STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 9, 2014

AC MIlan bado mwaka wa tabu Italia yanyukwa tena

Di Natale alipowatungua Milan jana
KLABU ya AC Milan imeendelea kusuasusa kwenye Ligi Kuu ya Italia Seria A baada ya jana usiku kudonyolewa bao 1-0 ugenini na Udinese na kuzidi kuiweka katika wakati mgumu hata kupata nafasi ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani.
Bao pekee lililoizamisha Milan iliyomweka benchi mshambuliaji wake nyota, Mario Balotelli na kumuingiza kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Robinho, liliwekwa kimiani na Antonio di Natalie katika dakika ya 67 akimaliza kazi nzuri ya Bruo Fernandes.
Kwa kipigo hicho Milan imeendelea kusalia na pointi 35, ikiwa ni kama nusu ya pointi ilizonazo vinara na watetezi wa ligi hiyom Juventus yenye pointi 69 na inayotarajiwa kushuka dimbani leo kukamilisha mchezo wake wa 27.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa jana Catania na Cargliari zilitoka sare ya kufungana bao 1-1.









No comments:

Post a Comment