STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 30, 2013

SHEREHE YA WAFANYAKAZI WA IPP MEDIA ZILIZOFANA JANA


Watu walikuwa wkaitabasamu muda wote

Umakini nao ulikuwa muhimu ili kufuatilia matukio ukumbini

eeh wacha nicheke mwanakwetu!

Mpaka kieleweke hapa

Mtaalam Sultan akitabasamu kwa mbali


We pale unaelewa wanafanya nini? Ni kama wanaulizana

Kwa raha zetu

Kula bata kwa kwenda mbele

Ooh anataka kuharibu yule au Kiwewe unasemaje?

Mmeremeto kwa sana

Hayaa unajua sikujipanga kwa picha bana!


Mmoja wa waliong'ara kwa kunyakua tuzo, Angel Navuri

Raha ya Dunia
Kazi na dawa jamani mwili haujengwi kwa matofali

Mwili hujengwa kwa msosi au vipi!

Msosi kwanza

Sivunji mbavu hapa mpaka tumbo lienee

Kumbukumbu muhimu

Hatufukii twala kawaida






























Mamaaaa!









MAITI AZIKWA MARA MBILI KWIMBA MKOANI MWANZA.


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, mwili wa kijana umezikwa mara mbili, baada ya maziko ya kwanza kufanywa na wanakijiji cha Mwalubungwe Kata ya Hungumalwa Kwimba, Mwanza, baada ya kumuua wakidhani jambazi na kumzika bila nguo wala sanda.

Akizungumza kwa njia ya simu jana, baba mzazi wa kijana huyo, Seni Kamera alisema mwanawe Valence Abel (23), mkazi wa Zunzuli, Shinyanga, alikuwa akiishi Kahama kwa mganga wa kienyeji, akipata matibabu ya upungufu wa nguvu za kiume.

Alisema mwanawe huyo aliishi kwa mgan
ga huyo kwa miaka miwili bila kurudi nyumbani. 

Alidai wiki mbili zilizopita, aliamua kuondoka kwa mganga huyo kwa miguu akiwa amefuga ‘rasta’ na kuvaa kaniki na ngozi, masharti ambayo alipewa na mganga wake ili tatizo lake liweze kumalizika.

Alisema akiwa njiani kurudi nyumbani, alifika katika kijiji cha Mwalubungwe, na kwenda nyumba ya mkazi wa kijiji hicho kuomba chakula kutokana na njaa.

“Alipofika katika nyumba hiyo alikuta watoto wanacheza nje.Kwa mwonekano aliokuwa nao, walimpiga kwa mawe na kumwita mwizi, kisha mzazi mmoja akapigana naye huku akipiga kelele, watu walifika na kumshambulia na hatimaye alipoteza maisha na kumzika bila nguo wala sanda,“ alisema Kamera.

Alisema taarifa za kifo cha mwanawe, alizipata kwa mtu aliyemwambia kuna mtu ameuawa ambaye alijitambulisha kwa jina la Kamera.

Alifuatilia na kufukua kaburi hilo na kukuta ni mwanawe. Alichukua maiti na kumzika tena.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu alipohojiwa kuhusu tukio hilo, alisema hana taarifa. Lakini, aliahidi kufuatilia ili kufahamu undani wake.
CHANZO HABARILEO.

Sumaye awapiga kijembe wapenda rushwa


Waziri Mkuu wa zamani, Mhe. Fredrick Sumaye

WAZIRI Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, ameibuka tena na kusema, wanaokerwa na karipio lake kuhusu rushwa, wanapaswa kuachana na vitendo hivyo viovu.
Hivi karibuni, Sumaye, alitoa karipio kwa viongozi wa dini hususani ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), akionya kuhusu kasi ya wanasiasa kutumika katika harambee zake.
Sumaye, alikaririwa akisema miongoni mwa wanasiasa hao, wanatumia mwanya huo kama njia ya kuungwa mkono watakapotangaza kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Ingawa hakuwataja wanasiasa hao kwa majini, kauli yake ilitafsiriwa kumgusa Waziri Mkuu ‘aliyemrithi’ na baadaye kujiuzulu, Edward Lowassa.
Lowassa ameshiriki harambee mbalimbali nchini, hali inayoelezwa na baadhi ya wachunguzi wa mambo ya siasa kuwa ina lengo la ‘kujisafishia’ njia kuelekea urais wa 2015.
Lakini Lowassa amekanusha kushiriki harambee hizo kwa nia ya kutafuta urais, badala yake akasisitiza kwamba ana karama ya ushawishi inayomfanya afanikishe shughuli hizo kwa kupata fedha nyingi.
Jana, Sumaye alizungumza na vijana wa klabu za Jogging za Ukwamani na Islamic katika uwanja wa Tanganyika Packers jijini Dar es Salaam jana.
Alisema kama mtu anaumizwa na karipio lake dhidi ya vitendo vinavyoashiria rushwa, anapaswa kuachana navyo na si kumjibu kwa kejeli.
Sumaye alisema ushiriki wake katika vita dhidi ya vitendo viovu kama rushwa, umeanza muda mrefu na kwamba hata karipio lake kwa wanaousaka uongozi kwa njia zisizo sahihi ni sehemu ya kuisimamia imani na dhamira yake.
Alisema, “kama kuna mtu anayeumizwa kwa kauli zangu ninapokaripia uovu, nikipinga rushwa basi watoaji na walaji rushwa waache kujihusisha na vitendo hivyo, na kama hawataki kusemwa basi wapasuke.”
Sumaye alisema si rahisi akaacha kukemea vitendo viovu hasa vinavyofanywa na viongozi kwa sababu, ukimya ni sehemu ya kishawishi kwa waovu kuendeleza vitendo viovu.
Akimnukuu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliposema, serikali ya wala rushwa haiwezi kuleta maendeleo kwa wananchi wake.
Sumaye rushwa ikiachwa ishamiri, itakuwa vigumu kujenga nchi yenye usawa, hivyo kuifanya nchi kuwa katika hatari ya kuangamia.
“Hivi sasa imebaki miaka miwili ya kuingia katika Uchaguzi Mkuu, hivyo tutaanza kushuhudia namna kanga, kofia, fedha na vitu vingine vitakavyotembezwa kwa ajili ya kutafuta uongozi. Tusipolisema sasa, tutaangamia,” alisema.
Alisema wananchi wanapaswa kuwa makini na viongozi wanaotumia ushawishi wa fedha na rushwa, kwani hawafai kuongoza.
Alisema viongozi wa aina hiyo wana kundi la watu nyuma yao, wanaowafadhili hivyo pindi watakapopata uongozi, watalazimika kuwatumikia waliomo katika ufadhili huo.
Alipinga dhana kuwa vijana ni kama bomu linalongoja kulipuka, badala yake ameitaka serikali kuhakikisha wanapata fursa ili wazitumie kuliko kuwaita kwa majina hatarishi.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Azam Academy yainyuka Ashanti Utd

Azam Academy jana ilicheza na timu ya Ligi kuu ya Ashanti United kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Karume Ilala na kushinda kwa bao moja bila goli likifungwa na Mshambuliaji wa pembeni toka shinyanga Mange 

Vijana wa Azam Academy wanaonolewa na kocha Vivek Nagul akisaidiwa na Iddi Cheche chini ya meneja Philip Alando walicheza kandanda safi na kuwapoteza kabisa vijana wa Ashani United wanaocheza ligi kuu Tanzania.

Mechi hii ya kirafiki ni ya tatu ndani ya siku nne ambapo siku ya jumatano Azam Academy ilishuka kwenye uwanja wake wa nyumbani na kukwaana na timu ya Transit Camp inayoshiriki ligi daraja la kwanza na kuiangushia kipigo cha 3-1, katika mchezo huo ambao uliacha gumzo kutokana na Azam Academy kutawala mchezo huo wakipiga pasi wanavyotaka.

Baada ya mechi hiyo viongozi wa Transit Camp walikwenda kwa uongozi wa Azam FC na kuwapongeza na kusema kama timu hii ingekuwa inashiriki ligi daraja la kwanza hakika ingeweza kupanda ligi kuu bila matatizo yoyote.

Wachezaji wanaotia fora kwenye kikosi hicho ni Kaijage, Rey, Dismas, Kevin Friday, Mkomola, Mgaya, Mange, Adam Juma, Jamir Brison na Adam Gambo.

Jumamosi Asubuhi licha ya kucheza vizuri na kutawala sehemu kubwa ya mchezo lakini walijikuta wakipokea kipigo cha goli moja bila bao likifungwa na Brian Umony ambaye alitumia vizuri mchezo wa mtego wa counter attack
TIMU ya vijana ya Azam, Azam Academy jana iliinyuka timu ya Ligi Kuu Tanzania Bara, Ashanti United kwa bao 1-0 katika pambano la kujipima nguvu lililochezwa uwanja wa Karume Ilala.
Vijana hao walipata ushindi huo kupitia bao tamu lililofungwa na mshambulia wao kutoka mkoani Shinyanga aitwaye Mange.
Azam Academy inayonolewa na kocha Vivek Nagul akisaidiwa na Iddi Cheche chini ya umeneja wa Philip Alando waliwafunika kabisa Ashanti kwa soka murua walililoionyesha.
Hiyo ilikuwa mechi ya tatu kwa timu hiyo ya Azam Academy ndani ya siku nne ya awali kuumana na Transit Camp inayocheza Ligi Daraja la Kwanza na kuwakung'uta mabao 3-1 kabla ya kulala bao 1-0 toka kwa kaka zao Azam Fc katika mechi iliyofuata.

Binti aoza mkono, kisa baiskeli


Janeth Nicholaus (25)mkazi wa Rwanzari Manispaa ya Tabora akionesha mkono wake wa kulia ukiwa tayari umeanza kuoza baada ya kupata ajali ya baiskeli maarufu daladala wakati akitokea nyumbani kwenda Soko kuu la Tabora mjini ajali ambayo ilitokea kwenye makutano ya barabara ya NBC. 

Huu ndio mkono wenyewe unavyoendelea kuharibika baada ya kupita hospitali kadhaa hapa Tabora mjini na kushindikana kupona lakini sasa aliamua kufika kwenye huduma ya Maombezi  Kanisa la AGAPE MIRACLE CENTER Mwanza road Tabora manispaa kwa Mchungaji Mbagata. 

NA KAPIPIJ

Vipaji vya soka mkoani Tanga hivi hapa!

Mchezaji wa timu ya Watukutu kulia Idrisa Bakari akijaribu kumtoka mchezaji wa timu ya Sepras ya jijini Tanga wakati wa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika katika viwanja vya walewale Makolola jijini Tanga.
Mchezaji wa jimu ya Sepras Hassani Abdallah akimiliki mpira mbele ya mchezaji wa Watukutu wakati wa mchezo wao wa kirafiki.
Timu ya Sepras
Nyota wa baadaye

Wapenzi wadondoka na kufa wakifanya mapenzi dirishani

Wapenzi wameanguka na kufa baada ya dirisha walipokuwa wakifanyia mapenzi kufunguka ghafla nchini China.

Wawili hao wanasemekana kudondoka kutoka kwenye dirisha la jengo moja la makazi kwenye jiji la Wuhan nchini humo pale dirisha hilo walilokuwa wameegemea kufunguka.


Mashuhuda walivieleza vyombo vya habari vya China kwamba wapenzi hao walikumbatiana wakati wakianguka kwenye njia ya waenda kwa miguu nje.

Kwa mujibu wa The Sun, chanzo kimoja cha habari kilisema: "Huku wawili hao wakiwa wameshikamana vilivyo, walianguka nje ya jengo hilo."

Picha za kuogofya zimefichuliwa kwenye tovuti za nchini humo zikionesha wapenzi hao wakiwa wamefunikwa kwa mashuka na polisi.

Damu ilitapakaa kwenye njia ya waenda kwa miguu karibu na wapelelezi wanaonekana wakichunguza eneo la tukio.


Miili ya wapenzi hao ilipigwa picha karibu na baiskeli ambayo ilikuwa imelazwa chini, lakini hakukuwa na ripoti zozote kwamba yeyote chini alikuwa amejeruhiwa katika ajali hiyo.

Ripoti zinasema kwamba madirisha hayo kwenye jengo hilo la makazi yalikuwa hayana ubora unaotakiwa.

Inafikiriwa kwamba mwanaume huyo na mwanamke wanawezekana walikuwa wakijaribu kujipooza kando ya dirisha hilo ndipo tukio hilo likatokea.

Haikufahamika ni umbali gani kutoka juu wawili hao walikuwa wakati wakianguka.
 

Wuhan ni jiji maarufu zaidi lililopo katikati ya China.
Ukiwa na historia ya miaka 3,500 ni moja kati ya miji mikongwe na iliyostaarabika katika China.


zero99

Saturday, June 29, 2013

Hivi ndivyo Golden Bush ilivyoizima Chuo Kikuu Veterani


Wachezaji wa Golden Bush na Chuo Kikuu wakiwania mpira hewani

Kudra Omar akizidhibitiwa na beki wa Chuo Kikuu Veterani

Mtanikoma leo

Kudra Omar 13, akitafuta mbinu za kumtoka Ernest





Nasema faulo, jipangeni pale:Refa akiwaelekeza wachezaji wa Chuo kujipanga ilia Golden Bush wapige faulo

Heka heka langoni mwa Chuo Kikuu veterani

Mchesaji wa Golden Bush akiwa chini baada ya kuumia
 
Salum Swedi 'Kussi' akionyesha kiwango uwanjani

Mshikemshike dimbani

Kipa Amani Simba akiwapanga mabeki wake wakati wa kupigwa faulo langoni mwake.

John Mwansasu na Wazir Mahadh 'Mandieta' wao walikuwa mashuhuda tu kwa leo

Hawa Madogo wanakaza niingie nini?

Kudra Omar na salum Athuman wakiwa kwenye mapumziko

Amani Simba, Onesmo Wazir 'Ticotico' na Salum Swedi 'Kussi' wakiwa kwenyue mapumziko

Hoi mapumziko hata kama tunaongoza 2-1

Kocha Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio' akiwapa nasaha wachezaji wake wa Golden Bush


Mmecheza vyema, lakini mabao hawatoshi; kocha msaidizi, Herry Morris akiwapwa nasaha wachezaji wake
Mmekosaje bao pale nyie...enzi zangu yule kipa angekuwa analilia atolewe nje kuepuka kapu la mabao

Jamani jahazi linazama nyumbani inajuwake sasa?
Benchi la ufundi la Chuo Kikuu veterani hawaamini kinachowakuta




Wachezaji wa Golden Bush wanamchezea rafu mchezaji wa Chuo Kikuu

Aaaghhh! Shija Katina akiugulia maumivu

Utanijua kwa nini naitwa 'Mbududu'

Kwa nini wanaume ulala wamalizapo kusex?JAMBO hili huwaacha wanawake wakiwa wamechanganyikiwa na kujiuliza maswali chungu mzima kama kuna mahali wamekosea au hawajawavutia wapenzi wao, pale wenzi wao wanapogeukia upande wa pili na kushikwa na usingizi punde tu baada ya kumaliza tendo la kujamiiana.

Lakini utafiti uliofanywa hivi na wanasayansi unawapa wanaume ahuweni katika kuepuka lawama hizo, kwamba, kumbe siyo hiyari yao, bali ni maumbile.

Wanasayansi hao wamebaini kwamba, kwa sababu za kimaumbile ubongo wa wanaume unawalazimisha kulala muda mfupi baada ya kushiriki tendo la kujamiiana. 


Katika utafiti wao wanasayansi hao walibaini kwamba, kwa jinsi ubongo wa mwanaume ulivyotengenezwa, pale wanapomaliza tendo la kujamiiana na kufika kileleni kuna eneo linalozimika na kuwafanya kupata usingizi.

Wakati hilo likitokea kwa wanawake hali ni tofauti, kwani wao hubaki wakikodolea macho dari wakiwa wamechanganyikiwa na kujiuliza maswali lukuki, wakijihisi kutowaridhisha wapenzi wao.

Utafiti huo ulifanyika kwa kuhusisha kipimo cha kumulika, maarufu kama scan, ambapo kilitumika kuwamulika wanaume katika ubongo wao pale wanapofanya tendo la kujamiiana na baada ya kumaliza kujamiiana na kufika kileleni na kubaini kwamba, eneo linalojulikana kama cerebral cortex, eneo linalohusika na ‘fikra’ huzimika baada ya mwanaume kufika kileleni.

"Utafiti huu unatupa matokeo ya kile kinachotokea ndani ya ubongo pale mwanaume anapofika kileleni.” Gazeti la Mirror lilimnukuu mwanasayansi mmoja wa serikali ya Ufaransa aitwae Serge Stoleru.

“Lakini kwa wanawake inaonekana ni tofauti kabisa……” Aliongeza kusema mwanasayansi huyo.

Mwanasayansi huyo aliendelea kusema kwamba, wanawake hushangazwa sana na jambo hilo na ndio sababu hubaki wakiwashangaa wapenzi wao wanapolala baada ya kumaliza tendo il hali wao wakitaka zaidi….

Kwa hiyo hakuna sababu ya wanawake kuwalaumu tena wanaume baada ya kumaliza tendo na kulala kwa sababu hivi sasa wameshajua sababu, watuwache tupumuwe……

Source: Jamii Forums