STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 12, 2015

Rama Pentagone wa Twanga Pepeta Tajiri Penzi

MUIMBAJI mahiri wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta', Ramadhan Mhoza 'Pentagone' amefyatua wimbo wake binafsi uitwao 'Tajiri Penzi'.
Wimbo huo uliorekodiwa kwa mtayarishaji Amaroso ni utambulisho wa albamu binafsi ya muimbaji huyo wa zamani wa bendi ya Double M Sound, Levent Musica na Extra Bongo.
Akizungumza na MICHARAZO, Pentagone alisema wimbo huo ulio katika mahadhi ya rhumba ni kati ya nyimbo zitakazokuwa katika albamu yake aliyopanga kuitoa baadaye mwaka huu.
"Katika kutimiza ahadi yangu kwa mashabiki, nimetengeneza wimbo mpya uitwao 'Tajiri Penzi' ambao upo katika miondoko ya rhumba na ni kazi yangu binafsi nje ya Twanga Pepeta," alisema.
Pentagone alisema kwa sasa anajipanga kwa ajili ya kutengeneza video ya wimbo huo kabla ya kuanza kurekodi nyimbo nyingine kukamilisha albamu yake ya kwanza itakayokuwa na jumla ya nyimbo sita au nane

No comments:

Post a Comment