STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 30, 2011

Mwandido kuja nchini kuzindua kibao cha Assosa


MWANAMUZIKI nyota wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Ny'boma Mwandido anatarajiwa kuja nchini kutumbuiza kwenye uzinduzi wa kitabu cha gwiji la muziki wa dansi nchini, Tshimanga Kalala Assosa kiitwacho 'Jifunze Lingala'.
Uzinduzi wa kitabu hicho unatarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam, ingawa tarehe na jina la ukumbi, bado hazijawekwa bayana.
Akizungumza na MICHARAZO juzi, Assosa, alisema mipango ya uzinduzi wa kitabu chake yanaendelea vema ikiwemo kufanya mpango wa kumleta Ny'boma, aliyewahi kufanya naye kazi katika bendi mbalimbali nchini Congo, ili kushiriki uzinduzi huo.
Assosa alisema tayari wameshakubaliana na gwiji hilo linalotamba na nyimbo kama 'Double Double', 'Masua' na 'Abisina' kuja katika uzinduzi huo, kinachoendelea kwa sasa ni kumtafutia tiketi ya ndege ya kumleta na kumrejeshwa baada ya shughuli hiyo.
"Maandalizi ya uzinduzi wa kitabu changu yanaendelea vema, ambapo natarajia kuja

kushindikizwa na Ny'boma Mwandido, ambaye ameafiki mualiko wetu na kuhitaji tumtumie tiketi ya ndege," alisema Assosa.
Assosa, anayemiliki bendi ya Bana Marquiz, alisema umoja wao wa Wana 'Dar Kavasha Club', unafanya mipango ya kuisaka tiketi hiyo pamoja na ufadhili kwa ajili ya shughuli nzima ya uzinduzi wa kitabu hicho ambacho tayari kipo mtaani karibu miezi sita sasa.
"Kwa sasa tunasubiri majibu ya maombi yetu ya udhamini tuliotuma katika makampuni ya masharika mbalimbali ili kufanikisha uzinduzi huo utakaoenda sambamba na burudani ya muziki," alisema.
Aliongeza mbali na kitabu hicho cha 'Jifunze Lingala-Toleo la Kwanza', pia tayari ameanza maandalizi ya toleo la pili la kitabu hicho na na kile kinachohusu maisha yake binafsi.
Vitabu vyote vinafadhiliwa Klabu ya Dar Kavasha, umoja ambao Assosa ameomba mashabiki wa miondoko hiyo mikoani kuanzisha matawi yao, ili kuupanua zaidi.

Mwisho

No comments:

Post a Comment