STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 15, 2014

MAMIA WAMZIKA MAMA TUNDA WA AFANDE SELE

 Professor akiwa na Afande Sele Morogoro
 Professor Jay amesafiri hadi mkoani Morogoro kwenda kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa mke wa msanii mwenzake Afande Sele.
Kupitia Instagram, Professor ameshare picha akiwa kwenye mazishi na kuandika: Msibani Morogoro nyumbani kwao marehemu Asha au mama Tunda sasa hivi… tunajiandaa kwenda kumpumzisha kwenye nyumba yake ya milele saa kumi jioni ya leo, bwana alitoa bwana ametwaa, jina la bwana lihimidiwe….Amen
Jeneza la marehemu likiwa nje pamoja na watu mbalimbali waliojitokeza katika mazishi hayo
Awali Afande Sele alisema kifo cha Mama Tunda kimetokana na uzembe wa madaktari. Mama Tunda alifariki baada ya kulazwa kutokana na kuugua Malaria. Akizungumza na Bongo5 leo, Afande alidai kuwa bila uzembe wa madaktari huenda malaria isingechukua uhai wa Mama Tunda.

Afande Sele akilia kwa uchungu
“Mama Tunda ametuachia pengo kubwa sana kwenye familia,” alisema Afande. 
 “Amefariki jana saa tano usiku katika hospitali kubwa hapa Morogoro kutokana na uzembe wa madaktari. Walimpa matibabu akarudi nyumbani, sitaki kulizungumzia kiundani kwa sasa hivi kwa sababu tupo kwenye wakati mgumu. 
Huku mazishi yatafanyika kuanzia kama saa tisa hivi lakini bado hatutajua itakuwa wapi bado tupo kwenye mipango. Malaria ilimchukua sana, kwa familia na watoto kwetu ni msiba mkubwa sana, yaani ni huzuni sana,” aliongeza.
MAMIA ya wakazi wa mkoa wa Morogoro na wasanii wa fani mbalimbali jana walijitokeza katika mazishi ya mke wa nyota wa muziki wa kizazi kipya Seleman Msindi 'Afande Sele' yaliyofanyika katika makaburi ya Kola katika Manispaa ya Morogoro.
Mke wa Afande Sele, Asha Shengo maarufu kama Mama Tunda alifariki usiku wa kuamkia Alhamisi majira ya saa 5.45 katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro alikokuwa akitibwa baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa malaria iliyomuanza siku ya Jumatatu.
Akizungumza kabla ya mazishi hayo, mmoja wa ndugu wa marehemu, Ally Bushiri alisema Mama Tunda alianza kujisikia vibaya siku ya Jumatatu na kwenda kupimwa na kubainika alikuwa na malaria nne.
Alisema kuwa baadaye Mama Tunda alipatiwa matibabu na siku ya Jumanne hali yake haikuwa nzuri na kupelekwa katika hospitali ya Mtakatifu Mary iliyopo eneo la la kata ya Mafiga na ilipofika Jumatano asubuhi hali yake iliimarika na kuruhusiwa kurudi nyumbani.
Bushiri alisema kuwa siku ya Jumatano jioni hali ya Mama Tunda ilibadilika na hivyo ndugu waliamua kumpeleka katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro ambako alianzishiwa matibabu na wakati akiendelea na matibabu ghafla ilipofika majira ya saa 5.45 hali ilibadilika na kufariki dunia.
Akizungumza kwa uchungu, msanii Afande Sele alisema kuwa marehemu Mama Tunda amemuachia pengo kubwa hasa watoto wake wawili Tunda pamoja na Asante, mwenye umri wa miaka mitatu .
Afande Sele ambaye muda wote alionekana kububujikwa na machozi alisema kuwa mpaka sasa anashindwa kuamini kama mzazi mwenzake huyo ametangulia mbele za haki kwakuwa ndiyo alikuwa mmoja wa washauri wa karibu katika mambo yake ya muziki.
Mmoja wa marafiki wa karibu wa Afande Sele, Nickson Mkilanya akimuelezea marehemu Mama Tunda alisema kuwa alikuwa ni miongoni mwa wanawake shupavu, mvulivu na mwenye kupenda ushirikiano katika kila jambo.
Mungu alaze roho ya marehemu Mama Tunda mahali pema poponi Amina.
 

KUMEKUCHA TAMASHA MIAKA 16 YA HOME GYM

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEglDi10hCTdPFV9XxEqn-1KSWZYuF_sACGfpP12l93qXdf8kdG-xuil-cmSIFlYKe09y6W2DnhzXOcRrsDtyv4EDe4H6FFqQ25J9cHiQ-OX2OzBUxnUpD90byP0kV5t7JkIIYvK5exbhCo/s1600/HPIM1779.jpgKLABU 12 za timu za soka za maveterani zinazooundwa na nyota wa zamani nchini zinatarajiwa kuchuana katika michezo maalum ya Tamasha la Miaka 16 ya Home Gym, itakayofanyika Septemba 6 kwenye uwanja wa Mwenge, Dar es Salaam.
Aidha zaidi ya klabu 30 za Jogging nazo zinatarajiwa kupamba tamasha hilo ambalo litahusisha pia michezo mbalimbali ikiwamo ya netiboli, kuvuta kamba, kukimbia kwenye magunia na kukimbiza kuku.
Kwa mujibu wa mratibu wa tamasha hilo, Andrew Mangomango, klabu za maveterani zilizothibitisha kushiriki tamasha hilo ambalo litapambwa na burudani ya muziki na shoo ya watunisha misuli, wanyanyua vitu vizito, ngumi na karateka ni Mbagala Veterani, Boko, 501, Break Point, Survey, Mwenge na Msasani.
Mangomango alizitaja nyingine kuwa ni Biafra Veterani, Meeda, Mikocheni, Mbezi, Mabenzi, Segerea na Ukonga Veterani ambazo zinaundwa na nyota wa zamani wa kandanda waliowahi kutamba na timu za Simba, Yanga na Taifa Stars.
Juu ya klabu za Jogging mratibu huyo alizitaja kuwa ni pamoja na Temeke Jogging, Mwananyamala, Kingungi, Amani, Magenge, Makuka, 501, Ndiyo Sisi, Wastaarab, Makutanom, Pasada, FBI, Kongowe, Oysterbay Police, Zakheem, Kwa Nyoka, Kawe Beach, Satoji, Kawe Mkwamani na nyingine.
Mangomango aliongeza kuwa baada ya michezo yote wanamichezo washiriki watajumuika pamoja kuwatembelea yatima wanaolelewa kituo cha Chakuhama kwa ajili ya kuwapeleka misaada mbalimbali.
"Ni tamasha ambalo litaambatana na michezo mbalimbali kama ya kuvuta kamba, kukimbiza kuku, kukimbia kwenye magunia, na shoo za watunisha misuli, wanamieleka, mabondia na karateka kisha kwenda kutembelea yatima," alisema.
Mangomango alisema mgeni rasmi wa shughuli zote hizo anatarajiwa kuwa Mkuu wa Kikosi cha Jeshi cha 501, J.B Kapumbe.
Hii ni mara ya pili kwa tamasha hilo kufanyika mwaja jana lilifanyika wakati Home Gym ikiadhimisha miaka 15 tangu kuasisiwa kwake ambapo shughuli zake kuu ni kufanyisha mazoezi na kutoa ushauri juu ya afya ya mwili.

Thursday, August 14, 2014

Snura abaki njia panda na mbili mpya

NYOTA wa filamu anayekimbiza kwenye muziki, Snura Mushi, amekamilisha nyimbo mbili mpya za 'Ime-expire' na 'Mtaka Basi' japo hajui wimbo gani atakaouachia kati ya hizo.
Nyimbo hizo zimekamilika kurekodiwa chini ya watayarishaji mahiri nchini, Maneke na Adidad na zimekuja baada ya kuachia video ya wimbo wake unaotamba kwa sasa hewani uitwao 'Umeshaharibu'.
Akizungumza na MICHARAZO, Snura maarufu pia kama 'Mama Majanga' alisema atakaa na meneja wake ili kuamua wimbo upi kati ya nyimbo hizo uanze kutoka kwa mashabiki wake.
"Baada ya kuwashushia hewani video ya wimbo wa 'Umeshaharibu', nimekamilisha nyimbo mbili mpya ambazo zijajua upi utakaoanza kuruka hewani kabla ya mwingine kwani zote ni kali," alisema.
Snura alisema kuwa, mara baada ya mojawapo ya nyimbo hizo kuachiwa hewani mchakato wa kutengeneza video zake utaanza mara moja, japo hajajua kazi hiyo itafanyika katika kampuni gani.
"Video zake zitatengenezwa baada ya kuanza kuachiwa hewani kwa moja ya nyimbo hizo," alisema.
Kabla ya 'Umeshaharibu' Snura alitamba na nyimbo za 'Majanja' na 'Umevurugwa' ambazo zimemfanya msanii huyo kuwa matawi ya juu.

CAS kuamua hatma ya Suarez leo

MAHAKAMA ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) imethibitisha kwamba itatangaza maamuzi yake katika kesi ya kufungiwa kwa Luis Suarez leo.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay alifungiwa kujihusisha na masuala yote ya soka kwa miezi minne kufuatia kumng'ata beki wa ti,u ya taifa ya Italia, Giorgio Chiellini wakati wa mechi yao ya Kombe la Dunia mjini Natal, Juni.
Chama cha soka cha nchi yake haraka kilipinga adhabu hiyo, lakini FIFA ilikataa kupunguza adhabu hiyo na kusababisha kesi hiyo kupelekwa CAS.
Suarez kisha akahama Liverpool na kutua Barcelona, ambao wamerudia mara kwa mara kuelezea matumaini yao kwamba atacheza mepema kuliko ilivyotarajiwa awali.
Na sasa imethibitishwa kwamba hatima yake itajulikana saa 10:00 leo, baada ya rufaa yake kusiklizwa.
"Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) itatangaza maamuzi yake katika suala la Luis Suarez, FC Barcelona na chama cha soka cha Uruguayan Alhamisi Agosti 14, 2014 majira ya saa 4:00 jioni," taarifa rasmi ilisomeka.
"Kesi hii ilisikilizwa Agosti 8, 2014 katika ofisi za CAS mjini Lausanne. Kwa maombi ya warufani na kwa maafikiano na Fifa, CAS ilifanya hatua zake za usuhilishi.
"Kufuati hilo, Jopo la CAS liliafiki kutoa maamuzi yake ndani ya muda mfupi lakini kwa mazingira yanayofuata baadaye."

Tata kocha mpya wa Argentina kutangazwa rasmi leo



ALIYEKUWA kocha wa Barcelona, Gerardo 'Tata' Martino amechaguliwa kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Argentina.
Tata amepata ulaji huo baada ya kocha aliyeifikisha fainali ya kombe la dunia Alejandro Sabella kujiuzuru mara tu baada ya kufungwa bao 1-0 na Ujerumani kwenye mchezo wa fainali ya mwaka 2014.
Martino alisitishiwa huduma kwenye klabu ya baada ya kuwa na msimu mbaya huku akiiongoza Barcelona kumaliza msimu bila taji lolote kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2008.
Martino mwenye umri wa miaka 51 ana uzoefu wa kufundisha soka akiwa ameiongoza timu ya taifa ya Paraguay kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo kati ya mwaka 2006 hadi 2011, Martino atatangazwa rasmi leo Alhamis.

Akiwa kocha wa Barcelona aliiongoza timu hiyo kushinda michezo 40 kati ya michezo 59.

Rais Kikwete ateua majaji wa Mahakama Kuu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, baada ya kushauriana na Tume ya Utumishi wa Mahakama, amewateua wafuatao kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuanzia tarehe 13 Agosti, 2014.

WATUMISHI WA MAHAKAMA

(i)                 Bw. Penterine Muliisa KENTE, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani, Dar es Salaam.

(ii)               Bw. Benedict Bartholomew MWINGWA, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Msajili wa Mahakama Kuu, Dar es Salaam.

(iii)             Bw. Edson James MKASIMONGWA, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Katibu wa Jaji Mkuu.

(iv)             Bw. David Eliad MRANGO, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Msajili, Baraza la Ushindani, Dar es Salaam.

(v)               Bw. Mohamed Rashid GWAE, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Msajili, Mahakama Kuu, Kitengo cha Kazi, Dar es Salaam.

(vi)             Dkt. John Eudes RUHANGISA, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Msajili, Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Arusha.

(vii)           Bw. Firmin Nyanda MATOGORO, ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Naibu Mwenyekiti, Baraza la Rufaa la Kodi, Dar es Salaam.

MAWAKILI WA SERIKALI NA TAASISI MBALIMBALI ZA SERIKALI

(i)                 Dkt. Eliezer Mbuki FELESHI, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Mkurugenzi wa Mashitaka, Dar es Salaam.

(ii)               Bi. Barke Mbaraka Aboud SEHEL, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Kaimu Mkurugenzi, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam.

(iii)             Bi. Winfrida Beatrice KOROSSO ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Katibu Mtendaji, Tume ya Kurekebisha Sheria, Dar es Salaam.

(iv)             Bi. Lilian Leonard MASHAKA, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa,                      (TAKUKURU), Dar es Salaam.

(v)               Bi. Leila Edith MGONYA, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Msaidizi wa Waziri Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Dar es Salaam.

(vi)             Bw. Awadhi MOHAMED, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Mchunguzi Mkuu, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, (TAKURURU), Dar es Salaam.

MAWAKILI WA KUJITEGEMEA

(i)                 Bw. Lugano J.S. MWANDAMBO, kutoka REX Attorneys, Dar es Salaam.

(ii)               Bw. Amour Said KHAMIS, kutoka AKSA Attorneys, Dar es Salaam.

(iii)             Dkt. Paul KIHWELU, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Wakili wa Kujitegemeana na Mhadhiri Mwandamizi, Chuo Kikuu Huria, Dar es Salaam.

(iv)             Bi. Rose Ally EBRAHIMU, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Wakili wa Kujitegemea, Bulyankulu Gold Mine Ltd, Shinyanga.

(v)               Bi. Salma MAGHIMBI, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Mjumbe, Tume ya Ushindani, (FCC), Dar es Salaam.

WATUMISHI WA VYUO VIKUU

(i)                 Dkt. Mary Caroline LEVIRA, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu Kishiriki cha Ruaha.

(ii)               Dkt. Modesta Opiyo MAKOPOLO, ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Mkuu wa Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu, Mzumbe, Morogoro.

Wateuliwa wote wataapisha tarehe 15 Agosti, 2014 Saa 05.00 asubuhi katika Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam.

Imetolewa na Mkurugenzi Idara ya habari Maelezo
13 Agosti, 2014

NANI KATOKA NA KUINGIA KLABU ZA ENGLAND




WIKI chache kabla ya dirisha la usajili wa wachezaji barani Ulaya kufungwa Agosti 31, nyota mbalimbali wameshahama na kuhamia katika klabu za Ligi Kuu ya England.
Chini ni baadhi ya orodha ya majina ya wachezaji na klabu zao waliohama au kununuliwa wakati Ligi Kuu ya England ikitarajiwa kuanza rasmi siku ya Jumamosi.

ARSENAL
WALIOSAJILIWA
Alexis Sanchez (Barcelona, £30m),
Calum Chambers (Southampton, £12m),
Mathieu Debuchy (Newcastle, £10m),
David Ospina (Nice, £3m)

WALIOONDOKA
Thomas Vermaelen (Barcelona, £15m),
Thomas Eisfeld (Fulham, undisclosed),
Bacary Sagna (Manchester City, free),
Lukasz Fabianski (Swansea, free),
Nicklas Bendtner (released),
Park Chu-young (released),
Chuks Aneke (released),
Daniel Boateng (released),
Wellington Silva (Almeria, loan),
Carl Jenkinson (West Ham, loan),
Benik Afobe (MK Dons, loan)

ASTON VILLA
WALIOSAJILIWA
Philippe Senderos (Fulham, free),
Joe Cole (West Ham, free),
Tom Leggett (Southampton, undisclosed),
Isaac Nehemie (Southampton, undisclosed),
Kieran Richardson (Fulham, undisclosed),
Aly Cissokho (Valencia, £2m)

WALIOONDOKA
Marc Albrighton (Leicester City, free),
Nathan Delfouneso (Blackpool, free),
Jordan Bowery (Rotherham, undisclosed),
Samir Carruthers (MK Dons, undisclosed),
Nicklas Helenius (Aalborg, loan),
Yacouba Sylla (Kayseri Erciyesspor, loan),
Jed Steer (Doncaster Rovers, loan),
Antonio Luna (Hellas Verona, loan)

BURNLEY
WALIOSAJILIWA
Lukas Jutkiewicz (Middlesbrough, £2.5m),
Michael Kightly (Stoke, undisclosed),
Marvin Sordell (Bolton, free),
Matt Gilks (Blackpool, free),
Matt Taylor (West Ham, free),
Steven Reid (West Brom, free)

WALIOONDOKA
Chris Baird (West Brom, free),
Junior Stanislas (Bournemouth, free),
David Edgar (Birmingham, free),
Keith Treacy (released),
Brian Stock (released),
Nick Liversedge (released)

CHELSEA
WALIOSAJILIWA
Cesc Fabregas (Barcelona, £30m),
Diego Costa (Atletico Mdrid, £32m),
Mario Pasalic (Hadjuk Split, undisclosed),
Filipe Luis (Atletico, £16m),
Didier Drogba (Galatasaray, free)

WALIOONDOKA
David Luiz (Paris Saint-Germain, £50m),
Romelu Lukaku (Everton, £28million),
Samuel Eto'o (released),
Frank Lampard (New York City, free),
Sam Hutchinson (Sheffield Wednesday, free),
Mark Schwarzer (released),
Henrique Hilario (released),
Wallace (Vitesse Arnhem, loan),
Bertrand Traore (Vitesse Arnhem, loan)
Thorgan Hazard (Borussia Monchengladbach, loan),
Ashley Cole (Roma, £1.5m),
Demba Ba (Besiktas, £8m),
Mario Pasalic (Elche, loan)
Patrick van Aanholt (Sunderland, undisclosed),
Ryan Bertrand (Southampton, loan),
Gael Kakuta (Rayo Vallecano, loan),
John Swift (Rotherham, loan),
Oriol Romeu (Valencia, loan)

CRYSTAL PALACE
WALIOSAJILIWA
Chris Kettings (Blackpool, free)
Fraizer Campbell (Cardiff, £800,000),
Brede Hangeland (Fulham, free)

WALIOONDOKA
Jonathan Parr (Ipswich, free),
Dean Moxey (Bolton, free),
Aaron Wilbraham (Bristol City, free),
Kagisho Dikgacoi (Cardiff, free),
Danny Gabbidon (released),
Neil Alexander (released),
Ibra Sekajja (released),
Alex Wynter (Portsmouth, loan),
Kwesi Appiah (Cambridge, loan),
Jose Campana (Sampdoria, undisclosed),
Jack Hunt (Nottingham Forest, loan),
Stephen Dobbie (Fleetwood, loan)

EVERTON
WALIOSAJILIWA
Romelu Lukaku (Chelsea, £28m),
Gareth Barry (Manchester City, free),
Muhamed Besic (Ferencvaros, £4m),
Brendan Galloway (MK Dons, Undisclosed)

WALIOONDOKA
Apostolos Vellios, (Lierse, free)
Mason Springthorpe (released)
Magaye Gueye (Millwall, free)

HULL
WALIOSAJILIWA
Robert Snodgrass (Norwich, £8m),
Jake Livermore (Tottenham, £6m),
Tom Ince (Blackpool, free),
Harry Maguire (Sheffield United, £2.5m),
Andrew Robertson (Dundee United, £2.85m)

WALIOONDOKA
Matty Fryatt (Nottingham Forest, free),
Cameron Stewart (Ipswich, free),
Nick Proschwitz (Brentford, free),
Robert Koren (released),
Abdoulaye Faye (released),
Conor Henderson (Crawley, free),
Dougie Wilson (released),
Conor Townsend (Dundee United, loan),
Joe Dudgeon (Barnsley, loan)

LEICESTER CITY
WALIOSAJILIWA
Matthew Upson (Brighton, free),
Marc Albrighton (Aston Villa, free),
Leonardo Ulloa (Brighton, £7m),
Ben Hamer (Charlton, free),
Jack Barmby (Manchester United, free),
Louis Rowley (Manchester United, free)

WALIOONDOKA
Lloyd Dyer (Watford, free),
Neil Danns (Bolton, free),
Sean St Ledger (released),
Zak Whitbread (Derby, free),
Paul Gallagher (Preston, loan),
Marko Futacs (released),
George Taft (Burton Albion, free)

LIVERPOOL
WALIOSAJILIWA
Adam Lallana (Southampton, £23m),
Lazar Markovic (Benfica, £20m),
Emre Can (Bayer Leverkusen, £9.8m),
Rickie Lambert (Southampton, £4m),
Dejan Lovren (Southampton, £20m),
Divock Origi (Lille, £10m),
Javier Manquillo (Atletico Madrid, loan)

WALIOONDOKA
Luis Suarez (Barcelona, £75m),
Pepe Reina (Bayern Munich £2m),
Conor Coady (Huddersfield, £500,000),
Luis Alberto (Malaga, loan),
Iago Aspas (Sevilla, loan),
Andre Wisdom (West Brom, loan),
Divock Origi (Lille, loan),
Brad Smith (Swindon, loan)

MANCHESTER CITY
WALIOSAJILIWA
Eliaquim Mangala (Porto, £32million),
Fernando (Porto, £12m),
Willy Caballero (Malaga, £6m),
Bruno Zuculini (Racing Club, £3m),
Bacary Sagna (Arsenal, free),
Frank Lampard (New York City, loan)

WALIOONDOKA
Costel Pantilimon (Sunderland, free),
Joleon Lescott (West Brom, free)
Gareth Barry (Everton, free),
Alex Nimely (released),
Rony Lopes (Lille, loan),
Emyr Huws (Wigan, loan),
Reece Wabara (Doncaster Rovers, free),
Jack Rodwell (Sunderland, £7m)

MANCHESTER UNITED
WALIOSAJILIWA
Luke Shaw (Southampton, £31.5m),
Ander Herrera (Athletic Bilbao, £29m),
Vanja Milinkovic (FK Vojvodina, undisclosed)

WALIOONDOKA
Alexander Buttner (Dinamo Moscow, £5.6m),
Rio Ferdinand (QPR, free),
Nemanja Vidic (Inter Milan, free),
Federico Macheda (Cardiff City, free),
Jack Barmby (Leicester, free),
Louis Rowley (Leicester, free)
Ryan Giggs (retired),
Patrice Evra (Juventus, £2.5m)
Bebe (Benfica, £2.4m)

NEWCASTLE
WALIOSAJILIWA
Remy Cabella (Montpellier, £12m),
Emmanuel Riviere (Monaco, £6m),
Siem de Jong (Ajax, £6m), Daryl Janmaat (Feyenoord, £5,m),
Jamaal Lascelles and Karl Darlow (Nottingham Forest, £7million -joint fee),
Ayoze Perez (Tenerife, £1.5m),
Jack Colback (Sunderland, free),
Facundo Ferreyra (Shakhtar Donetsk, loan)

WALIOONDOKA
Mathieu Debuchy (Arsenal, £10m),
James Tavernier (Wigan, undisclosed),
Dan Gosling (Bournemouth, free),
Shola Ameobi (released),
Conor Newton (Rotherham, free),
Michael Richardson (released),
Sylvain Marveaux (Guingamp, loan),
Jamaal Lascelles (Nottingham Forest, loan),
Karl Darlow (Nottingham Forest loan),
Adam Campbell (Fleetwood, loan)

QUEENS PARK RANGERS
WALIOSAJILIWA
Rio Ferdinand (Manchester United, free),
Steven Caukler (Cardiff, £8m),
Jordon Mutch (Cardiff, £6m),
Mauricio Isla (Juventus, loan)

WALIOONDOKA
Tom Hitchcock (Mk Dons, free),
Aaron Hughes (Brighton, free)
Stephane Mbia (released),
Andrew Johnson (released),
Luke Young (released),
Hogan Ephraim (released),
Angelo Balanta (released),
Yossi Benayoun (Maccabi Haifa, undisclosed),
Esteban Granero (Real Sociedad, undisclosed)

SOUTHAMPTON
WALIOSAJILIWA
Dusan Tadic (Twente, £10.3m),
Fraser Forster (Celtic, £10m),
Graziano Pelle (Feyenoord, £8m),
Ryan Bertrand (Chelsea, loan),
Saphir Taider (Inter Milan, loan)

WALIOONDOKA
Luke Shaw (Manchester United, £31.5m),
Adam Lallana (Liverpool, £23m),
Dejan Lovren (Liverpool, £20m),
Calum Chambers (Arsenal, £12m),
Rickie Lambert (Liverpool, £4m),
Tom Leggett (Aston Villa, undisclosed),
Isaac Nehemie (Aston Villa, undisclosed),
Guly do Prado (released),
Lee Barnard (Southend, free),
Jonathan Forte (Oldham, free),
Danny Fox (Nottingham Forest, free),
Andy Robinson (Bolton, free),
Dani Osvaldo (Inter Milan, loan)

STOKE
WALIOSAJILIWA
Mame Biram Diouf (Hannover, free),
Dionatan Teixeira (Banska Bystrica, undisclosed),
Phil Bardsley (Sunderland, free),
Steve Sidwell (Fulham, free),
Bojan Krkic (Barcelona, undisclosed)

WALIOONDOKA
Michael Kightly (Burnley, undisclosed),
Matthew Etherington (released),
Juan Agudelo (released)

SUNDERLAND
WALIOSAJILIWA
Jack Rodwell (Man City, £7m),
Patrick van Aanholt (Chelsea, undisclosed),
Billy Jones (West Brom, free),
Jordi Gomez (Wigan, free),
Costel Pantilimon (Manchester City, free),
Santiago Vergini (Estudiantes, loan)

WALIOONDOKA
Ignacio Scocco (Newell's, £800,000),
Jack Colback (Newcastle, free),
Craig Gardner (West Brom, free),
Phil Bardsley (Stoke, free),
Billy Knott (Bradford, free)
Keiren Westwood (Sheffield Wednesday, free),
Carlos Cuellar (released),
Andrea Dossena (released),
Louis Laing (released),
Oscar Ustari (Newell's, free),
David Vaughan (Nottingham Forest, free),
John Egan (Gillingham, free),
El Hadji Ba (Bastia, loan)

SWANSEA
WALIOSAJILIWA
Marvin Emnes (Middlesbrough, £1.5m),
Bafetimbi Gomis (Lyon, free),
Lukasz Fabianski (Arsenal, free),
Stephen Kingsley (Falkirk, undisclosed),
Gylfi Sigurdsson (Tottenham, swap)
Jefferson Montero (Monarcas Morelia, £4m)

WALIOONDOKA
Leroy Lita (released),
David Ngog (released),
Daniel Alfei (Northampton, loan),
Jernade Meade (released),
Darnel Situ (released),
Michu (Napoli, loan),
Ben Davies (Tottenham, £10m),
Michel Vorm (Tottenham, £5m)
Alejandro Pozuelo (Rayo Vallecano, undisclosed),
Leroy Lita (Barnsley, free),
Chico Flores (Lekhwiya, free)

TOTTENHAM
WALIOSAJILIWA
Ben Davies (Swansea, swap), Michel Vorm (Swansea, £5m),
Eric Dier (Sporting Lisbon, £4m)

WALIOONDOKA
Jake Livermore (Hull, £6m),
Gylfi Sigurdsson (Swansea, swap),
Iago Falque (Genoa, £4m)
Heurelho Gomes (Watford, free),
Cameron Lancaster (released),
Alex Pritchard (Brentford, loan), Shaquile Coulthirst (Southend, loan)

WEST BROMWICH ALBION
WALIOSAJILIWA
Brown Ideye (Dynamo Kiev, £10m),
Jason Davidson (Heracles, undisclosed),
Cristian Gamboa (Rosenborg, undisclosed),
Craig Gardner (Sunderland, free),
Joleon Lescott (Manchester City free),
Chris Baird (Burnley, free),
Sebastien Pocognoli (Hannover 96, undisclosed),
Andre Wisdom (Liverpool, loan)

WALIOONDOKA
Liam Ridgewell (Portland Timbers, free),
Billy Jones (Sunderland, free),
Steven Reid (Burnley, free),
Cameron Gayle (Shrewsbury, free),
Diego Lugano (released),
Zoltan Gera (released),
Scott Allan (released),
Nicolas Anelka (released),
George Thorne (Derby County, undisclosed)

WEST HAM
WALIOSAJILIWA
Enner Valencia (Pachuca, £12m), Cheikhou Kouyate (Anderlecht, £7m),
Mauro Zarate (Velez Sarsfield, undisclosed),
Aaron Cresswell (Ipswich, undisclosed),
Diego Poyet (Charlton, undisclosed),
Carl Jenkinson (Arsenal, home)

WALIOONDOKA
Joe Cole (Aston Villa, free),
Matt Taylor (Burnley, free),
Stephen Henderson (Charlton, free),
Jack Collison (released),
George McCartney (released),
Callum Driver (released),
Jordan Spence (released),
George Moncur (Colchester, free

Moto waleta balaa msikiti wa Mtambani


Moto Mkubwa uuliokuwa ukiendelea kuwaka katika eneo la juu la Jengo la Shule ya Sekondari ya Kiislam ya Mivumoni (Mivumoni Islamic Seminary) iliyopo ndani ya Msikiti wa Mtambani, Kinondoni B Jijini Dar es Salaam jana jioni.
Eneo hilo ambalo lilikuwa likitumika kama Mabweni ya Wanafunzi wa Shule hiyo,Maabara na Ofisi za Walimu limeteketea kabisa kiasi kwamba hakuna kitu chochote kilichoweza kuokolewa.
Jitihada za kuuzima moto huo zilifanywa huku sehemu ya Waumini wa Kiislam wakijitokeza kwa wingi kusaidia juhudi hizo za kuuzima moto huo zilizokuwa zikiendesha na Kampuni ya Kuzima moto ya Ultimate,japo baadae gari hilo liliisha maji,hali iliyowapelekea Waumini hao kulijaza maji gari hilo kwa kutumia ndoo huku kazi ya Uzimaji moto huo ikiendelea.
Chanzo cha Moto huo,inadaiwa ni hitilafu ya Umeme iliyokuwepo kwenye Bweni la Wasichana Wanafunzi wa Shule hiyo.Hakuna mtu yeyote aliepoteza maisha wala kujeruhiwa katika tukio hilo.Picha zote na Othman Michuzi. 
Moto mkubwa ukiendelea kuwaka kwenye eneo hilo.
Ulinzi mkali wa Polisi ulitawala katika eneo la Msikiti huo wa Mtambani kuhakikisha Usalama unakuwepo kwenye eneo hilo.
Sehemu ya Waumini wa Kiislam wakishirikiana kusombelea maji ili kuuzima moto huo. 
Jitihada zikiendelea. 
Gari la Zima Moto mali ya Kampuni ya Ultimate Security likijazwa maji kwa ndoo ili kuendelea na zoezi la uzimaji w amoto huo. 
Likafika na gari hili kwa ajili ya kusaidia kuzima moto huo.

Mashuhuda wakiwa nje ya eneo hilo.CRDT JIACHIE BLOG

TFF HAITAMBUI MABADILIKO YA UONGOZI COASTAL UNION


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) halitambui mabadiliko ya uongozi ndani ya Coastal Union yanayodaiwa kufanywa na mkutano wa wanachama wa klabu hiyo uliofanyika hivi karibuni.

Uongozi wa Coastal Union uliochaguliwa na mkutano wa uchaguzi wa klabu hiyo ndiyo ambao tunautambua, na tutaendelea kufanya nao kazi, na sio uongozi mwingine wowote ule.

Tunapenda kuwakumbusha wanachama wetu (ikiwemo Coastal Union) kuheshimu katiba ya TFF pamoja na katiba zao, kwani hazitambui mapinduzi ya uongozi wala kamati za muda za utendaji. TFF inafanya kazi za kamati za utendaji zilizopatikana kwa njia ya uchaguzi tu.

Tayari tumepokea barua kutoka kwa Kaimu Mwenyekiti wa Coastal Union, Steven Mnguto ikilalamikia kusimamishwa kwake.

Hivyo, tunafuatilia suala hilo kwa kina, na ikibainika kuwa kuna viongozi wamehusika katika mapinduzi hayo watafikishwa katika vyombo husika kwa hatua zaidi.

Afande Sele apata msiba wa Mama Tunda

Afande Sele
Afande Sele na aliyekuwa mkewe pamoja na mtoto wao Tunda
MSANII mkiongwe wa muziki wa kizazi kipya nchini, Selemani Mshindi 'Afande Sele' amepata pigop baada ya aliyekuwa mkewe, Asha au Mama Tunda kufariki dunia.
Afande Sele amewajulisha watu wake wa karibu na mashabiki kuhusu msiba uliomkuta kwa kufiwa na mama wa mwanae Tunda kupitia ukurasa wa facebook.
Msiba huo umekuja ikiwa ni miezi kadhaa tangu wawili hao walipotangaza kuachana wakiwa tayari wamejaliwa kuzaa watoto wawili. MUNGU AIPOKEE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA.
AFANDE