STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 4, 2015

Didier Drogba kustaafu rasmi mwishoni mwa msimu

Atakapostaafu Didier Drogba atakuwa msaidizi wa Jose Mourinho kwenye benchi la ufundi.NYOTA wa Ivory Coast anayechezea klabu ya Chelsea Didier Drogba anatarajiwa kutangaza kustaafu kuichezea klabu hiyo mara baada ya kumalizika kwa msimu huu akiwa amerejea Chelsea akitokea Galatasaray ya Uturuki .
Drogba ambaye kwa Chelsea anahesabika kama gwiji  ametengenezewa nafasi ya kubaki ndani ya klabu hiyo mara atakapostaafu ambapo ataendelea kuwepo chini ya kocha Mreno Jose Mourinho .
Drogba anatarajiwa kukaa kwenye benchi la Chelsea akiwa mmoja wa makocha wasaidizi wa Mourinho jukumu ambalo nyota huyu wa Afrika ameafiki kulichukua baada ya kukubali kuwa hawezi kuendelea kucheza katika kiwango cha juu .
Drogba amepanga kustaafu mwishoni mwa msimu huu .
Drogba amepanga kustaafu mwishoni mwa msimu huu .
Drogba alijiunga na Chelsea akitokea klabu ya Olympique Marseille mwaka 2003 ambapo aliichezea klabu hiyo kwa miaka 9 ambapo alifanikiwa kutwaa mataji kadhaa huku akijijengea sifa ya kuwa nyota wa mechi kubwa kutokana na uwezo wake w akufunga mabao muhimu kwenye mechi kubwa zikiwepo hatua za nusu fainali na fainali .
Atakapostaafu Didier Drogba atakuwa msaidizi wa Jose Mourinho kwenye benchi la ufundi.
Drogba alirudi Chelsea msimu huu baada ya kuondoka mwaka 2012 wakati klabu hiyo ilipotwaa ubingwa wa ulaya baada ya kuifunga Bayern Munich ya Ujerumani huku Drogba akifunga penati ya mwisho iliyoipa Chelsea ubingwa .

No comments:

Post a Comment