STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 2, 2014

Manchester City yatwaa taji la Capital One


KLABU ya Manchester City jioni hii imenyakua taji lake la kwanza kati ya manne ambayo kocha wae, Manuel Pellegrini alitangaza kuyawinda kwa msimu huu baada yta kuifumua Sunderland katika Fainali ya Kombe la Ligi (Captital One).
Pellegrini aliahidi mwezi uliopita kwamba timu yake itanyakua mataji manne likiwemo hilo la Ligi, FA, Ligi ya Mabingwa Afrika na Ligi Kuu ya England.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Wembley ilishuhudiwa Sunderland ikitangulia kupata bao kupitia kwa 
Fabio Borini katika dakika ya 10 na kudumu hadi mapumziko.
hata hivyo kipindi cha pili Man City ilicharuka na kusawazisha bao dakika ya 55 kupitia kwa Mchezaji Bora wa Afrika, Yaya Toure kabla ya Samir Nasir kuongeza la pili dakika ya moja baadaye na Jesus Navas kuongeza la tatu dakika ya 90.






No comments:

Post a Comment