STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 9, 2014

Manchester City yatupwa nje FA Cup

James Perch
City wakitunguliwa bao
NDOTO za kocha Manuel Pellegrini kunyakua mataji manne kwa mpigo msimu huu katika michuano mbalimbali inayoshiriki klabu yake ya Manchester City imeanza kuyeyuka baada ya kung'olewa kwenye hatrua ya Robo Fainali na Wigan Athletic muda mfupu uliopita.
City ikiwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Etihad, imejikuta ikinyukwa mabao 2-1 na Wigan na kushindwa kukutana na Arsenal kama wengi walivyokuwa wakitarajia na kuona ndoto za kocha huyo kutoa Chile zikitimia.
Mabao ya Jord Gomes kwa mkwaju wa penati dakika ya 27 na jingine la pili la dakika ya 47 lililofungwa na James Perch yalitosha kuizima wababe hao wa Manchester City licha ya Samir Nasir kufunga bao dakika ya 68 lililoshindwa kuisaidia timu yake.
Kwa ushindi huo sasa, Wigan inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza itaumana na Arsenal kwenye mechi ya Nusu Fainali, huku nusu fainali nyingine ikizikutanisha Hull City dhidi ya Sheffield United.

No comments:

Post a Comment