STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 11, 2013

Azam yaanza kuingiwa mchecheto kwa Yanga

Na Mahmoud Zubeiry, Johannesburg, Afrika Kusini, IMEWEKWA AGOSTI 11, 2013 SAA 5:05 ASUBUHI
KOCHA Muingereza wa Azam FC, Stewart John Hall ameridhishwa na maandalizi ya timu yake katika kambi ya kujiandaa na msimu hapa Afrika Kusini, lakini kuelekea mchezo dhidi ya Yanga SC Jumamosi ijayo kuwania Ngao ya Jamii, mwalimu huyo anahofia sana juu ya marefa.
Stewart ameiambia BIN ZUBEIRY leo mjini hapa kwamba ana imani na timu yake imenufaika mno na kambi ya Afrika Kusini na inaweza kwenda kuwapa burudani nzuri wapenzi wa soka Tanzania baada ya hapa.
Marefa watende haki; Kocha Stewart Hall kulia akiwa na Msaidizi wake, Kali Ongala. Amemba marefa watende haki Agosti 17 Taifa dhidi ya Yanga.

Hata hivyo, Stewart amesema mchezo wa kufungua pazi la Ligi Kuu dhidi ya Yanga, Agosti 17, wasiwasi mkubwa ni marefa kuwabeba wapinzani wao siku hiyo.
“Nina wasiwasi na marefa, tena sana. Mara ya mwisho tulipocheza na Yanga, walitufunga 1-0, lakini refa alitunyima penalti na akakataa bao letu lililofungwa na John Bocco,”.
“Imekuwa kawaida unapocheza na Simba SC au Yanga, marefa wanakuwa upande mwingine. Sasa kama na kwenye mechi ya Ngao itajirudia hivyo, itakuwa mbaya. Naomba marefa watakaopangwa wachezeshe kwa haki,”alisema Stewart.
Azam ipo hapa tangu Agosti 3, kwa ajili ya kujiandaa na msimu- ambapo wataanza na mechi ya kuwania Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga SC, Agosti 17, mwaka huu, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mwaka jana, Azam FC ilifungwa 3-2 na Simba SC katika mechi ya kuwania Ngao, licha ya kuongoza kwa mabao 2-0 hadi mapumziko, lakini kocha Stewert amepania kubeba ‘Ubao’ safari hii.  
Kikosi kazi; Kikosi cha Azam katika moja ya mechi zake hapa Afrika Kusini

Tangu iwasili hapa, Azam, ambayo imekuwa ikijifua katika viwanja vizuri vya Chuo Kikuu cha Wits, ikitokea kwenye hoteli ya nyota tano, Rundburg Towers, imekwishacheza mechi tatu na kufungwa mbili, ikishinda moja.
Ilifungwa 3-0 katika mchezo wa kwanza na Kazier Chiefs, ikashinda 1-0 katika mchezo uliofuata na Mamelodi kabla ya kufungwa 2-1 na Orlando Pirates, wakati kesho itacheza mechi ya mwisho na Moroka Swallows kabla ya Jumanne kurejea Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment