hassan (JKT), Irene Elias Kanile (Filbert Bayi), Jacqueline Sikozi (Filbert Bayi) na Faraja Malaki wa Jeshi Stars.
"Tuzo ya heshima itatangazwa ukumbini... mshindi wa tuzo ya mwanamichezo bora wa mwaka 2012 atapatikana miongoni mwa washindi wa kila mchezo," imesema sehemu ya taarifa hiyo ya Manara, ikifafanua zaidi kuwa sherehe zitafanyika mwanzoni mwa Juni.
Kapombe wa Simba ndiye aliyeibuka mshindi wa "Tuzo ya Mwanamichezo Bora wa TASWA Mwaka 2011". Wengine waliowahi kuibuka washindi wa jumla wa tuzo hiyo ni Mwanaidi Hassan (2009 na 2010), Mary Naali (2008), Martin Sulle (2007) na Samson Ramadhan (2006).