STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 12, 2015

Manchester United yapigwa nyumbani, yaporomoka EPL

Dusan Tadic (second right) pounces upon the rebound and converts coolly to hand Southampton the lead against Manchester United
Dusan Tadic akifunga bao pekee la Southampton
Southampton captain Jose Fonte led from the back for Southampton and kept Robin van Persie from having any impact on the game
van Persie akiwania mpira na Jose Fonte
Juan Mata (right) missed a number of good chances to level the scores shortly after Southampton went ahead against United
Juan Mata akijaribua kufunga bao
United captain Wayne Rooney cut a dejected figure as he left the pitch after the full time whistle was blown
Nahodha Wayne Rooney akiwa haamini kama wamepigwa kidude nyumbani
KLABU ya Manchester United licha ya kucheza uwanja wa nyumbani na ikiwa imefarijika kwa kurejea dimbani kwa baadhi ya nyota wake waliokuwa majeruhi imeshindwa kufurukuta baada ya kuchapwa bao 1-0 na Southampton katika mechi ya Ligi Kuu ya England.
Bao pekee la wageni ambao ni maarufu kama 'Watakatifu' lililowanyong'onyesha Mashetani Wekundu liliwekwa kimiani katika dakika ya 69 na Dusan Tadic na kuwafanya Southampton kukwea hadi nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo wakiiengua Manchester United.
Ushindi umeifanya Southampton ambayo imelipa kisasi cha kufungwa nyumbani mwezi uliopita kwa mabao 2-1 na wapinzani wao kufikisha pointi  39, mbili zaidi ya ilizonazo vijana wa Luis Van Gaal licha ya zote kucheza mechi 21 kila moja.
Pia ni ushindi wa kwanza wa vijana wa Ronald Koeman katika uwanja wa Old Trafford tangu miaka 27 iliyopita kitu ambachop kimempa faraja kubwa koxcha huyo Mholanzi aliyewahi kuwa msaidizi wa Van Gaal.

No comments:

Post a Comment