STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 12, 2015

Mchungaji auwawa Kanisani akiendesha ibada

Security officers examin the lifeless body of an assistant pastor George Karidhimba Muriki of the Maximum Revival Ministries Church after he was shot dead by...
maafisa wa Polisi wakimsaidia msaidizi wa mchungaji aliyeuwawa nje ya kanisa hilo (Picha:AP)
WATU wenye silaha wasiofahamika walimfyatulia risasi na kumuuwa mchungaji mmoja wakati wa ibada kanisani siku ya jumapili katika mji wa Mombasa nchini Kenya  maahala ambako polisi wanapambana na vijana wa ki-islam wenye msimamo mkali.
Mauaji hayo yalitokea ndani ya mlango mkuu wa kuingilia kwenye kanisa la Maximum Revival Centre katika mtaa wa majengo. 
Mashahidi wanasema polisi waliwazuia watu wenye silaha kuingia ndani ya kanisa na kuuwa waathirika Zaidi. Watu hao wenye silaha hawajafahamika  lakini kundi la wanamgambo wa Al-Shabab kutoka nchi jirani ya Somalia limeshambulia malengo kadhaa nchini Kenya. Kundi hilo la Al-Shabab liliapa kulipiza kisasi kwa majeshi ya Kenya kuwepo nchini Somalia kwa ajili ya kusaidia  wanajeshi wa serikali dhidi ya wanamgambo hao.
VOA

No comments:

Post a Comment