STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 9, 2014

Simba yabanwa Mbeya, Prisons yaendeleza rekodi

Prisons
Simba
WEKUNDU wa Msimbazi imeendeleza rekodi mbaya ya kushindwa kuibuka na ushindi mjini Mbeya baada ya jioni hii kulazimishwa suluhu na Prisons-Mbeya katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Simba ambayo ilikuwa ikihitaji ushindi ili angalau kuendelea kuwepo kwenye mbio za kuwania ubingwa, ilishindwa kufurukuta katika mchezo huo uliochezwa kwenye uwanja wa Sokoine-Mbeya.
Ikiwa na nyota wake wote wakiwamo waliokuwa na timu ya taifa, Taifa Stars iliyokuwa Namibia kucheza mechi ya kirafiki na wenyeji wao, Simba haikuweka kuvunja mwiko wa Maafande hao wa Magereza ambao hawajapoteza mchezo wowote katika duru hili la pili la ligi.
Kwa sare hiyo Simba imeendelea kujiimarisha kwenye nafasi ya nne kwa kujikusanyia pointi 36 nyuma ya Yanga yenye pointi 38 ila ikiwa na michezo mitatu mkononi.
Prisons yenyewe imejiongeza pointi moja na kufikisha pointi 22 baada ya kucheza mechi ya 20.

No comments:

Post a Comment