STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 11, 2013

Cheka abadilishiwa bondia pambano la WBF

Francis Cheka

Bondia Phil Williams ndiye atakayepigana na Cheka,

WAKATI akiendeleza rekodi yake ya kutopigwa katika ardhi ya Tanzania kwa karibu miaka 10 sasa, bondia Francis Cheka 'SMG' amebadilishiwa mpinzani atakayepigana naye Agosti 30 kuwania ubingwa wa WBF ulio wazi kwa sasa kutoka Findley Derrick hadi Phil Williams.
Mabondia wote hao wawili waliobadilioshana ili kupigana na Cheka anayeshikilia ubingwa wa IBF Afrika na mikanda minginje inayotambuliwa kimataifa wanatokea Marekani.
Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO-Limited), linalosimamia pambano hilo la kimataifa litakalochezwa kwenye ukumbi wa Dimaond Jubilee,  Yassin Abdallah 'Ustaadh' alisema Derrick ameondolewa kwa kukosa sifa za kupigana a Cheka.
Ustaadh alisema baada ya kupitiwa kwa rekodi za mabondia wote ilionekana Cheka amemuacha mbali Derrick na hivyo WBF ikamteua Williams anayeshikilia nafasi ya 45 duniani kati ya mabondia zaidi ya 900 wa uzito wa Super Middle kupigana na Mtanzania huyo.
Cheka yeye yupo nafasi ya 34 duniani katika uzito huo tofauti na ilivyokuwa kwa Derrick anayeshikilia nafasi ya 95 kati ya mabondia 1220 wa uzani wa kati, kitu ambacho kingempa nafasi nzuri Cheka kumshinda kirahisi mpinzani wake kwa wasifu na vigezo hiovyo.
Rais huyo wa TPBO-Limied alisema kutokana na hali hiyo ndiyo ikaamuliwa Derrick aenguliwee na nafasi yake kupewa Williams ambapoa tayari Cheka ameshataarifiwa juu ya mabadiliko hayo na anapaswa kujiandaa vyema ili kuipeperusha vizuri bendera ya Tanzania.
"Haya ni mabadiliko ya kawaida, hivyo kila kitu kinaendelea vyema juu ya maandalizi ya mchezo huo ambao ufasindikizwa na  mingine kadhaa ukiwamo wa kuwania ubingwa wa Afrika wa WBF kati ya Thomas Mashali na Mada Maugo," alisema Ustaadh.
Wakati akibadilishiwa mpinzani, Cheka juzi alimfumua Mmalawi Chiotcha Chimwemwe kwa pointi na kuendeleza rekodi ya kutipigwa katika ardhi ya Tanzania tangu Agosti 2013.
Cheka alimshinda Mmalawi huyo katika pambano lisilo la ubingwa lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro lililokuwa la raundi nane, ingawa baadhi ya mashabiki wanaamini kuwa Mtanzania huyo alibebwa mbele ya Chiotcha.
Hiyo ni mara ya pili kwa Cheka kumpiga Mmalawi huyo na kuibua hisia hizo baada ya awali kufanya hivyo Desemba 24 jijini Arusha walipokuwa wakiumana kuwania taji la IBF Afrika, ambapo Cheka alishinda na kutetea taji hilo kwa pointi huku akiachiwa majeraha makubwa.

No comments:

Post a Comment