STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 9, 2014

Juventus haishikiki Italia, Inter nayo yang'ara

Kwadwo Asamoa scores
Kwadwo Asamoah akiifungia Juventus bao pekee leo dhidi ya Fiorentina

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Italia (Seria A) Juventus imeendelea kutamba kwenye ligi hiyo baada ya jioni hii kuifumua Fiorentina kwa kuilaza bao 1-0, huku Inter Milan nayo ikichomoza na ushindi kama huo dhidi ya Torino.
Bao la dakika ya 42 lililofungwa na Mghana, Kwadwo Asamoah lilitosha kuwapa pointi tatu 'kibibi' cha Turin na kuongeza pengo la pointi na timu inayowafuata nyuma yao, Roma kwa pointi 14 ambayo itashuka .
Juve imefikisha pointi 72 wakati Roma itakayoshuka dimbani baadaye kuumana na Napoli ikiwa na pointi 58.
Katika mechi nyingine Inter Milan iliilaza Torino kwa 1-0, huku Lazio ikilala nyumbani kwa bao 1-0 dhidi ya Atalanta, Chievo ikishinda mabao 2-1 nyumbani dhidi ya Genoa, Parma ikiifumua Hellas Verona mwaka 2-0 na Sampdoria ikishinda nyumbanio mabao 4-2 dhidi ya Livorno na Bologna na Sassuolo zikitoka suluhu.




































No comments:

Post a Comment