STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 4, 2015

Bingwa Malembeka Cup kunyakua RAV4

http://thechronicleherald.ca/sites/default/files/imagecache/ch_article_main_image/articles/2006_Toyota_RAV4_08web.jpgDIWANI wa Kata ya Msongola, Jimbo la Ukonga, Wilaya ya Ilala Mkoa wa Dar es Salaam Angelina Malembeka amesema mshindi katika kombe la Malembeka ataibuka na gari aina RAV4 na mshindi wa kila Kata atapa pikipiki moja aina ya Honda.
Malembeka aliyasema hayo jana wakati akizungumza jijini Dar es Salaam ambapo alibainisha kuwa katika mashindano hayo timu 89 kutoka katika Kata nane.
Alisema lengo la kuandaa mashindano hayo ni kuhakikisha kuwa vijana ambao wana vipaji katika jimbo hilo wanatumia ipasavyo na kuwasaidia kupata soko katika timu kubwa.
Diwani huyo ambaye pia ni Katibu wa Madiwani wa Wilaya ya Ilala alisema katika mashindano hayo kila kata inashiriki ambapo mshindi ataibuka na pikipiki moja aina ya Honda.
Katibu huyo wa Madiwani wa Ilala alisema baada ya timu kushindana katika ngazi ya Kata timu tatu bora zitaingia katika hatua ya pili ambapo ziicheza hadi msindi wa jumla apatikane.
"Nimeandaa mashindano ya mpira wa miguu ambapo timu 89 kutoka Kata nane zimeshiriki na bingwa atapata RAV4 na washindi wa kata watapata pikipiki," alisema Malembeka.
Malembeka alisema jitihada zake ni kuhakikisha kuwa michezo yote ambayo ipo inachezwa katika Jimbo na Kata yake ambapo kwa kuanza ameanza na mpira wa miguu na bao.
Alisema bao ameanza katika Mitaa tisa ya Kata yake ya Msongole ambapo kwa sasa yupo katika mkakati wa kuandaa mashindano.

No comments:

Post a Comment