STRIKA

USILIKOSE

Sunday, May 19, 2013
Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa atiwa mbaroni kisa...!
Warembo Miss Tabata 2013 kutembelea Mbuga ya Mikumi
![]() |
Miss Tabata wakiwa kwenye pozi ya picha ya pamoja |
WAREMBO watakaoshiriki kinyang'anyiro cha shindano la Miss Tabata
2013 watatembelea mbuga ya wanyama ya
Mikumi wikiendi ijayo.
Mratibu wa shindano hilo
Godfrey Kalinga mapema leo kuwa, lengo la ziara hiyo ni kukuza utalii wa ndani.
Alisema kuwa warembo hao pia watapata fursa ya kujua vivutio vilivyomo kwenye
mbuga hiyo iliyoko mkoani Morogoro.
“Hii siyo mara yetu ya kwanza
kuwapeleka warembo wetu mbugani. Tumekuwa tukifanya kila mwaka,” alisema
Kalinga.
Kapinga alisema kuwa
ziara hiyo imedhaminiwa na CXC Africa.
Shindano la kumsaka Miss
Tabata litafanyika Mei 31 katika ukumbi
wa Da’ West Park, Tabata.
Wadhamini wa shindano
hilo ni Nipashe, Redds, Dodoma Wine, Nipashe, Vayle Springs, Multichoice, Fredito
Entertainment, CXC Africa, Brake Point na Saluti5.
Warembo watakaoshiriki
kwenye shindano hilo linaloandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts ni
Madgalena Bhoke (21), Kabula Juma Kibogoti (20), Upendo Dickson Lema (22), Hidaya David Mwenda (22), Aneth Ndumbalo (19), Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19),
Kazunde Musa Kitereja (19), Rehema Kihinja (20), Pasilida Mandali (21), Brath Chambia (23),
Joaniter Kabunga (21), Recho Mushi (20),Caroline Sadiki (20) na Suzan Daniel (18).
Warembo watano watachaguliwa
kushiriki mashindano ya Miss Ilala na baadaye Miss Tanzania.
Anayeshikilia taji la
Miss Tabata kwa sasa ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.
Simba na Yanga zaingiza Mil, 500, zenyewe zazoa Mil. 250
Simba na Yanga zilipoumana jana uwanja wa Taifa |
PAMBANO la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh. 500,390,000.
Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.
Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.
Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.
Golden Bush Veterani yaendeleza ubabe Dar
![]() |
Wakali wa soka la maveterani Dar, Golden Bush |
Timu hiyo ilipata ushindi katika michezo ya Bonanza iliyofanyika kwenye viwanja wa Staki Shari, Ukonga ambapo wakali hao waliwacharaza wapinzani wao hao.
Mabao ya Di Natale na 'kisiki' wa zamani wa Moro Utd na Yanga, Yahya Issa yalitosha kuizamisha Ukonga Veterani na kuwafanya Golden Bush kurejea maskani mwao wakichekaaa kwa ushindi huo.
Msemaji wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema licha ya ushindi huo bado hakufurahishwa kwa vile walipania kutoa kipigo zaidi ya hicho.
Ticotico alisema wamekuwa na mazoea ya kuzigonga timu pinzani mabao kuanzia manne hiyo ushindi wa 2-0 wanaona kama hawakutenda haki kwa Ukonga.
Saturday, May 18, 2013
Wanawake Mbeya wamcharukia Mchumba wa Dk Slaa kwa kumkashifu Mama Salma Kikwete
UMOJA
wa wanawake wa chama cha Mapinduzi Mkoani Mbeya(UWT) umemshukia
Bi.Josephine Mushumbusi ambaye ni mchumba Katibu Mkuu wa chama cha
Demokrasia na maendeleo CHADEMA kufuatia kauli za udhalilishaji dhidiya Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
Hatua hiyo inatokana na kauli za kiudhalilishaji zilizotolewa mwishoni mwa wiki na mchumba huyo wa Katibu Mkuu wa Chadema kuwa mama Kikwete ameshindwa kumshauri Rais ambaye ni mume wake kuiongoza nchi vizuri.
Demokrasia na maendeleo CHADEMA kufuatia kauli za udhalilishaji dhidiya Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
Hatua hiyo inatokana na kauli za kiudhalilishaji zilizotolewa mwishoni mwa wiki na mchumba huyo wa Katibu Mkuu wa Chadema kuwa mama Kikwete ameshindwa kumshauri Rais ambaye ni mume wake kuiongoza nchi vizuri.
Kauli
hiyo imetolewa jana na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Mkoa wa Mbeya
Bi.Priscilla Mbwaga wakati akitoa Tamko kwa waandishi wa habari juu
ya Matusi ya wazi yaliyotolewa na Bi.Mushumbusi kwa Mke wa Rais katika
mikutano ya hadhara iliyofanyika Wilayani Mbozi Kata ya Vwawa Mkoani hapa.
Bi.Mbwaga alisema kuwa katika mikutano yake ya Hadhara Bi.Mushumbusi alidai kuwa mama Salma Kikwete ameshindwa kumshauri mume wake kuingoza nchi na kuacha Twiga wakiwa wanakunjwa na kuondoka na kwamba yeye akiwa Ikulu hataacha kumshauri mume wake Dkt.Slaa katika masuala ya kuingoza Nchi
Hata hivyo Mwenyekiti huyo alisema kama umoja huo wanalaani vikali lugha chafu na za kichochezi zinazopandikizwa chuki miongoni mwa jamii ya watanzania .
Alisema kuwa kama umoja wa wanawake wanalaani matusi hayo na kwamba umoja huo ulifuatilia mikutano hiyo na kugundua kuwa ilikuwa imetawaliwa na matusi badala ya kutoa sera kwa wananchi kuwa wanataka kufanya nini.
“Sisi kama umoja wa wanawake Mkoa tunaeleza umma ambao una imani na kuwa katika utamaduni na maadili yao hawapendi na wala hawajazoea kusikia matusi katika jamii yao hivyo wakiangalie vizuri na kwa makini Chadema kuwa cha hicho kina watu wa maadili gani , mahali pote siku zote na miaka yote ni matusi,kuongea uongo, uzushi na kashfa wasimamapo majukwaani “alisema Mwenyekiti huyo.
Aidha Bi.Mbwaga alisema kuwa wanawake wa mkoa wa Mbeya wanadhani kuwa kauli ambazo zimetolewa na Mushumbusi ni ni za kuwadhalilisha wanawake wote wa Tanzania kwani Mama Salma ni Kiongozi wa juu pamoja
na Mushumbusi .
“Tunamshangaa sana Mushumnbusi anaposimama majukwaani na kutoa kashfa nzito za namna hii ni kama nani kwa wanawake wa Tanzania 'alihoji Mwenyekiti huyo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoani hapa (CCM),Bw.Amani Kajuna alisema kauli aliyotoa Dkt.slaa kuwa Rais Kikwete ana Udini ni ulaghai mkubwa ambao anaufanya kwa wananchi na kuendelea kuiweka nchi katika mazingira magumu .
“Kama vijana tunatambua kuwa Rais Kikwete ni kiongozi wa watanzania, na kwamba hana sifa ya Udini hii ajenda inaanzishwa kisiasa ili kujipatia umaarufu wa bure wa kudhani kuwa ndiyo njia ya kuwapeleka ikulu mwaka 2015 jambo ambalo halitawezekana ,maana watanzania hawataweza kukubali" alisema Mwenyekiti huyo.
Hata hivyo Bw.Kajuna aliendelea kusema kuwa Dkt. Slaa amekuwa akimtuhumu Rais Kikwete kuwa ni FREEMASON , “hebu tumuulize huyu mtu amekutana lini na Rais kwenye iman hiyo” na kwamba katika uongozi wake watanzania wameona miradi mikubwa ya maendeleo ya nchi yetu kwa ukuaji wa wa pato la Taifa.
Bi.Mbwaga alisema kuwa katika mikutano yake ya Hadhara Bi.Mushumbusi alidai kuwa mama Salma Kikwete ameshindwa kumshauri mume wake kuingoza nchi na kuacha Twiga wakiwa wanakunjwa na kuondoka na kwamba yeye akiwa Ikulu hataacha kumshauri mume wake Dkt.Slaa katika masuala ya kuingoza Nchi
Hata hivyo Mwenyekiti huyo alisema kama umoja huo wanalaani vikali lugha chafu na za kichochezi zinazopandikizwa chuki miongoni mwa jamii ya watanzania .
Alisema kuwa kama umoja wa wanawake wanalaani matusi hayo na kwamba umoja huo ulifuatilia mikutano hiyo na kugundua kuwa ilikuwa imetawaliwa na matusi badala ya kutoa sera kwa wananchi kuwa wanataka kufanya nini.
“Sisi kama umoja wa wanawake Mkoa tunaeleza umma ambao una imani na kuwa katika utamaduni na maadili yao hawapendi na wala hawajazoea kusikia matusi katika jamii yao hivyo wakiangalie vizuri na kwa makini Chadema kuwa cha hicho kina watu wa maadili gani , mahali pote siku zote na miaka yote ni matusi,kuongea uongo, uzushi na kashfa wasimamapo majukwaani “alisema Mwenyekiti huyo.
Aidha Bi.Mbwaga alisema kuwa wanawake wa mkoa wa Mbeya wanadhani kuwa kauli ambazo zimetolewa na Mushumbusi ni ni za kuwadhalilisha wanawake wote wa Tanzania kwani Mama Salma ni Kiongozi wa juu pamoja
na Mushumbusi .
“Tunamshangaa sana Mushumnbusi anaposimama majukwaani na kutoa kashfa nzito za namna hii ni kama nani kwa wanawake wa Tanzania 'alihoji Mwenyekiti huyo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoani hapa (CCM),Bw.Amani Kajuna alisema kauli aliyotoa Dkt.slaa kuwa Rais Kikwete ana Udini ni ulaghai mkubwa ambao anaufanya kwa wananchi na kuendelea kuiweka nchi katika mazingira magumu .
“Kama vijana tunatambua kuwa Rais Kikwete ni kiongozi wa watanzania, na kwamba hana sifa ya Udini hii ajenda inaanzishwa kisiasa ili kujipatia umaarufu wa bure wa kudhani kuwa ndiyo njia ya kuwapeleka ikulu mwaka 2015 jambo ambalo halitawezekana ,maana watanzania hawataweza kukubali" alisema Mwenyekiti huyo.
Hata hivyo Bw.Kajuna aliendelea kusema kuwa Dkt. Slaa amekuwa akimtuhumu Rais Kikwete kuwa ni FREEMASON , “hebu tumuulize huyu mtu amekutana lini na Rais kwenye iman hiyo” na kwamba katika uongozi wake watanzania wameona miradi mikubwa ya maendeleo ya nchi yetu kwa ukuaji wa wa pato la Taifa.
CHANZO:MPEKUZI HURU
Hivi Ndivyo Yanga walivyoitambia Simba Taifa
Beki
wa Simba, Musa Mudde (kushoto) akichuana na mshambuliaji wa Yanga,
Didier Kavumbagu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara
uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, leo.
Beki wa Simba, Shamte Ramadhani akimtoka mshambuliji wa Yanga, Simon Msuva
Nahodha
wa Yanga, Nidir Haroub 'Canavaro' akiwa amenyanyua kombe la Ubingwa wa
Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara pamoja na wachezaji wenzake.
Shabiki wa Yanga akipelekwa kupewa huduma ya kwanza baada ya kuzimia wakati mchezo ukiendelea.
Kikosi cha Simba.
Makocha wa yanga wakipanga mikakati ya Ushindi.
Timu zikiingia uwanjani.
Timu zikisalimiana.
Kocha wa Simba, Patrick Liewig
Kocha wa Yanga, Ernst Brandts
Beki wa Simba, Shomari Kapombe akimtoka mshambuliji wa Yanga, Simon Msuva
Msanii Juma Nature akitumbuiza wakati wa mchezo huo.
Mshambuliaji wa Simba, Felix Sunzu akitafuta mbinu za kuwatoka mabeki wa Yanga.
Mashabiki wa Yanga.
Raha ya ushindi.
Kocha wa Yanga, Ernst Brandts akiwa amebebwa na wachezaji wake.
Kiduku
KARIBU JANGWANI NGASA
Mashabiki wa Yanga wakiwa wamembeba mshambuliaji
wa Simba, Mrisho Ngasa mara baada ya mpira kumalizika, ikiwa ni ishara ya
kumkaribisha katika klabu yao.
Mashabiki wa yanga.
Wachezaji wa timu ya Yanga wakishangilia ubingwa
wa Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuifunga Simba 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam
Kipa wa Simba, Juma Kaseja akijaribu bila
mafanikio kuokoa mpira wa kichwa uliopigwa na mshambuliaji wa Yanga, Didier
Kavumbagu katika mchezo wa kufunga pazia la Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
KARIBU NYUMBANI
Mashabiki
wa Yanga wakiwa wamembeba mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngasa mara
baada ya mpira kumalizika, ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika klabu
yao.
Refa
wa mechi ya Simba na Yanga, Nartin Saanya akiwa chini baada ya kugongwa
kwa bahati mbaya na mchezaji wa Yanga, Didir Kavumbagu.
Refa, Martin Saanya akipata matibabu.
PICHA ZOTE NA FRANCIS DANDE WA HABARI MSETO
Majina ya wanavyuo walionaswa wakijiuza haya hapa
Wanafunzi wa kike wa chuo kikuu cha Dar es salaam [UDSM],Chuo cha elimu ya biashara [CBE]na chuo cha mamlaka ya Elimu na ufundi stadi [VETA],Dar es salaam ,wamefikishwa katika mahakama ya jiji samora wakidaiwa kufanya biashara ya kuuza mili yao.
Washitakiwa hao waliokamatwa katika eneo la kona Baa Ambiance Sinza wilayani kinondoni ambao ni miongoni mwa wanawake 35 wanaodaiwa kufanya biashara hiyo na wote walifikishwa mahakamani hapo.
Kesi hiyo ilikuwa chini ya hakimu Willian Mtaki ambapo muendesha mashitaka,bwana John Kijumbe,alisema wasichana hao walikamatwa katika mazingira tofautitofauti.
Wanafunzi hao ni Yasinta Kilimo mwenye miaka 21 CBE mkazi wa upanga,Morin Masatu miaka 19 UDSM,mkazi wa kinondoni na mwanafunzi wa VETA aliyefahamika kwa jina moja la Khadija.
“Nilikwenda pale baa kuchukua simu yangu ambayo ilipotea hivyo waliniita nikaichukue ndipo askari wa jiji wakanikamata,”Alisema Khadija akijitetea.
Kwa mujibu wa bw. Kijumbe washitakiwa hao wamekosa dhamana baada ya kushindwa kutimiza masharti ya kila mmoja kuwa na wadhamini wawili au kulipa faini ya kulipa sh. 200,000.
Kesi hiyo inatarajiwa kusikilizwa tena mei 28 mwaka huu,ambapo washitakiwa wote walipelekwa Segerea.
Wakati huohuo, jeshi la Polisi mkoa wa kinondoni , limewakamata watuhumiwa 716 waliokuwa wakijihusisha na biashara ya kuuza miili kati yao wanaume 38 na wanawake 678.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni Charles Kenyela, alisema watu hao walikamatwa kwenye msako uliodumu kwa miezi sita kwenye maeneo mbalimbali ya Kinondoni.
Maeneo hayo ni baa, kumbi za starehe, madanguro, sehemu za wazi katika ufukwe wa Bahari ya Hindi, na makaburini ambapo kati ya wanaume waliokamatwa wengine ni mashoga pamoja na wateja wa machagudoa.
“Msako huo ulifanyika Maisha Club, Coco Beach, Barabara ya Tunisia , Travertine Hotel, Tandale Uwanja wa Fisi, Ambiance Club, Shekilango pamoja na Mwinanyamala” Alisema
Kamanda Kenyela aliongeza kuwa , jeshi hilo pia limewakamata raia 12 kutoka nchini Ethiopia walioingia nchini bila kibali kati ya Mei 2 na 6, mwaka huu katika eneo la Kimara Mwisho na Tegeta Kibaoni.
Alisema kukamatwa kwao kulitokana na taarifa walizozipata kutoka kwa raia wema waliowaona maeneo.
Credit:Mpekuzi Huru
Mbunge Chadema aanguka ghafla Bungeni
![]() |
Mhe. Taratibu Abama |
MBUNGE wa Viti Maalum, pichani Mwanamrisho
Taratibu Abama (Chadema), ameanguka
bungeni, baada ya kujisikia vibaya.
Mbunge huyo alianza kujisikia vibaya,
hali iliyomfanya kuketi katika viti vilivyo karibu na zahanati ya Bunge.
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia
walisema mbunge huyo alipata huduma ya kwanza katika zahanati hiyo kwa zaidi ya
saa mbili kabla ya kupelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Dodoma.Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya
hospitali hiyo, zinasema mbunge huyo alilazwa wodi namba 18.
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Dk. Zainab Chaula, alithibitisha kupokelewa kwa mbunge
huyo.
“Ni kweli yupo hapa na hali yake inaendelea vizuri sasa ,”alisema.
Subscribe to:
Posts (Atom)