STRIKA

USILIKOSE

Friday, February 1, 2013
TEGETE, MAFTAH WATOSWA STARS ITAKAYOIVAA CAMEROON
Mshambuliaji nyota wa Yanga, Jerryson Tegete |
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametaja kikosi cha wachezaji 21
kitakachoingia kambini siku ya Jumapili kwa ajili ya
mechi ya kirafiki dhidi ya Cameroon (Indomitable Lions), huku akiwaacha mshambuliaji aliyerejea kwa kasi, Jerryson Tegete na beki wa kushoto, Amir Maftah.
Akitangaza kikosi hicho jana, Poulsen aliwataja wachezaji watakaoingia kambini ni makipa Juma Kaseja (Simba), Mwadini
Ali (Azam) na Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Erasto Nyoni (Azam),
Nassoro Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Nadir Haroub (Yanga),
Kelvin Yondani (Yanga), Shomari Kapombe (Simba) na Issa Rashid (Mtibwa
Sugar).
Viungo
ni Amri Kiemba (Simba), Simon Msuva (Yanga), Frank Domayo (Yanga),
Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Salum Abubakar (Azam), Khamis Mcha (Azam),
Athuman Idd (Yanga) na Mwinyi Kazimoto (Simba). Washambuliaji ni Mrisho
Ngasa (Simba), na Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea timu ya
TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
Kocha Poulsen, alisema mechi dhidi ya Cameroon itakuwa kipimo kizuri kwake kwa sababu
ni sehemu ya maandalizi kabla ya kucheza mechi ya mchujo ya Kombe la
Dunia dhidi ya Morocco itakayofanyika Machi mwaka huu.
“Itakuwa
mechi ngumu na kipimo sahihi kwetu. Tuko tayari, tutacheza kwa staili
yetu kwa sababu ni sehemu ya maandalizi kabla ya mechi dhidi ya Morocco.
Ni mechi nzuri kwa sababu wachezaji wameonyesha wako tayari.
“Tumetoka
kucheza dhidi ya Zambia na Ethiopia. Lengo ni Taifa Stars kucheza
fainali za AFCON 2015, kwa hiyo mechi dhidi ya Cameroon ni sehemu ya
mipango yetu kuhakikisha tunafika huko,” amesema Kim ambaye amerejea
nchini juzi kutoka Afrika Kusini kuzifuatilia timu za Morocco na Ivory
Coast zilizo kundi moja na Tanzania katika mechi za mchujo za Kombe la
Dunia.
Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itacheza na Morocco,
Machi 24 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Stars inashika nafasi
ya pili katika kundi lake nyuma ya Ivory Coast inayoongoza. Timu
nyingine katika kundi hilo ni Gambia.
PINGAMIZI DHIDI YA MALINZI, MANJI, WAMBURA YATUPWA TFF
![]() |
Angetile Osiah, Katibu wa Kamati ya Uchaguzi |
1. Waombaji uongozi wa TPL Board
(a) Pingamizi dhidi ya Ndg. Said Muhammed Abeid anayeomba kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi (TPL Board): Kamati ilijadili pingamizi iliyowasilishwa na Ndg. Frank M. Mchaki dhidi ya Ndg. Said Muhammed, aliyeoomba Kamati ya Uchaguzi ya TFF kumwondoa mwombaji uongozi kugombea nafasi aliyoomba, kwamba Ndg. Said Muhammed:
(i) Si Mwenyekiti wa Klabu ya Azam na hivyo hana sifa za kugombea uongozi wa TPL Board.
(ii) Si mkweli katika maelezo aliyoyatoa kwenye fomu yake ya maombi ya uongozi.
Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilipitia maelezo ya Mweka pingamizi na ilijiridhisha kuwa pingamizi iliyowasilishwa mbele yake na Ndg. Mchaki haikukidhi matakwa Kanuni za Uchaguzi za TFF Ibara ya 11(2) kwa kuwa haikuambatanishwa na vielelezo vyovyote kuthibitisha maelezo ya pingamizi. Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeitupa pingamizi hiyo.
(b) Pingamizi dhidi ya Ndg. Yusufali Manji anayeomba kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi (TPL Board): Kamati ilijadili pingamizi zilizowasilishwa na Ndg. Daniel T. Kamna na Ndg. Juma Ally Magoma walioomba Kamati ya Uchaguzi ya TFF kumwondoa mwombaji uongozi kugombea nafasi aliyoomba, kwamba Ndg. Yusufali Manji:
(i) Hana uzoefu wa uendeshaji wa Mpira wa Miguu uliothibitishwa wa angalau miaka mitano (5) wa uendeshaji wa mpira wa miguu.
(ii) Hana sifa ya kuwa ama mchezaji Mpira wa Miguu, Kocha, Mwamuzi au kushiriki katika uendeshaji wa Mpira wa Miguu katika ngazi ya Mkoa au Ligi daraja la kwanza.
(iii) Hana elimu ya kidato cha nne
(iv) Ameshindwa kusimamia katiba ya Young Africans Sports Club Ibara ya 10(6), 18(1)b, 27 (2) na (5).
Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilipitia pingamizi hizo na ilijiridhisha kuwa pingamizi zilizowasilishwa mbele yake na Ndg. Daniel T. Kamna na Ndg. Juma Ally Magoma hazikukidhi matakwa Kanuni za Uchaguzi za TFF Ibara ya 11(2) kwa kuwa hazikuambatanishwa na vielelezo vyovyote kuthibitisha maelezo ya pingamizi. Kamati ya Uchaguzi ya TFF imezitupa pingamizi hizo.
(c) Pingamizi dhidi ya Ndg. Hamad Yahya Juma anayeomba kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi (TPL Board): Kamati ilijadili pingamizi iliyowasilishwa na Ndg. Frank M. Mchaki dhidi ya Ndg. Hamad Yahya Juma, kwamba Ndg. Hamad Yahya Juma:
(i) Si Mwenyekiti wa Klabu ya Mtibwa na hivyo hana sifa za kugombea uongozi wa TPL Board.
(ii) Si mkweli na mwadilifu na amekuwa akijipachika cheo cha mwenyekiti wa klabu.
Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeitupa pingamizi ya Ndg. Frank M. Mchaki kwa kuwa pingamizi iliyowasilishwa mbele yake haikukidhi matakwa ya Kanuni za Uchaguzi za TFF Ibara ya 11(2) kwa kutoambatanishwa na vielelezo vyovyote kuthibitisha maelezo ya pingamizi.
2. Waombaji uongozi wa TFF
(a) Pingamizi dhidi ya Ndg. Athumani K. Kambi anayeomba kugombea nafasi ya Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF kupitia Kanda ya 9 (Mtwara na Lindi): Ndg. Kambi aliwekewa pingamizi kwamba amefanya Kampeni kabla ya muda uliopangwa.
Kamati imeitupa pingamizi ya Ndg. Jeremiah John Wambura kwa kuwa mweka pingamizi hakutokea wakati alipotakiwa kufika kwenye Kamati ya Uchaguzi kutoa utetetezi wake kuhusu pingamizi.
(b) Pingamizi dhidi ya Ndg. Eliud P. Mvella anayeomba kugombea nafasi ya Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF kupitia Kanda ya 7 (Iringa na Mbeya): Ndg. Mvella aliwekewa pingamizi na Ndg. Said Kiponza, Ndg. Abu Changawa na Ndg. Peter Naminga, kwamba Ndg. Mvella:
(i) Akiwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF kupitia Kanda hiyo ameshindwa kuleta maendeleo ya soka katika ukanda huo.
(j) Ana kesi ya rushwa katika mahakama ya wilaya ya Iringa
Kamati imeitupa pingamizi hiyo kwa kuwa haikukidhi matakwa ya Kanuni za Uchaguzi za TFF Ibara ya 11(2) kwa kutoambatanishwa na vielelezo vyovyote kuthibitisha maelezo ya pingamizi.
(c) Pingamizi dhidi ya Ndg. Epaphra Swai anayeomba kugombea nafasi ya Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF kupitia Kanda ya 3 (Shinyanga na Simiyu): Kamati ilijadili pingamizi zilizowasilishwa na Ndg. Ramadhani Sesso na Ndg. Tsotsie Chalamila, kwamba Ndg. Epaphra Swai:
(i) Alifanya ubadhilifu wa fedha alipokuwa Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA).
(ii) Alitumia madaraka yake vibaya alipokuwa MZFA kujinufaisha kwa kutumia MZFA.
(iii) Alivunja Katiba ya MZFA na FIFA
(iv) Anavuruga shughuli za uendeshaji mpira wa miguu mkoani Simiyu.
Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilipitia pingamizi hizo na ilijiridhisha kuwa wawekaji pingamizi hawakuwa na sababu za msingi zilizoambatana na vielelezo vinavyothibitisha maelezo ya pingamizi na kuwa pingamizi zilizowasilishwa mbele yake zina chembechembe za wazi za mapatano ya hila na udanganyifu (collusion) dhidi ya Ndg. Epaphra Swai. Kwa kutokidhi matakwa ya Kanuni za Uchaguzi za TFF Ibara ya 11(2) na hila/udanganyifu kwa Kamati, Kamati ya Uchaguzi ya TFF imezitupa pingamizi hizo.
(d) Pingamizi dhidi ya Ndg. Vedastus F.K Lufano na Ndg. Mugisha Galibona wanaoomba kugombea nafasi ya Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF kupitia Kanda ya 2 (Mwanza na Mara): Ndg. Lufano na Ndg. Galibona waliwekewa pingamizi na Ndg. Paul Mhangwa kwamba hawana uzoefu wa uendeshaji wa Mpira wa Miguu wa miaka mitano (5).
Kamati imeitupa pingamizi hiyo kwa kuwa haikuzingatia Kanuni za Uchaguzi za TFF Ibara ya 11(2).
(e) Pingamizi dhidi ya Ndg. Michael R. Wambura anayeomba kugombea nafasi ya Makamu wa Rais wa TFF: Pingamizi ziliwasilishwa na Ndg. Said Rubea Tamim na Ndg. Josea Samuel Msengi kwamba Ndg. Wambura:
(i) Alikiuka Katiba ya TFF kwa kuishitaki Klabu yake ya Simba mahakamani kuhusu masuala ya uchaguzi.
(ii) Alikosa uadilifu kwa kutumia kampuni yake binafsi kufanya biashara na Taasisi aliyokuwa aniongoza akiwa Katibu Mkuu wa FAT.
(iii) Amekuwa akijaribu kupotosha umma kwamba vyombo vya TFF havifanyi kazi zake kwa kutumia haki na kuviita ‘Mahakama za Kangaroo (Kangaroo Courts).
(iv) Mwaka 2004 alikiri kwamba alikuwa akiandikwa vizuri na vyombo vya habari kwa kuwa alikuwa akivipa pesa na kwamba vyombo vya habari vilimgeuka kwa sababu aliacha kuwapa waandishi pesa.
(v) Mwaka 2004 alikataa kutekeleza maagizo ya FIFA ya kutaka nafasi ya Katibu Mkuu wa FAT iwe ya kuajiliwa.
(vi) Alikosa uwezo wa kutekeleza wajibu na malengo ya TFF.
Ndg. Josea Samuel Msengi aliondoa pingamizi lake dhidi ya Ndg. Wambura. Kamati imelitupa pingamizi la Ndg. Said Rubea Tamim kwa kuwa halikukidhi matakwa ya Kanuni za Uchaguzi za TFF Ibara ya 11(2).
(f) Pingamizi dhidi ya Ndg. Jamal E. Malinzi anayeomba kugombea nafasi ya Rais wa TFF; Aliwekewa Pingamizi na Ndg. Agape Fue kwamba:
(i) Alivunja Katiba ya TFF kwa kufanya jitihada kubwa za kuhakikisha kuwa wanachama wa TFF kikiwemo Chama chake cha Mkoa wa Kagera haviheshimu wala kutekeleza maagizo ya TFF, CAF, CECAFA na FIFA baada ya Kamati ya Utendaji ya TFF kuwasilisha mapendekezo ya mabadiliko ya Katiba kwa njia ya Waraka, ambayo yalihusisha pia maagizo ya FIFA na CAF
(ii) Hana sifa ya uzoefu wa miaka mitano katika uongozi wa mpira wa miguu.
(iii) Anakosa uadilifu na haiba ya kuliwakilisha Shirikisho nje na ndani.
Kamati imeitupa pingamizi ya Ndg. Agape Fue kwa kuwa mweka pingamizi hakutokea wakati alipotakiwa kufika kwenye Kamati ya Uchaguzi kutoa utetetezi wake kuhusu pingamizi hilo.
(g) Pingamizi dhidi ya Ndg. Athumani J. Nyamlani anayeomba kugombea nafasi ya Rais wa TFF: Ndg. Nyamlani aliwekewa pingamizi na Ndg. Mintanga Yusuph Gacha na Ndg. Medard Justiniani kwamba:
(i) Ni Hakimu Mkazi katika Mahakama ya Tanzania na kwa maana hiyo ni mtumishi wa umma hivyo alikosa kigezo na sifa ya kugombea nafasi ya urais wa TFF.
(ii) Anakatazwa na Judicial Service Act, Public Service Act 2002 na Code of Conduct for Judicial Officers of Tanzania kugombea nafasi aliyoomba ya Rais wa TFF.
(iii) Kutakuwa na Mgoganao wa kimaslahi endapo Ndg, Nyamlani atachaguliwa kuwa Rais wa TFF.
(iv) Amekosa umakini na uadilifu kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake na kusababisha Akaunti za TFF kufungiwa na TRA.
Ndg. Mintanga Yusuph Gacha hakufika kutetea Pingamizi lake ni hivyo halikujadiliwa na Kamati. Kamati imelitupa pingamizi la Ndg. Medard Justiniani kwa kuwa alishindwa kuithibitishia Kamati kuwa alikuwa na ufahamu wa kutosha wa pingamizi lake ikiwa ni pamoja na viambatanisho vyake, hali iliyotanabaisha kuwa pingamizi hilo lilikuwa na chembechembe nyingi za hila na udanganyifu.
Imetolewa na:
Angetile Osiah
KATIBU
KAMATI YA UCHAGUZI
Thursday, January 31, 2013
BREAKING NEWS: DIZUMBA WA MAJIMAJI AFARIKI
HABARI zilizotufikia muda huu zinasema kuwa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Majimaji Songea inayojiandaa na duru la pili la Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara, Ahmed Dizumba amefariki dunia.
Taarifa zilizopatikana asubuhi hii ambazo MICHARAZO inaendelea kuzifuatilia kwa ukaribu zinasema Dizumba amefariki usiku wa kuamkia leo na anatarajiwa kuzikwa leo mjini Songea.
Kwa yeyote mwenye taarifa zaidi anaweza kutupenyezea, juu ya msiba huu ulioikumba Majimaji ikiwa katika harakati za kuanza duru la pili la ligi daraja la kwanza kuwania kurejea ligi kuu.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na TFF, Majimaji imepangwa kuanza utepe wa duru hilo kwenye uwanja wake wa Majimaji Songea kuvaana na Kurugenzi mechi ya kundi A.
Taarifa zilizopatikana asubuhi hii ambazo MICHARAZO inaendelea kuzifuatilia kwa ukaribu zinasema Dizumba amefariki usiku wa kuamkia leo na anatarajiwa kuzikwa leo mjini Songea.
Kwa yeyote mwenye taarifa zaidi anaweza kutupenyezea, juu ya msiba huu ulioikumba Majimaji ikiwa katika harakati za kuanza duru la pili la ligi daraja la kwanza kuwania kurejea ligi kuu.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na TFF, Majimaji imepangwa kuanza utepe wa duru hilo kwenye uwanja wake wa Majimaji Songea kuvaana na Kurugenzi mechi ya kundi A.
Mtibwa Sugar ipo tayari kuivaa Yanga, Mgosi majaribuni...!
![]() |
Kocha wa Mtibwa Mecky Mexime |
TIMU ya soka ya Mtibwa Sugar imesema imejiandaa vya kutosha kuweza kuwakabili vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga watakaovaana nao keshokutwa jijini Dar es Salaam.
Mtibwa inatarajiwa kuvaana na Yanga katika mfululizo wa mechi za ligi hiyo duru la pili ikiwa na kumbukumbu ya kipigo cha bao 1-0 walichopewa nyumbani kwao na Polisi Morogoro.
Katika pambano lao la awali Mtibwa iliisasambua Yanga mjini Morogoro kwa mabao 3-0, hali inayofanya pambano hilo la marudiano kuwa la aina yake, ndio maana benchi la ufundi la timu hiyo limedai kuwa limepania kurekebisha makosa mbele ya wapinzani wao wanaoongoza msimamo wa ligi hiyo kwa sasa.
Kocha wa Mtibwa, Mecky Mexime, amesema kuwa kikosi chao kipo katika hali nzuri kuweza kuikabili Yanga na kuendeleza ubabe wao, licha ya kukiri wanatarajia upinzani mkali.
Mexime, alisema hana shaka na pambano hilo kwa namna alivyoweza kurekebisha makosa yaliyowagharimu katika pambano lao lililopita walilopoteza nyumbani.
"Tumejiandaa na tupo tayari kuivaa Yanga na hatuna hofu yoyote, vijana wangu wapo kamili kuweza kurekebisha makosa yaliyotuponza kwa Polisi Moro," alisema Mexime.
Mexime, alisema ushindi pekee ndiyo kitu kinachohitajika kwa Mtibwa ili kuweza kujipanga kwa ajili ya kumaliza nafasi za juu mwishoni mwa msimu.
Mbali na mechi hiyo ya Yanga na Mtibwa, siku hiyo ya jumamosi kutakuwa na mechi nyingine kadhaa kabla ya Jumapili Mabingwa watetezi, Simba kuvaana na JKT Ruvu ambayo .inatarajiwa kumtumia nyota wqa zamani za Msimbani Mussa Hassani Mgosi kuweza kuwasimamisha Simba walioilaza Africans Lyon katika mechi yao iliyopita.
Manchester United yazidi kujichimbia kileleni Ligi ya England
![]() |
Rooney akipachika mpira wavuni |
MABAO mawili yaliyopachikwa wavuni na mshambuliaji Wayne Rooney imeiwezesha Manchester United kuendelea kujikita kileleni mwea msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kuilaza Southampton kwa mabao 2-1 katika mfululizo wa ligi hiyo.
Mashetani hao Wekundu waliokuwa uwanja wao wa nyumbani wa Old Trafoord, walijikuta wakishtukizwa kwa kufungwa bao la mapema na wageni wao lililofungwa na Jay Rodriguez dakika ya tatu tu ya mchezo huo, hata hivyo dakika tano baadae Rooney aliwatuliza mashabiki wa timu yake kwa kusawazisha bao.
Rooney aliendelea kung'ara kwa kuongeza bao la pili dakika ya 27 akimalizia kazi nzuri ya Patric Evra na kufanya hadi mapumziko timu hizo ziwe zimefungana mabao 2-1 yaliyomudu hadi zilipomalizika dakika 90 za pambano hilo.
Kwa ushindi huo Manchester imeongeza pengo la pointi saba kati yao na wapinzani wao, Manchester City ambayo juzi ililazimishwa sare na kusalia na pointi zao 52 huku timu zote zikiwa zimecheza mechi 24 kila mmoja.
Katika mapambano mengine yaliyochezwa usiku wa jana, Liverpool iliwabana wenyeji wao Arsenal na kufungana nao mabao 2-2, huku Norwich City ilijikuta ikibanwa mbavu nyumbani kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1.
Nayo Reading iliing'ang'ania waliokuwa mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Chelsea kwa kufungana nao magoli 2-2 na Fulham iliicharaza West Ham United mabao 3-1 na Everton iliendeleza maajabu wake msimu huu kwa kupata ushindi wa mabao 2-1 mbele ya West Bromwich.
Ligi hiyo inatarajiwa kuingia mzunguko wa 25 mwishoni mwa wiki kwa mechi katika viwanja mbalimbali nchini humo.
![]() |
Rooney akishangilia moja ya mabao yake ya jana |
Balotelli ilibidi tu aondoke - Mancini
![]() |
Kocha Mancini akiwa na Balotelli wakipeana majukumu wakati walipokuwa pamoja Manchester City |
KOCHA wa Manchester City, Roberto Mancini amesema kuondoka
kwa Mario Balotelli kwenda AC Milan kunaifanya timu yake ipungukiwe wachezaji.
Sare yao ya 0-0 dhidi ya QPR usiku wa kuamkia jana iliwaacha
mabingwa wakiwa hatarini kupitwa zaidi na vinara Manchester United, ambao usiku
wa kuamkia leo walitarajiwa kucheza dhidi ya Southampton.
"Ni ngumu kwa sababu nimempoteza mchezaji mmoja muhimu
na ambaye angekuwa muhimu katika mechi 14 zijazo," alisema Mancini.
"Lakini ilikuwa ni muhimu kwa Mario kurejea Italia,
kurejea kwenye familia yake na kuchezea Milan."
Mancini anaamini kwamba Balotelli amefanya kazi "nzuri
sana" katika miaka yake miwili na nusu akiwa na Man City, ingawa amekubali
kwamba msimu huu ulikuwa mgumu zaidi kwa mshambuliaji huyo.
Mancini pia haraka alikanusha mtazamo kwamba kuondoka kwa
Balotelli kumetokana na ugumu wa kumdhibiti mshambuliaji huyo mtata.
"Hapana, hapana, hapana, siyo kwangu," alisema.
"Kwangu mimi, Mario alikuwa kama mwanangu mwingine.
"Mario yuko hivyo lakini anaweza kukufadhaisha wakati
mwingine.
"Klabu imeniambia kwamba imepokea ofa kutoka Milan.
Nilizungumza na Mario na nadhani alitaka uhamisho huu.
"Nadhani kwake kucheza miaka mitatu England na kisha
kurejea Italia itakuwa ni jambo zuri kwake."
Balotelli alitambulishwa rasmi jana na klabu yake mpya ya AC Milan akikabidhiwa jezi yenye namba kama alivyokuwa akiitumia alipokuwa City, 45.
AZAM, JKT OLJORO ZAZIDI KUPAA LIGI KUU BARA
TAIFA STARS KUIVAA CAMEROON WIKI IJAYO
Na Boniface Wambura
TANZANIA
(Taifa Stars) itacheza na Cameroon katika moja ya mechi za kirafiki za
Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)- FIFA Date
zitakazofanyika duniani kote Februari 6 mwaka huu.
Mechi
hiyo itafanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11
kamili jioni. Kikosi cha Cameroon kinachoundwa na wachezaji wengi wa
kulipwa wanaocheza katika nchi mbalimbali duniani kitaanza kuwasili
nchini Februari 3 mwaka huu.
Nchi
kadhaa ziliomba kucheza na Taifa Stars katika tarehe hiyo ya FIFA,
lakini Kocha wa Stars, Kim Poulsen ameamua kucheza mechi hiyo dhidi ya
Cameroon ambayo nahodha wake ni mchezaji nyota wa kimataifa, Samuel Etoo
Fils.
Congo
Brazzaville, Equatorial Guinea, Rwanda na Swaziland nazo zilikuwa
zimeomba kucheza dhidi ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro
Premium Lager. Ukiondoa Swaziland iliyotaka mechi hiyo ichezwe Dar es
Salaam, nyingine zilitaka kucheza nyumbani kwao.
Wakati
huo huo, Kocha Kim Poulsen atakutana na Waandishi wa Habari kuzungumzia
maandalizi ya mechi hiyo ikiwemo kutaja kikosi ambacho atakitumia.
Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Madrid yaidindia Barca Kombe la Mfalme
![]() |
Cesc Febregas akishangilia bao katika pambano la jana la El Clasico |
Ikicheza bila baadhi ya nyota wake kutokana na kutumikia adhabu na kuwa majeruhi, Real Madrid iliibana Barca na kwenda nao mapumziko wakiwa nguvu sawa bila kufungana.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Barcelona kuwashtua wenyeji wao kwa kujipatia bao la kuongoza lililofungwa dakika ya 50 na kiungo Cesc Fabregas akimalizia kazi nzuri ya Lionel Messi.
Timu hizo zilizoenda kushambuliana na kufanya kosa kosa kadhaa na kwenye dakika ya 81, wenyeji walifanikiwa kusawazisha bao hilo kupitia kwa Raphael Varane aliyemaliza kazi murua ilioyofanywa na Mjerumani Mesut Ozil.
Wapinzani hao wa jadi wa nchini Hispania wanatarajiwa kurudiana mwishoni mwa mwezi Februari, ambapo ndiyo itaamua hatma ya timu ipi itinge fainali za michuano hiyo kuungana na mshindi kati ya Sevilla na Atletico Madrid ambazo nufa fainali yao ya kwanza inatarajiwa kuchezwa kesho mjini Madrid kabla ya kwenda kurudiana nyumbani kwa Sevilla.
Katika pambano hilo la El Clasico lililoshuhudia Barcelona ikiwatumia wachezaji wake waliokuwa nje kwa muda mrefu kwa majereha, wachezaji sita, watatu kila upande wakionyeshwa kadi za njano kwa makosa mbalimbali.
Subscribe to:
Posts (Atom)