STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 12, 2015

Messi azikata maini zinazomnyemelea, adai haiendi kokote

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/72166000/jpg/_72166204_hi020543910.jpg
Siendi Kokote
NYOTA wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi amesisitiza kuwa haendi kokote wakati kukiwa na taarifa za kuhusishwa kunyemelewa na Chelsea na Manchester City.
Messi alisema klabu hizo zinazodaiwa kutaka kumnyakua 'wote ni waongo' na kwamba atasalia katika klabu yake ya Barcelona.
Mshambuliaji huyo wa Argentina ambaye jana alifunga bao la tatu wakati timu yake ikishinda nyumbani 3-1 dhidi ya Mabingwa watetezi alidai taarifa zote kwamba anataka kuondoka Nou Camp ni uzushi.
"Sijaulizwa chochote kuhusu kusalia hapa kwa sababu sitaki kwenda kokote kwa sasa," alisema Messi.
Aliongeza kuwa anasikia kwamba amefanya mazungumzo na klabu za Chelsea na Manchester City kwa ajili ya kujiunga na Ligi Kuu tya England na kudai 'klabu zote hizo ni waongo'.
Akihojiwa na kituo cha TV ya klabu hiyo katika kipindi cha El Marcador alisema
"Nimesikia kwamba nimefanya mazungumzo na Chelsea na (Manchester) City....lakini ni uongo mtupu."
Taarifa kwamba kuna ufa mkubwa baina ya Messi na Kocha wake, Luis Enrique zimechochea taarifa za ama Messi au kocha huyo kung'oka Nou Camp.
Messi amekanusha pia taarifa kwamba amekuwa sehemu ya kutimuliwa kwa majkocha na wachezaji ndani ya klabu hiyo kwa kudai hakuna kitu kama hicho.
"Kuna taarifa nyingi juu ya mahusiano mabovu baina ya (Pep) Guardiola, (Samuel) Eto'o, (Zlatan) Ibrahimovic Bojan (Krkic) hakuna ukweli wowote," alisema.
Mchezaji huyo alisema amechoka kusikia habari za uzushi kuhusu yeye.

No comments:

Post a Comment