STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 11, 2013

Kagera Sugar yatakata Uganda, kesho kuivaa URA

Kikosi cha Kagera Sugar

KAGERA Sugar iliyosafiri mpaka Uganda jioni ya leo imeanza vyema michezo yao ya kujiandaa na Ligi kuu Tanzania Bara baada ya kuikwanyua Bunawaya Fc kwa bao 1-0 katika pambano la kirafiki la kimataifa lililochezwa jijini Kampala.
Kocha Msaidizi wa Kagera, Mrage Kabange wimba wa zamani wa Simba na Taifa Stars, alisema kikosi chao kilionyesha soka la kuvutia katika pambano hilo licha ya ugeni na kujipatia bao katika kipindi cha kwanza lililofungwa na Juma Mpola.
Timu hiyo itashukla tena dimbani kesho kuumana na URA katika pambano jingine kabla ya kuangalia mechi nyingine na kurejea Kagera tayari kujiandaa na mechi yao ya fungua dimba ya ligi kuu msimu wa 2013-2014 dhidi ya 'wageni'  Mbeya City mechi itakayochezwa uwanja wa Sokoine, Agosti 24.

No comments:

Post a Comment