STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 16, 2013

Ntiro, Nyagawa waibeba Golden Bush Veterani wakiilaza Mburahati Veterani 3-2

Onesmo Waziri 'Ticotico' akimiliki mpira langoni mwa Mburahati, huku Salum Swedi (11) akiwa tayari kutoa msaada.

Hekaheka langoni mwa Mburahati baada ya Machota (2) kukaribia kufunga bao

Peter Kalumbeta (kushoto) akitafuta mbinu za kumtoka Shija Katina wa Golden Bush

Mohammed wa Mburahati akichuana na Shomari

Nico Nyagawa 'akikusanya kijiji' kwa kuwatoka wachezaji wa Mburahati Veterani
Faraji wa Golden Bush (kulia) akikokota mpira huku akifuatwa na beki wa Mburahati huku Abuu Ntiro akiwa tayari kumsaidia wakati timu zao zilipoumana asubuhi ya leo.
Wachezaji wa Golden Bush Veterani wakati wa mapumziko
 
Kudra Omar wakati wa mapumziko
Nico Nyagawa akitafakari wakati wa mapumziko
Onesmo Waziri 'Ticotico' akichuana na wachezaji wa Mburahati huku Nahodha wake Yahya Issa akiwa makini kumsaidia

Yahya Issa akiambaa na mpira mbele ya mchezaji wa Mburahati
Salum Swedi (11) akiambaa na mpira huku akichungwa na beki wa Mburahati Veterani

Mshambuliaji nyota wa zamani Atufugwegwe Mwakalukwa (kushoto) akiwa na wachezaji wenzake wa Mburahati nje ya uwanja
Benchi la timu ya Mburahati Veterani wakiwa hawaamini kama Golden Bush wamewashika leo kwenye uwanja wa Chuo Kikuu

Mchezaji wa Mburahati akiambaa na mpira huku mwenzake akiwa makini kumsaidia

Peter Kalumbeta wa Mburahati (kulia) akimtoka beki wa Golden Bush
WAKATI vijana wao jana kulala mabao 2-0 mbele ya Simba, timu ya Golden Bush Veterani leo asubuhi wamejifariji baada ya kuinyuka Mburahati Veterani kwa magoli 3-2 katika mchezo wa kirafiki.
Vijana wa Golden Bush walilala kwa Simba katika pambano lililochezwa jana jioni kwenye uwanja wa Kinesi, lakini wazee wao walifanya kweli viwanja vya Chuo Kikuu Dar es Salaam.
Golden Bush Veterani ambayo wiki kadhaa ilikuwa 'baba huruma' kwa kuchezea vipigo kwa wapinzani wao, walianza kuandika bao katika kipindi cha kwanza kupitia Abuu Ntiro.
Licha ya Golden Bush iliyosheheni nyota waliowahi  kutamba nchini kama ivo Mapunda, Salum Swedi 'Kussi', Nico Nyagawa, Yahya Issa, Kudra Omar, Wisdom Ndlhovu, Steven Marashi na wengine kusakama lango la Mburahati matokeo yalibaki bao 1-0 hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko ya wachezaji na kwa kiasi fulani ilibadili kasi na Mburahati ilifanikiwa kusawazisha bao kupitia shuti kali lililopigwa na Peter Kalumbeta.
Hata  bao hilo lilidumu kwa dakika moja tu kwani Nico Nyagawa alifunga bao la pili la Golden Bush akimalizia kazi nzuri ya Shoamri aliyepanda mbele.
Winga msumbufu wa Mburahati Ally 'Neymar' alifunga bao la kusawazisha kwa timu yake baada ya kuwatoka mabeki wa Golden Bush na kupiga shuti lililomshinda kipa Steven Marashi.
Dakika za lala salama baada ya kulilia kuingizwa dimbani, Machota alionyesha hakulilia bure kucheza mechi hiyo kwani aliiandikia Golden Bush bao la tatu na la ushindi kwa kichwa akimalizia krosi safi ya De Natale.
Mbuharati alikaribia kupata bao la kusawazisha kama sio uzembe uliofanywa na winga wao wa kulia, Karume kushindwa kutumbukiza wavuni mpira akiwa yeye la lango kufuatia kroshi ya 'Neymar'.
Mpaka filimbi ya mwamuzi Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio' ikilia kuashiria mwisho wa pambano hilo Golden Bush waliibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 3-2 mbele ya wapinzani wao, Mburahati iliyowakosa baadhi ya nyota wao kama Abdul na Juma Chilumba na Atufugwegwe Mwakalukwa katika mchezo huo.

Arusha sasa ni 'vita', Mbunge Nassari apigwa na kujeruhiwa Monduli


Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari muda huu amepigwa na kujeruhiwa vibaya damu zinamtoka Puani, amepigwa na vijana wa kisomali, katika eneo la Zaburi kata ya Makuyuni Jimbo la Monduli, Taarifa za awali zinasema baada ya Nassari kuondoka na gari  jingine, waliokuwa wanafuatana naye walienda kujibanza sehemu.

Kiongozi wa Chadema aliyetambulika kwa jina la Teddy Ndossi na dereva wa Nassari. Dereva wa Nassari Guardian  Palangyo amepigwa mdomoni amevunjwa meno mawili, na kwa sasa wamempiga Katibu wa Chadema wa eneo hilo anayeitwa Kilongola, wapo Kituo cha Polisi Makuyuni kutafuta msaada zaidi.
Picha na taarifa zaidi zitawajia baadae.
Credit:Udaku Specially

Saturday, June 15, 2013

Watatu wafa wa bomu mkutano wa CHADEMA




Uwanja wa Soweto ambapo Mkutano wa Chadema kufunga kampeni za kuwania Udiwani Kata ya Kaloleni Jijini Arusha ulikuwa unafanyika umegeuka kuwa uwanja wa vilio baada ya kinachodhaniwa kuwa bomu kulipuka na kuua watu watatu na zaidi ya 50 kujeruhiwa vibaya huku baadhi yao wakiwa wamevunjika miguu.
Katika Mkutano huo walikuwapo pia Mwenyekiti wa Chadema na  Mbunge wa Arusha Mjini, Mh Godbless Lema sambamba na viongozi wengine wa Chadema Mkoa wa Arusha lakini bahati nzuri Mbowe na Lema   hawakudhurika moja kwa moja na mlipuko huo.

Mlipuko huo ulitokea mbele ya gari ambalo lilikuwa ni jukwaa la matangazo mara  tu baada ya Mh Mbowe, Lema na viongozi wote waliokuwa jukwaa kuu kushuka chini na kujichanganya katikati ya watu wakikusanya michango ya watu, hali inayoashiria mrushaji huenda alilenga kuwajeruhi viongozi hao.

Miili ya marehemu na majeruhi walipelekwa hospitali ya Mt Meru lakini hawakupokelewa baada ya kilichoelezwa ni vurumai iliiyoletwa na mamia ya wafuasi wa Chadema waliokuwa na hasira baada ya wenzao kuuawa.

Hali ikiwa bado tete viwanjani hapo, magari kadhaa ya askari polisi yalifika huku askari wakiwa na silaha lakini walilazimika kupiga mabomu ya machozi kadhaa hewani na kisha kuondoka kutokana na baadhi ya wananchi waliokuwa na hasira kuwafuata na kupaza sauti wakitaka wawaue pia.

Kijana mmoja muuza machungwa aliieleza blogu hii kuwa aliyerusha bomu hilo alitokea upande wa nyuma ya jukwaa kuu na baadae kukimbilia nyumba zilizo jirani.
DSC07403
Mbowe - SowetoMwenyekiti wa Chadema, Mh Freeman Mbowe akiwasili viwanja vya Soweto, Kata ya Kaloleni Jijini Arusha jioni ya leo katika Mkutano wa Chadema kufunga kampeni zake.
DSC07401Mh Mbowe akichangisha pesa mkutanoni hapo sekunde chache kabla ya mlipuko kutokea
DSC07413Hali ilivyokuwa baada ya mlipuko ulioua na kujeruhi vibaya
DSC07407Hali za majeruhi na marehemu wakiwa chini kabla ya kukimbizwa hospitalini
DSC07408

Tamasha la Usiku wa Matumaini lanoga hawa kuzichapa Taifa

Ray atakayezipiga na Mhe. Zitto Kabwe
Mhe Zitto Kabwe atakayepigana na Ray

Mhe. Idd Azam atakayepigana na JB
JB Mpinzani wa Mbunge Idd Azan

Mhe Halima Mdee atakayepimana ubavu na Wolper
Wolper atakayechapana na Mhe. Mdee

Mhe Esther Bulaya
Aunty Ezekiel

KATIKA kunogesha Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika Julai 7 kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano watapanda ulingoni kuzichapa na wasanii wa Bongo Movie.
Kwa mujibu wa Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO) Yasin Abdallah 'Ustaadh' siku hiyo Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe atapanda ulingoni ili kuonyeshana kazi na Vincent Kigosi 'Ray' katika pambano la raundi nne.
Naye Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azan yeye  ataonyeshana kazi na Jacob Stephen 'JB'. wakati Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na Jacklyne Wolper wenyewe watapimana ubavu, kabla ya Ester Bulaya kuchapana na Aunty Ezekiel michezo yote hiyo pia ikiwa ya raundi nne.
Ustaadh, alisema katika kuhakikisha mabondia hao hawaumizani ulingoni watavishwa vifaa maalum vya kukinga vichwa vyao ili wasipate majeraha kichwani.
Rais huyo wa TPBO alisema mara baada ya mapambano hayo ya utangulizi, itashuhudiwa michezo miwili ya kimataifa kati ya mabondia Thomas Mashali na Francis Miyeyusho kuzichapa na Wakenya Patrick Amote na Shadrack Machanje.
Pia maboindia Ramadhani Mkundi atapanda ulingoni pia kupigana na Martin Richard, huku pia ikitarajiwa kuwepo kwa burudani mbalimbali za muziki na mchezo wa soka kati ya wabunge mashabiki wa Simba dhidi ya wale wenzao wa Yanga na Bongo Fleva kuumana na Bongofleva.
Ustaadh alisema michedzo hiyo iliyoandaliwa na Global Publishers ni maalum kwa ajili ya kuchanisha fedha za ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike na kutoa wito wadhamini na watu mbalimbali kujitokeza kwa wingi kuchangia na pia kuhudhuria tamasha hilo.

Hivi ndivo Jide 'Anaconda' alivyofunika Dar usiku wa jana

Mwanadada Judith Mbibo aka Lady Jaydee usiku wa kuamkia Jumamosi ya June 15 amefanikiwa kuweka historia kwenye muziki wa Tanzania kwa kulijaza eneo zima la Nyumbani Lounge alipokuwa akifanya show yake ya kuadhimisha miaka 13 tangu aanze muziki. 
DSC_4275

Katika show hiyo, Lady Jaydee amesindikizwa na wasanii mbalimbali wakiwemo Juma Nature, Sugu, Profesa Jay, Wakazi, Grace Matata na wengine. Pia Jaydee ameitumia siku hiyo kuzindua albam yake mpya, Nothing But The Truth na kusherehekea siku yake ya kuzaliwa. Hizi ni picha za show hiyo.

Umati wa watu unaoshuhudia show ya Lady J Dee sasa hivi hapa Nyumbani Longe.

Lady J Dee anatoa burudani ya kutosha kwa mashabiki.

Professa Jay akiwa back stage anajiandaa kupanda jukwaani kutoa burudani nzuri kwa mashabiki
 

Miaka 13 ya Lady j Dee#sasa hivi ndiyo Mh.Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu ameingia

Lady J Dee anatoa burudani ya kutosha kwa mashabiki.

Lady J Dee anatoa burudani ya kutosha kwa mashabiki.

Team Times Fm 100.5 (Dj Jors Bless,Ndimbo na Mariam)

Sugu na Mkoloni wanatoa burudani kali kwa mashabiki.

Mama mzazi wa Lady J Dee naye amekuja kushuhudia show ya mwanae.

Juma Nature anatoa burudani kwa mashabiki

Sugu akitoa burudani kali kwa mashabiki
M 2 The P akiongea machache baada ya kukaribishwa kwenye jukwaa na Juma Nature

Waziri Malima mgeni rasmi tamasha la wasanii Mkuranga

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh7svkFfS1FO4ul84Yj7YOFVUx2UQ5vnLtmrp1ethu9jlrAwt_84Vp70KCjvPSXRH7fygzPzAl0y2vxbU5mXxZL6LpG-fM4tvSSsV4avn8aP3EJeGTVhqjE0qvHj9UjjreaJwP5gLZwpPI4/s1600/AdamMalima.jpg
Naibu Waziri Adam Malima
Na Peter Mwenda
NAIBU Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Wasanii na mastaa  litakalofanyika Juni 29, kwenye kijiji cha Mwanzega, Mkuranga mkoa wa Pwani.

Akizungumza na viongozi wa Mtandao wa Wasanii (SHIWATA) mjini Dodoma katika vikao vya Bunge vinavyoendelea, Malima alisema amekubali kuwa mgeni rasmi vile vile tukio hilo linafanyika katika jimbo lake la uchaguzi la Mkuranga.

Mwenyekiti wa SHIWATA, Caasim Taalib alisema maandalizi ya tamasha hilo yanaendelea vizuri na kuongeza kuwa kutakuwa na matukio ya wanachama kukabidhiwa nyumba zao kwa wale waliomaliza michango yao akiwemo mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars, Jellah Mtagwa atakabidhiwa nyumba yake.

Alisema Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida ambaye alikuwa mgeni rasmi tamasha lililopita Mei mwaka huu Dar es Salaam na kuahidi kukarabati barabara za kuingia kijiji cha wasanii Mkuranga atakabidhiwa kadi pia taasisi yake ya ujasiriliamali ambayo itawakopesha wasanii wa SHIWATA sh. Bil. 7 kwa ajili ya kuendeleza wasanii, itaanza kutekeleza mpango huo wa Awamu ya Kwanza siku hiyo.

Alisema mbunge wa Kinondoni Bw. Idd Azzan naye atakabidhiwa kadi ya kujiunga na SHIWATA ambako pia wabunge mbalimbali wamealikwa kuhudhuria tamasha hilo akiwemo mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu, Mbunge wa Ilala, Mussa Zungu.

Wabunge wengine wa mkoa wa Dar es Salaam walioalikwa katika tamasha hilo ni John Mnyika wa Ubungo, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, na Mwenyekiti wa Taifa wa NCCR- Mageuzi , James Mbatia.

Alisema mtandao wa SHIWATA ambao umekuwa ukiandaa matamasha ya wasanii kila mwezi limepeleka tamasha la Juni kwenda wilaya ya Mkuranga ambako ndiko zinakojengwa nyumba zao katika kijiji cha Mwanzega-Kimbili ambako mpaka sasa watu nane watakabidhiwa nyumba zao.

Wasanii 400 kutoka vikundi mbalimbali vikiwemo vya mkoa wa Pwani wanatarajiwa kushiriki katika tamasha hilo .

Wanachama wa SHIWATA nao wanakaribishwa kuhudhuria tamasha hilo.

Mwisho