STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 9, 2014

CS Sfaxien, Cotonsport, AS Vita nazo zafuzu Afrika, Yanga ipo dimbani wakiwakimbiza Ahly Niyonzima nje

http://www.africatopsports.com/wp-content/uploads/2013/09/CS_SFAXIEN_ONZE.jpg
CS Sfaxien waliyofuzu hatua ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika
AS. VITA CLUB
AS Vita ya DR Congo
CS Sfaxien ikiwa nyumbani nchini Tunisia imeizamisha Dedebit ya Ethiopia kwa mabao 2-0 na kufuzu katika raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao 4-1.
Katika mechi yao ya kwanza mjini Addis Ababa, Dedebit ilifungwa mabao 2-1.
Nayo timu ya Coton Spors ilifungwa bao 1-0 ugenini wiki iliyopita nchini Burundi leo ikiwa nyumbani imeifanyia mauaji ya kutisha Flambeau de l'Est kwa kuifumua mabao 5-0 na kufuzu kwa jumla ya mabao 6-1.
Mchezo mwingine uliochezwa DR Congo imeshuhudia AS Vita ikifuata nyayo za ndugu zao TP Mazembe kusonga mbele baada ya kuiondosha patupu Dyanamos ya Zambia kwa kuilaza bao 1-0.
Dynamos iliyolazimishwa suluhu katika mechi yao ya nyumbani ilishindwa kufurukuta kwa wenyeji hao na kujikuta wakilala 1-0 ugenini.
Yanga kwa sasa ipo dimba la Alexandria ikiumana na Al Ahly ambapo mpaka sasa hakuna timu iliyoona lango la wenzake na timu zimeenda mapumziko.
Kikosi cha Yanga kipo hivi;
Deo Munishi, Mbuyi Twite, Oscar Joshua, Nadir Cannavaro, Kelvin Yondani, Frank Dumayo, Simon Msuva, Mrisho Ngassa, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza na Emmanuel Okwi. 

No comments:

Post a Comment