STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 12, 2015

Wakala wa Ronaldo atwaa tuzo kwa mara ya 5 mfululizo

http://globesoccer.wpengine.netdna-cdn.com/wp-content/uploads/2014/05/Globe-Soccer-Awards-2371.jpgWAKALA wa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo amefanikiwa kunyakuwa tuzo ya wakala bora kwa mara ya tano mfululizo ijulikanayo kama Globe Soccer Awards.
Wakala huyo Jorge Mendes amepewa tuzo hiyo kwa kutambua mafanikio yake kama wakala wa wachzaji mojawapo akiwa Ronaldo.
Mendes ambaye kwa mara kwanza kunyakuwa tuzo hiyo ilikuwa mwaka 2010 amekuwa akiwasimamia wachezaji bora kabisa duniani ambapo mbali ya Ronaldo mwingine ni James Rodriguez na hata meneja wa Chelsea Jose Mourinho.
Ronaldo ndio aliyenyakuwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka inayotolewa na Globe Soccer huku meneja wa Madrid Carlo Ancelotti akinyakuwa tuzo ya kocha bora.

No comments:

Post a Comment