STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 9, 2014

Al Ahli Benghazi yafuzu raundi ya pili Afrika

* Ndiyo ikayocheza na Yanga au Al Ahly
* TP Mazembe yapenya kwa kishindo 
* Raja Casablanca yatolewa kwa matuta
CAF Champions League | FIXTURES

Which clubs present your country?

Young Africans (Tanzania) v Al Ahly (Egypt)
Berekum Chelsea (Ghana) v Ahli Benghazi (Libya)
Gor Mahia (Kenya) v Esperance (Tunisia)
Enyimba (Nigeria) v AS Real (Mali)
Astres de Douala (Cameroon) v TP Mazembe (DR Congo)
B.Y.C (Liberia) v Sewe Sport (Cote d’Ivoire)
Dedebit (Ethiopia) v CS Sfaxien (Tunisia)
Horoya (Guinea) v Raja Casablanca (Morocco)
Flambeau de l’Est (Burundi) v Coton Sport (Cameroon)
Entente Setif (Algeria) v ASFA Yennenga (Burkina Faso)
Stade Malien (Mali) v El Hilal (Sudan)
AC Leopards (Congo) v Primeiro de Agosto (Angola)
Kaizer Chiefs (South Africa) v Liga Muçulmana (Mozambique)
Dynamos FC (Zimbabwe) v AS Vita Club (DR Congo)
Zamalek (Egypt) v Kabuscorp (Angola)
Nkana (Zambia) v Kampala City Council (Uganda) 

First leg: 28 February to 2 March 2014
Second leg: 7-9 March 2014
AL Ahli Benghazi ya Libya jioni hii imeifumua Berekum Chelsea ya Ghana kwa mabao 2-0 na kufuzu raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika ikisubiri mshindi kati ya Yanga ya Tanzania au Al Ahly ya Misri.
Ikiwa uwanja wa nyumbani Benghazi ilipata ushindi huo muhimu na kufanikiwa kufuzu raundi ya pili kwa jumla ya mabao 3-1 baada ya wiki iliyopita kulazimisha sare ya 1-1 ugenini.
Sasa timu hiyo itataka kujua itaumana na nani kati ya Yanga iliyopo ugenini kuwakabili mabingwa watetezi wa taji hili Al Ahly katika mechi inaytotarajiwa kucheza muda mfupi ujao mjini Alexandria, Misri.
Katika mechi ya kwanza Yanga ikiwa nyumbani jijini Dar es Salaam iliifumua Al Ahly kwa bao 1-0 na hivyo usiku huu itahitajika kupigania sare ya aina yoyote kuingia hatua hiyo ya pili na kukumbana na mwarabu mwingine.
Nao mabingwa wa zamani wa Afrika, TP Mazembe ikiwa nyumbani imepata ushindi wa kishindo baada ya kuicharaza Les Astres ya Cameroon mabao 3-0 na kufuzu kwa jumla ya mabao  4-1 baada ya awali kulazimishwa sare ya 1-1 ugenini na wapinzani wao hao.
Nao vijogoo wa Morocco Raja Casablanca pamoja na kushinda nyumbani bao 1-0 dhidi ya Horoya ya Guinea imejikuta iking'oa raundi ya kwanza kwa kunyukwa kwa mikwaju ya penati 5-4.
Katika mechi ya kwanza iliyochezwa mjini Conakry, Raja walifungwa bao 1-0 na hivyo ushindi wa leo uliifanya kuwa sare ya 1-1 na kulazimishwa kupigiana penati na kushindwa na wapinzani wao. 

No comments:

Post a Comment