STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 30, 2011

Siwezi kuchojoa nguo nicheze X-Skyner



MSANII wa filamu anayekuja juu nchini, Skyner Ally, amesema hata apewe kiasi gani cha fedha hawezi kucheza picha za watu wazima 'X' kwa madai kufanya hivyo mbali na kujidhalilisha, pia ni kwenda kinyume na mafundisho ya Mungu.
Akizungumza na MICHARAZO, Skyner, alisema ingawa yupo ndani ya fani ya uigizaji kwa nia ya kusaka fedha, lakini hayupo tayari kujivua utu wake, ili akubali kuchojoa nguo na kuigiza filamu za X.
Skyner, alisema anaamini kucheza filamu za namna hiyo ni kwenda kinyume na maadili na kukiuka mafundisho ya dini, mbali na yeye mwenyewe kujidhalilisha mbele ya jamii.
"Ingawa nasaka fedha kupitia kipaji cha uigizaji nilichonacho, lakini siwezi kukubali kucheza filamu za X hata nikiahidiwa kiasi gani cha fedha," alisema.
Kisura huyo, anayetamba kwenye filamu kama 'The Second Wife', 'Unpredictable', 'What is It', 'I hate My Birthday', 'Why I Did Love', 'Kizungumkuti' na nyinginezo, alisema kuwa msanii hakuna maana kujirahisisha na kufanya mtendo machafu, jambo alilolata wasanii wenzake kuepukana nayo ili kulinda heshima zao na fani zao kwa ujumla.
"Wasanii lazima tujiheshimu na kujithamini, kujiingiza kwenye skendo na matendo machafu ndiyo yanayotufanya tusiheshimike na kuichafua fani nzima ya sanaa, wakati imekuwa ikitusaidia baadhi yetu kumudu maisha na kuzisaidia familia zetu," alisema.
Skyner, anayetarajiwa kuolewa wiki ijayo, alisema wasanii wakijiheshimu na kuepuka skendo ni wazi jamii itawapenda na kuwathamini, hasa kama watajibidiisha kuboresha kazi zao.

No comments:

Post a Comment