STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 12, 2015

Nani kuwa Mwanasoka Bora wa FIFA leo, Ni Ronaldo au Messi?

http://static.goal.com/672500/672581_herol.jpg 
KITENDAWILI cha Nani kuwa Mwanasoka Soka wa Dunia wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA Ballon d'Or 2014 kinatarajiwa kutenguliwa leo wakati mshindi atakapotangazwa.
Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo kutoka Ureno, Lionel Messi Muargentina anayeichezea Barcelona na kipa Manuel Neuer Mjerumani wa klabu ya Bayern Munich ndiyo wanaochuana kwenye tuzo hizo.
Messi anayeshikilia rekodi ya kunyakua tuzo hizo mara nne safari hapewi nafasi kubwa kama Ronaldo ambaye anaishikilia kwa sasa tuzo hiyo.
Hata hivyo kitendo cha kuvunja rekodi mbalimbali na kuifikisha timu yake kwenye fainali inampa nafasi ya kumuangusha Ronaldo, ingawa haitegemewi.
Wafuatiliaji wa soka wanaamini wachezaji wote watatu walioingia kwenye fainali wanastahili kunyakua tuzo hiyo, huku kipa Neuer akipigiwa chapuo kwa kuiwezesha timu yake ya taifa kutwaa ubingwa wa Dunia katika fainali za Kombe la Dunia za Brazil.
Je ni Messi, Ronaldo au Neuer atakayenyakua tuzo hiyo hiyo leo huko Uswisi zitakapotolewa.

No comments:

Post a Comment