STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 13, 2014

Bao la TP Mazembe dhidi ya As Vita laua mashabiki 15 DR Congo


BAO pekee la dakika ya 35 lililofungwa na Gladson Awako wa TP Mazembe, klabu wanayochezea Watanzania  wawili Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu dhidi ya AS Vita katika mchezo wa Ligi Kuu ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) limesababisha vifo vya watu 15.
Ushindi huo kwenye Uwanja wa Tata Raphael, unaifanya TP Mazembe iendeleze ubabe wake kwa Vita baada kuifumua 4-1 katika mchezo wa mzunguko wa kwanza mjini Lubumbashi.
Timu hizo mbili zenye upinzani mkali pia zimepangwa kundi moja la Ligi ya Mabingwa Afrika na Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Issa Hayatou amehuzunishwa na vifo vya mashabiki zaidi ya 15 katika mechi hiyo huku 20 wakijeruhiwa baada ya Shirikisho la Soka DRC (Fecofa) kuipa CAF ripoti kamili ya kilichotokea.
Katika taarifa yake jana, Hayatou alisema bodi hiyo ya soka Afrika imesikitishwa na tukio hilo na kwamba wataweka mikakati ya kudhibiti vurugu viwanjani wakati wa mechi.
Hayatou raia wa Mcameroon ametoa pole kwa niaba ya CAF kwa familia za waliofiwa kutokana na vurugu hizo, Fecofa na kusema anatumai walioripotiwa kujeruhiwa wanapatiwa matibabu.
Juu ya hatua ambazo CAF itachukua kupambana na vurugu viwanjani, Hayatou alisema jana kuwa: "Aina yoyote ya vurugu haina nafasi kwenye uwanja wa soka. Lazima kuwe na sheria kali na ninawaagiza Fecofa na mamlaka husika DRC kufanya uchunguzi wa kina juu ya tatizo hili na kuhakikisha hatua kali zinachukuliwa ili isijirudie aina yoyote ya tukio kama hili."
Vurugu hizo zilianza baada ya filimbi ya mwisho ya mchezo huo, Mazembe yenye washambuliaji wawili Watanzania, Samatta na Ulimwengu ikishinda 1-0 na Polisi walijaribu kutuliza vurugu hizo kwa kulipua mabomu ya machozi.
Gavana wa Kinshasa, Andre Kimbuta mara moja aliagiza uchunguzi ufanyike juu ya tukio hilo.
Vurugu hizo zinatokea wakati Mazembe na AS Vita zimepangwa kundi moja katika Ligi ya Mabingwa Afrika na zitamenyana tena Mei 25, mwaka huu mjini Lubumbashi katika michuano hiyo ya Afrika. Mazembe iliifunga 4-1 Vita katika mchezo wa kwanza wa ligi ya DRC msimu huu Lubumbashi na inahofiwa mashabiki wa timu ya kina Samatta watalipa kisasi kwa mashabiki wa Vita Mei 25.
Rais wa Fifa, Sepp Blatter alieleza kupitia mtandao wa Twitter:  "Anasubiri habari zaidi kutoka DR Congo baada ya kuripotiwa tukio hilo. Huzuni yangu ni kwa wale waliopenda sana soka, ambao hawatarudi."

Shinji Kagawa aitwa kikosi cha Japan WC2014

WACHEZAJI nyota Keisuke Honda na Shinji Kagawa ni miongoni mwa wachezaji 23 walioteuliwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Japan kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Dunia mwezi ujao. Kocha Alberto Zaccheroni ambaye amekuwa kocha wa Japan toka mwaka 2010 amechagua wachezaji 12 wanaocheza soka barani Ulaya na 11 wanaocheza katika Ligi Kuu ya nchi hiyo maarufu kama J League. Honda anayecheza klabu ya AC Milan na Kagawa anayecheza Manchester United wanategemewa kwa kiasi kikubwa na nchi yao katika kuhakikisha wanavuka hatua ya makundi katika kundi C ambapo wamepangwa sambamba na Ivory Coast, Ugiriki na Colombia. Japan kwa kipindi kirefu imeshindwa kuwa na washambuliaji wa kutegemewa na Zaccheroni anatarajia kuwategemea Honda na Kagawa katika kutengeneza nafasi na kufunga mabao mengoi ya timu hiyo katika michuano hiyo.

Kikosi Kamili cha Japan:
Makipa: Shuichi Gonda (Tokyo), Eiji Kawashima (Standard Liege), Shusaku Nishikawa (Urawa Reds)

Mabeki: Masahiko Inoha (Jubilo Iwata), Yasuyuki Konno (Gamba Osaka), Masato Morishige (Tokyo), Yuto Nagatomo (Inter), Gotoku Sakai (Stuttgart), Hiroki Sakai (Hannover), Atsuto Uchida (Schalke), Maya Yoshida (Southampton)

Viungo: Toshihiro Aoyama (Sanfrecce Hiroshima), Yasuhito Endo (Gamba Osaka), Makoto Hasebe (Nuremberg), Keisuke Honda (Milan), Shinji Kagawa (Manchester United), Yoichiro Kakitani (Cerezo Osaka), Hiroshi Kiyotake (Nuremberg), Manabu Saito (Yokohama F Marinos), Hotaru Yamaguchi (Cerezo Osaka)

Washambuliaji: Shinji Okazaki (Mainz), Yoshito Okubo (Kawasaki Frontale), Yuya Osako (1860 Munich)

Zahoro Pazi hajui lolote Simba

WINGA machachari wa klabu ya Simba, Zahoro Pazi, amesema hana taarifa zozote za kuwa miongoni mwa wachezaji wanaotakiwa kuachwa ndani ya timu hiyo kwa msimu ujao.
Aidha mchezaji huyo ambaye ni mtoto wa mmoja wa makocha wa timu hiyo, Idd Pazi 'Father' amesema yeye bado ana mkataba na klabu hiyo na kama itakuwa kweli hatakiwi Msimbazi hana neno.
Akizungumza na MICHARAZO, Pazi alisema amekuwa akisoma na kusikia taarifa dhidi yake zikitolewa au kunukuliwa kutoka kwa kocha wake, Zdrakov Logarusic, lakini hajafahamishwa rasmi na viongozi.
"Sina taarifa yoyote rasmi ya kutaka kutemwa Simba, kwa vile nina mkataba na klabu yangu naendelea kujitambua kama mchezaji wa Simba nikiendelea kujipanga kwa msimu ujao," alisema.
Nyota huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar, Azam na JKT Ruvu alisema hata kama Simba itaamua kuuvunja mkataba wao, hatakuwa na neno zaidi ya kutuliza akili yake ili kujipanga upya kuendeleza kipaji chake.
Pazi aliyesajiliwa na Simba msimu ulioisha hivi karibuni alikuwa akipata wakati mgumu mbele ya Logarusic, japo katika mechi za lala salama za ligi hiyo alikuwa akipewa nafasi na kufunga mabao.
Hivi karibuni iliripotiwa kuwa Pazi na baadhi ya wachezaji zaidi ya 10 wapo kwenye mipango ya kutemwa ndani ya Simba kutokana na pendekezo la kocha Logarusic lililopo katika ripoti yake kwa viongozi.

Kikosi cha England hiki hapa, wapo Jack Wilshere, Cole atemwa

KOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson ametua kikosi cha wachezaji 23 atakaowatumia kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia akiwajumuisha nyota wawili wa Arsenal Jack Wilshere na Alex Oxlade-Chamberlain pamoja na kuwa majeruhi. 
Wilshere alirejea uwanjani katika mchezo wa mwisho dhidi ya Norwich jana baada ya kukaa nje toka Machi baada ya kuumia kifundi cha mguu wa kulia wakati akiwa katika majukumu ya kimataifa. 
Oxlade Chamberlain yeye alikosa nusu ya kwanza ya msimu kwa kuuguza goti na bado kuna hati hati Arsenal wakamkosa katika mchezo fainali ya Kombe la FA kutokana na majeraha kigimbi. 
Pamoja na hayo meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema Hodgson hapaswi kujali sana afya za wachezaji hao kwani bado kuna mwezi mmoja kabla ya Kombe la Dunia hivyo wana muda wa kutosha wa kupona kabisa. 
Kwa upande mwingine chipukizi kama Luke Shaw, Ross Barkley na Raheem Sterling wote wamepata nafasi ya kuwepo katika kikosi cha Hodgson.

Kikosi kamili cha Uingereza ni:
Makipa: Joe Hart (Manchester City), Fraser Forster (Celtic), Ben Foster (West Brom)

Mabeki: Glen Johnson (Liverpool), Phil Jones (Manchster United), Phil Jagielka (Everton), Gary Cahill (Chelsea), Chris Smalling (Manchester United), Luke Shaw (Southampton), Leighton Baines (Everton)

Viungo: Steven Gerrard (Liverpool), Frank Lampard (Chelsea), Jordan Henderson (Liverpool), Ross Barkley (Everton), Jack Wilshere (Arsenal), Alex Oxlade-Chamberlain (Arsenal), Raheem Sterling (Liverpool), Adam Lallana (Southampton), James Milner (Manchester City)

Washambuliaji: Daniel Sturridge (Liverpool), Wayne Rooney (Manchester United), Danny Welbeck (Manchester United), Rickie Lambert (Southampton)

Wachezaji za ziada :
John Ruddy (Norwich City), John Stones (Everton), Jon Flanagan (Liverpool), Tom Cleverley (Manchester United), Michael Carrick (Manchester United), Jermain Defoe (Toronto), Andy Carroll (West Ham)

Yanga yataka mzizi wa fitina kwa Mbuyu Twite wamsainisha upya

Mbuyu Twite akiwa na Bin Kleb (picha na maktaba)



Mlinzi kiraka wa timu ya Young Africans Mbuyu Junior Twite leo ameongeza mkataba mpya wa mwaka mmoja kuendelea kuitumikia klabu ya Yanga baada ya kufikia makubaliano na uongozi na kupata majibu ya Shirikisho la Soka nchini TFF juu ya idadi ya wachezaji wa kimataifa kwa msimu ujao 2014/2015.
Usajili wa Twite umefanyika leo makao makuu ya klabu ya Yanga chini ya Katibu Mkuu Bw Beno Njovu ambapo mchezaji amesema ataendelea kujitolea kwa uwezo wake kuisaidia timu yake ya Yanga.
Katibu Mkuu wa Young Africans Beno Njovu amesema wameingia mkataba wa mwaka mmoja na Twite baada ya pande zote kukubaliana, hivyo kuanzia sasa Twite ataendelea kuwa mchezaji wetu kwa msimu ujao wa 2014/2015 na kusisitiza kuwa usajili ndio umeanza sasa.
Akiongea mara baada ya kuweka sahihi kwenye mkataba wake mpya Twite amesema anajisikia furaha kuendelea kuwa mchezaji wa Yanga, kwani anafurahia maisha ya Jangwani, wapenzi, washabiki, viongozi na wachezaji ni marafiki/ndugu ndani na nje ya Uwanja.
Aidha Twite amesema Yanga ni miongoni mwa timu kubwa barani Afrika, zenye washabiki na waachama wengi hivyo wangu ni fahari kuendelea kuitumika timu hii ambayo tangu kujiunga nayo nimekua nikijtoa kwa moyo wangu wote kusaka mafanikio. 
Mbuyu Twite amekua ni mchezaji wa Young Africans kwa kipindi cha miaka miwili tangu Julai 2012 alposajiliwa huku katika kipindi hicho chote akiwa ni mchezaji wa kikosi cha kwanza ambapo msimu uliopita aliweza kuisadia timu yake kutwaa Ubingwa wa Lig Kuu ya Vodacom na msimu huu kushika nafasi ya pili.
YOUNG AFRICANS

Friday, May 9, 2014

HAWA NDIYO WAIGIZAJI WAREMBO ZAIDI BONGO MOVIE


Irene Uwoya
Kiwanda cha filamu Tanzania kimezalisha waigizaji wengi wenye majina makubwa sasa. ifatayo ni orodha ya waigizaji 10 wakike wenye mvuto na kuvutia zaidi kati ya wengi waliopo.

Filamu alizocheza
Question Mark, Apple ,Safari, Zawadi Yangu, Innocent Case, Nyota Yangu, Last Card, Doa la Ndoa, Ngumi ya Maria, Chupa Nyeusi, Kiapo, Eagle Eyes, Diversion of Love, Fair Decision, Pretty Girl, Damu Moja, Shakira, Yolanda, Tanzanite

Elizabeth Lulu Michael
Filamu alizocheza
Oxygen, Elizabeth Michael,House Boy, Ripple of Tears, Confusion,Ritazo, Family Disaster, Woman with Principal, Foolish Age nk

Wema Sepetu
Filamu alizocheza
House Boy, Crazy Tenant, Basilisa, The Diary, Lerato, Tafrani, White Maria, Sakata, Family Tears, Madame

Skyner Ally
Filamu alizocheza
What is It, Why I Did Love, I Hate My Birthday’, Kizungumkuti’, Unpredictable, Shahada

 
Yobnesh Yusuph aka Batuli
Filamu alizocheza
Kazi Yangu, Waves of Sorrow, Fungate,Get Out, The Glory of Ramadhan, My Fiance,Ripple of Tears, Machozi

Jacky Wolper
Filamu alizocheza
After Death, Impossible,My Princess,Tikisa, Mahaba Niue, Pain for Pain P.F.P, Think Before,

Identity Card, Babylon, Before Wedding,I am Not Your Brother,Curse of Marriage, Ulimi, Mr.Nobody, Pusi na Paku, Lupepo Village, Hukumu ya Mande, Mtekaji, Chocolate, End of Evil, The Diplomat, My Intention, Time After Time, Chaguo Langu, Siri ya Moyo Wangu, God is Great, Saa4, Swadakta, Gaitan, The Impact,Mens Day Out, Dunia Nyingine, Determination, Aching Heart, Shoga Yangu, Mafisadi wa Mapenzi,All About Love, Eagle Eyes, Wrong Decision, Mtegoni, Fake Love, Life 2 Life, Mtumwa, Secretary, Last Minutes, Jozani.

 
 Nargis Mohamed
Filamu alizocheza
Magic House, Yellow Banana, Woman with Principal nk


Irene Paul
Filamu alizocheza
Love & Power, Kibajaji, Kalunde, Fikra Zangu, Penzi la Giza, Love Me or Love Me Not, I Hate My Birthday, The Shell, Handsome wa Kijiji


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgwsHv5OD53NQrNgvCQl2mGbOg0fGdrFS9K1i994pRdbT5bVCWdcMaCc57PrTxHTpk9hSgCFOYToo6JzW9Lu1PcS2tIEzsZHz89cWPj71R0AuDmIGuDk3nf_4ua9a0TIwjc08EBqrTgqbQ/s1600/P1010017.JPG               Shamsa Ford
Filamu alizocheza
Zawadi Yangu, Babylon, Get Out, Dont Try, I Think I hate My Wife, Loreen, Zawadi ya Birthday, Red Mzula, Mafisadi wa Mapenzi, Crazy Love, Saturday Morning



Salma Jabu aka Nisha
Movie alizocheza
Tikisa, Subiri Mama, Matilda, I am Lost, Pusi na Paku, Mchana wa Kiza,Kashfa Macho Yangu,Red Cross
 http://api.ning.com/files/xLH1QA7JYqCMGrVhlG4X5OjJKgpgXl04KJV1Rwlg38jbHQjHvCNi5OaaFW2tVeu2fRyYekZwet8tmh3e5T3GCo7z60VDBbje/AuntEzekiel2.jpg
                               Aunt Ezekiel
Filamu alizocheza
Pumba, Jungu la Urithi, Eyes on Me, Radio Presenter,Machozi Yangu, The Beauty Fools, Kijogoo,Siku za Maajabu, Best Losers, Alice & Janel, I Hate My Birthday, Lost Souls,Mens Day Out, Shoga Yangu, Lonely Heart, The Mask, Green Light, Sound of Death,Black Sunday,Taste of Love, Endless Love, Same Girl, The Village Pastor, Wicked Love, The Cold Wind

http://www.eatv.tv/media/picture/large/shilole.jpg Shilole
Filamu alizocheza
Chungu ya Nafsi, Barmaid, Macho Yangu, Kisasi cha Jessica, Mafisadi wa Mapenzi, Talaka Yangu


http://www.bongocelebrity.com/wp-content/uploads/2013/07/tatu.jpg                         Kajala Masanja
Filamu alizocheza
House Girl & Boy, Dhuluma, Shortcut, Basilisa, Devil Kingdom nk


http://api.ning.com/files/4jXfPWfoQHT2w6JX*yjkRMYviPQtx53F88QBQi7wErChIiWht9NQ86Za3dBhRKar08hNqT4OmMT0ZUkGGRZDHRlfuiMolUt4/RoseNdauka2.jpg Rose Ndauka
Filamu alizocheza
Waiting Soul, One Night, Fall in Love, Waves of Sorrow,Malaika,The Same Script, The Specialist, Real Promise, Swahiba,Kwa Heshima Ya Penzi, Love Me or Love Me Not,Jessica,Because of You, Ruben and Angel, The Diary, Solemba,Bad Girl, Cut Off, Sound of Death, Why Did I Love, Mahabuba

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXNOtf3uwUqr1vdmB-od-pIOAWQeVgpgxeWb8ldJx2POgrOYstvrIVNvR5-CfHFochNQelG9GjeUClNd4_-rF0d1XMlNwJ_QZplKKVjIOE-bmmRmjSa2LVvUjXNRP1mYfY4KSehN1l7Tvq/s1600/warda4.jpg

Warda Walid
Filamu alizocheza
Triple L, Nipende Monalisa, The Lost Adam



Monalisa