STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 9, 2014

Hull City, Sheffield Utd zaifuata Arsenal Nusu Fainali FA

Curtis Davies scores for Hull City
Hull City na Sunderland walipoumana leo
John Brayford
Huree tumefuzu mmoja wa wafungaji wa Sheffield Unitd akishangilia bao lake lililoivusha timu hiyo ya daraja la chini kutinga hatua hiyo ya Nusu Fainali tangu Wycombe Wanderers kufanya hivyo mwaka 2001.
TIMU ya Hull City imepata ushindi wa kishindo na kufuzu nusu fainali ya Kombe la FA kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1930 baada ya kuitambia Sunderland kwa mabao 3-0, huku Sheffeld United ikipenya hatua hiyo kuifuata Arsenal iliyotangulia jana kwa kuilaza Charlton Athletic kwa mabao 2-0.
Katika mechi ya kwanza Ryan Flynn aliifungia Sheffeld bao la kuongoza dakika ya 65 kabla ya dakika mbili baadaye John Brayford aliongeza la pili na kufuzu hatua hiyo baada ya miaka mingi, huku katika mechi ya pili Sunderland ilibanwa na wenyeji wao na kukubali kipigo hicho cha aibu na kuiondosha patupu.
Mabao ya Curts Davies katika dakika ya 68 kabla ya Meyler akaongeza la pili dakika ya 72 na Fryatt akafunga la tatu na kuihakikishia Hull City ikifuzu Nusu Fainali.
Mechi nyingine ya kuhitimisha robo fainali za michuano hiyo, Manchester City wenyewe wapo njiani sasa wakiumana na Wigan Athletic ambao wameshatangulia kupata mabao 2-0 ikiwa ni kipindi cha pili.

No comments:

Post a Comment