STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 4, 2015

Xavi aiponda CAS kutupa rufaa ya Barcelona

http://cdn.inquisitr.com/wp-content/uploads/2014/10/Xavi-On-His-Way-To-Man-Utd.jpg
Xavi
KIUNGO mahiri wa Barcelona Xavi, ameiponda Mahakama ya Michezo ya Kimataifa-CAS kwa uamuzi wake wa kutupilia mbali rufani ya klabu hiyo wakipinga adhabu ya kufungiwa kusajili na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA.
Barcelona walipewa adhabu hiyo kutokana na kupatikana na hatia ya kusajili wachezaji chini ya umri wa miaka 18 kutoka nje ya Hispania na baadae kukata rufani CAS ambayo katika maamuzi yake ilitupilia mbali. Uamuzi huo utaifanya Barcelona kushindwa kusajili mchezaji wa aina yeyote kwa mwaka huu na Xavi anadhani adhabu hiyo haijatenda haki.
Xavi ambaye ni nahodha wa Barcelona amesema wote wameshangazwa na uamuzi huo wa CAS kwani walitegemea kupunguza adhabu hiyo ambayo inaonekana kuwa kali kuliko kosa lenyewe.
Hata hivyo Xavi anaamini kuwa Barcelona bado ina vipaji vya kutosha vya kuifanya kuwa tishio katika kila mchezo wanaocheza.

No comments:

Post a Comment