STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 9, 2014

JKT Ruvu yaifumua Mtibwa Sugar Chamazi

JKT Ruvu walioifumua Mtibwa leo
Mtibwa sugar iliyopoteza matumaini ya kuwnaia ubingwa na sasa kupigana kubakia katika ligi
TIMU ya Mtibwa Sugar imeendelea kuwa urojo baada ya kubamizwa na JKT Ruvu mabao 2-1 katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara iliyochezwa uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Mabingwa hao wa zamani wa Tanzania, walishindwa kuwabana vijana wa Fred Felix Minziro na kupoteza mchezo huo ulioufanya uongozi wa Mtibwa kukiri kwamba mbio za ubingwa kwao ndiyo basi tena.
Nahodha Husseni Bunu aliifungia JKT Ruvu bao dakika ya 34 bao lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili kilianza kwa Mtibwa kusawazisha bao kupitia kiungo mkongwe, Vincent Barnabas katika dakika ya 70 kabla ya dakika tano baadaye Amos Mgisa kumaliza udhia kwa kuipatia JKT bao la pili./
Kwa ushindi huo JKT Ruvu imefanikiwa kufikisha pointi 25 licha ya kusalia kwenye nafasi ya 9 ikiwa nyuma ya Mtibwa waliolingana nao pointi ila wanatofautiana uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.

No comments:

Post a Comment