STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 23, 2013

Mwesigwa ndiye Katibu Mkuu TFF?

http://www.ippmedia.com/media/picture/large/mweigwachequetbl.jpg
Celestine Mwesigwa
HABARI zilitufikia hivi karibuni zinasema kuwa Katibu Mkuu wa zamani wa Yanga, Celestine Mwesigwa ndiye Katibu Mkuu  mpya wa Shrikisho la Soka Tanzania (TFF) na Katibu Mkuu wa Simba Evodias Mtawala ameukwaa ukurugenzi ndani ya shirikisho hilo.
Hata hivyo taarifa rasmi juu ya jambo hilo litawekwa bayana na Rais wa TFF, Jamal Malinzi kesho atakapotangaza safu mpya ya waajiriwa wa shirikisho hilo ikiwa ni mwezi mmoja na ushei tangu ashinde Urais katika Uchaguzi Mkuu wa TFF uliofanyika Oktoba 27.
Ila MICHARAZO inazo habari kwamba Mwesigwa aliyetimuliwa kihuni Yanga, ametwaa nafasi hiyo akiwashinda waombaji wengine. Ila vuteni subira hadi hiyo kesho mpate uhakika wa jambo hili toka mdomoni mwa Malinzi mwenyewe.

No comments:

Post a Comment