STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 11, 2013

Kiza kinene chatanda sakata la kupigwa risasi Sheikh Ponda

Katibu wa Kamati ya Kutetea Haki za Waislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda.
MPAKA muda huu bado hatujaweza kupata taarifa nyingine zozote kuhusu tukio la kupigwa kwa risasi kwa Sheikh Ponda Issa Ponda lililotokea mjini Morogoro.
Juhudi zetu zimeishia kupata taarifa kama tulizowafahamisha mapema, huku jeshi la Polisi likisisitiza kutohusika na kitendo hicho, licha ya mashuhuda kueleza kwamba Polisi walifyatua mabomu ya machozi na risasi za moto ambayo moja ilimpata Ponda begani.
Kadhalika hakuna ukweli wowote kwamba Sheikh Ponda amefariki dunia kama baadhi ya watu wanavyovumisha, kwa sababu mpaka tunapoandika taarifa hii kwenu tumefahamishwa kuwa sheikh huyo alikuwa kajeruhiwa na hakukuwa na yeyote kati ya vyanzo vya habari au hata Polisi wenyewe kuthibitisha juu ya Ponda kuaga dunia.
Hivyo wasomaji wa MICHARAZO, endeleeni kuvuta subira kupata ukweli wa kinachoendelea badala ya kupandwa presha kwamba Kiongozi huyo wa Umma wa Kiislam anayependwa kila kona ya nchi kwa harakati zake za kupigania haki za waislam walio wanyonge huenda amefariki.
Pia kama ni kweli Sheikh Ponda atakuwa amefariki basi ni mipango ya Mungu kwa vile kila nafsi itaonja mauti, ila ukweli ulivyo ni kwamba hakuna taarifa za kupoteza kwake maisha zaidi ya hizo za kujeruhiwa na pia haifahamiki kwa sasa yupo wapi, kitu ambacho hata Polisi kimesema na kutangaza kumsaka na kutaka wenye taarifa juu ya alipojichimbia Sheikh huyo watoe taarifa haraka. Vuteni subira.

No comments:

Post a Comment