STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 4, 2015

Yanga yazidi kutisha Zenji yaua tena ikifuzu robo fainali

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2014/12/IMG_0557-0.jpgWAKATI mabingwa watetezi wa Kombe la Mapinduzi, KCCA ya Uganda ikipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mtende, Yanga imeendeleza undava wake baada ya kuinyoa Polisi kwa mabao 4-0.
Yanga ilipata mabao yake kupitia kwa Andrey Coutinho aliyefunga mawili na mengine kuwekwa kimiani na Kpeh Sean Sherman na Simon Msuva.
Coutinho alifunga baoa lwa kuongoza dakika ya 27 kabla ya Mliberia kuongeza la pili dakika ya 33 na kufanya timu ziende mapumziko Yanga wakiwa mbele kwa mabao 2-0.
Kipindi cha pili Yanga waliendelea kuonyeshja dhamira yao kwamba wanalitaka taji hilo linaloshikiliwa na KCCA, baada ya Coutinho kuongeza la tatu kwa mkwaju wa adhabu ndogo dakika ya 56 na Msumva kufunga bao la nne la mchezo wa leo na la nne kwake katika michuano hiyo dakika kumi kabla ya mchezo kumalizika.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo, KCCA iliwalaza Mtende mabao 3-0 na Shaba ililala kwa bao 1-0 kwa Taifa ya Jang'ombe ambao walikandikwa mabao 4-0 na Yanga katika pambano lao lililopita.
Pambano linaloendelea kwa sasa ni kati ya Mabingwa wa Zanzibar KMKM inayoumana na mabingwa wa Tanzania Bara., Azam na matokeo kwa sasa bado 1-0, Azam wakiongoza dakika ikiwa ya 73.

No comments:

Post a Comment