STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 4, 2014

Coastal Union yazidi kuzoa nyota wapya

 

Aliyekuwa beki wa kulia wa timu ya Rhino Rangers ya Tabora, Amani Juma kulia akisaini mkataba wa kipindi cha miaka miwili kuitumika timu hiyo katika msimu mpya wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kushoto ni katibu
Mkuu wa Coastal Union Kassim El Siagi.???????????????????????????????Aliyekuwa beki wa kati wa timu ya Mgambo Shooting ya Tanga,Bakari Mtama akisaini mkataba wa kuijunga na timu ya Coastal Union ya Tanga jana wanaoshuhudia katikati ni Makamu Mwenyekiti wa Coastal Union, Steven Mguto wa kwanza kulia ni Katibu wa Coastal Union,Kassim El Siagi na wa pili kushoto ni mjumbe wa kamati ya usajili wa klabu hiyo, Salim Amiri.
???????????????????????????????Mshambuliaji Mpya wa timu ya Coastal Union,Husein Sued akisaini mkataba wa mwaka mmoja wa kujiunga na timu hiyo yenye makazi yake barabara ya kumi na moja jijini wanashuhudia katikati ni Katibu wa Coastal Union,Kassim El Siagi na wa kwanza kulia ni Meneja wa timu hiyo, Akida Machai.

NA OSCAR ASSENGA,TANGA.
BEKI wa Kulia wa timu ya Coastal Union,Amani Juma amesema atahakikisha
anashirikiana na wenzake ili kuweza kuipa mafanikio timu hiyo katika
michuano ya Ligi kuu Tanzania bara lengo likiwa kuiwezesha kuchukua
kombe hilo na kuweza kushiriki mashindano makubwa.

Juma ambaye alisajiliwa na Coastal Union kwa mkataba wa miaka miwili
alisema ni wajibu wake kujituma na kupambana vilivyo kuiwezesha timuhiyo kufikia malengo yao waliojiwekea msimu ujao ya kumaliza ligi hiyo
 wakiwa mabingwa.
Alisema katika kutimiza suala hilo wachezaji waliosajiliwa na timu hiyo hawana budi kushikamana na kuwa kitu kimoja kwa kuhakikisha wanafanya vizuri kwenye mechi zao za nyumbani na ugenini wakati ligi
 hiyo itakapoanza.

Aidha aliwashukuru viongozi wa klabu hiyo kwa kuthamini mchango wake
kwa kumpa ridhaa ya kuichezea timu hiyo katika kipindi hicho na kuahidi kupambana kufa na kupona kwa ajili ya kufikia mafanikio
 yatokanayo na soka hilo.

Katika hatua nyingine wachezaji wote waliosajiliwa na timu hiyo
 wanatakiwa kuwasili mkoani Tanga Kesho(leo) kwa ajili ya kuanza
 maandalizi ya kuelekea msimu mpya bila kukosa kwani watakaochelewa kuwasili watachukuliwa hatua za kinidhamu.

Barcelona wamruhusu Xavi kuhama

KLABU ya Barcelona kupitia Rais wake, Josep Maria Bartomeu imesema ipo tayari kumsaidia Xavi Hernandez kuondoka kama atataka kuihama klabu hiyo.
Nyota huyo wa timu ya taifa ya Hispania amekuwa gwiji tangu alipoanza kuichezea klabu hiyo mwaka 1998, lakini veterani huyo mwenye umri wa miaka 34 alijikuta akikosa nafasi ya kutosha katika kikosi cha kwanza chini ya kocha Gerardo Martino msimu uliopita.
Aliachwa pia nje ya kikosi cha kwanza kilichocheza mechi ya kuamua bingwa wa La Liga dhidi ya Atletico Madrid, ambayo kama Wacatalunya hao wangeshinda wangetwaa ubingwa.
Tangu wakati huo amehusishwa na klabu kadhaa, ikiwamo ya Al-Arabi ya Qatar, na bosi huyo wa Barca amemfungulia milango ya kuondoka Camp Nou.
"Amedumu katika kikosi cha kwanza kwa miaka mingi na anayo haki ya kuamua (kubaki ama kuondoka). Tutaheshimu maamuzi yake," Bartomeu alisema.
"Siku atakayoondoka, ataacha historia kama mchezaji bora kuliko wote waliopitia (Barcelona). Kama anataka kubaki nasi, tutafurahi, kama anataka kuondoka tutamsaiddia.
"Xavi atarejea hapa kwasababu atakuwa kucha mkubwa," aliongeza.
Barca ilimtambulisha kiungo mpya Ivan Rakitic Jumanne waliyemsajili kwa euro milioni 20 kutoka Sevilla.

Algeria waoinyesha mfano wa kuigwa

KATIKA mafundisho ya Qur'an na Hadithi za Mtume Muhammad (SAW) inasema Muislam ndugu na Uhurumiana wenyewe kwa wenyewe.
Hiyo imethibitishwa na timu iliyoonyesha soka la kusisimua nchini Brazil, Algeria iliyong'oka kishujaa mbele ya Ujerumani.
Mshambuliaji nyota wa timu ya taifa ya Algeria Islam Slimani aliyepo kwenye orodha ya wafungaji bora akiwa na mabao mawili amebainisha kuwa kikosi kizima cha nchi hiyo kinatarajiwa kutoa msaada wa posho zao kwa watu wa Gaza. 
Timu ilirejea nyumbani wakiwa mashujaa na wachezaji wameamua kutoa posho zao kwa wale ambao wanazihitaji zaidi, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa miongoni mwa Ibada ndani ya Uislam.
Hatua hiyo ya Algeria imekuja huku wawakilishi wengine wa Afrika katika michuano hiyo kama Ghana, Nigeria na Cameroon kukumbwa na msuguano katika kambi zao kutokana na posho hatua iliyochangia kwa kiasi kikubwa kuenguliwa mapema.
Algeria ni nchi ya Kiislam iliyopo Kaskazini mwa Afrika na inaelezwa kufungwa kwa mabao 2-1 katika hatua ya lala salama na Ujerumani ilitokana na swaumu.

Ujerumani, Ufaransa hapatoshi leo Brazil

* Wenyeji Brazil na Colombia kumaliza udhia

* Neymar shakani, akiwaonya majirani zao

Wenyeji Brazil

Wakali wa Colombia
UTAMU wa Fainali za Kombe la Dunia zinazoendelea nchini Brazil unatarajiwa kuanza kunoga leo wakati michezo ya Robo Fainali itakapochezwa kwa timu wenyeji Brazil kuvaana na majirani zao Colombia, huku mabingwa wa zamani Ujerumani na Ufaransa wakikumbushia nusu fainali ya mwaka 1982 nchini Hispania.
Ujerumani walionyakua taji hilo la Dunia mara tatu itawavaa mabingwa hao wa mwaka 1998 katika mechi ya kwanza ya hatua hiyo kwenye uwanja wa Maracana, kuanzia saa 1 usiku kwa saa za Afrika Mashariki huku kila timu ikitambia nyota wake na kuwa na kiu ya kusonga mbele katika nusu fainali.
Ni mechi ambayo haraka inaleta kumbukumbu ya mwaka za mechi ya nusu fainali ya Kombe la Dunia baina ya timu hizo mwaka 1982, pale Ujerumani iliposhinda kwa "matuta" baada ya sare ya 3-3  inayokumbukwa kwa rafu mbaya ya Harold Schumacher dhidi ya mshambuliaji wa Ufaransa, Patrick Battiston.
Ujerumani watakuwa wakicheza robo fainali yao ya tisa mfululizo ya Kombe la Dunia, lakini kikosi cha Joachim Low kimeshindwa kuonyesha ubora nchini Brazil tangu kiliposhinda 4-0 dhidi ya Ureno katika mechi ya ufunguzi.
Katika mechi yao iliyopita, walishinda kwa shida 2-1 dhidi ya Algeria katika muda wa nyongeza na kuzua mijadala mizito nyumbani kwao kuhusu kiwango cha timu hiyo, mbinu na staili ya uchezaji.
Moja ya mijadala ni kwa kocha Low anapojadili kikosi chake kwamba amchezeshe Philipp Lahm kama kingo ama beki wa kulia. Mijadala mingine ni kiwango cha chini cha wachezaji kama Mesut Ozil na Mario Gotze.
Wajerumani watapata nguvu kwa kurejea kikosini kwa beki Mats Hummels baada ya kuikosa mechi dhidi ya Algeria kutokana na kuwa mgonjwa kambini, lakini Shkodran Mustafi ameaga mashindano hayo kutokana na maumivu ya misuli ya nyuma ya paja.
Katika ushambuliaji, Andre Schurrle anatarajiwa kuanza baada ya kufunga goli akitokea benchini dhidi ya Algeria, wakati Thomas Muller ataongoza mashambulizi, jambo linalomaanisha kwamba Miroslav Klose atalazimika kuanzia benchi kama atahitaji kuvunja rekodi ya dunia ya kufunga magoli mengi zaidi.
Wakati Ujerumani wanaonekana kuwa na uchovu baada ya ratiba ngumu kaskazini, Ufaransa wanakuja kwenye mechi wakiwa na nguvu zaidibaada ya kuifunga Nigeria 2-0 katika raundi iliyopita.
Ufaransa hawakuwa katika kiwango cha kutisha katika hatua ya 16-Bora lakini wamecheza soka zuri mara moja moja katika michuano hiyo, huku kocha Didier Deschamps akiwatumia washambuliaji wake kiwerevu.
Uwanja ni wake Paul Pogba kuonyesha kwanini anatajwa kama mmoja wa viungo bora zaidi duniani akiwa na umri wa miaka 21 tu. Nyota huyo wa Juventus amekuwa na kiwango kinachopanda na kushuka katika fainali zake hizi za kwanza za Kombe la Dunia lakini tayari ameonyesha ishara za uwezo wake wa kuwa mchezaji mshindi kwa kufunga goli la kwanza dhidi ya Nigeria.
Bila shaka mechi hiyoya mapema itakuwa ni 'tamu' kuliko inavyotarajiwa kutokana na kuwepo kwa mchuano wa kimya kimya wa ufungaji baina ya Karim Benzema wa Ufaransa dhidi ya Thomas Muiller ambao wanatofautiana kwa bao moja, Muiller akiwa na manne sawa na Neymar na Messi, huku Benzema akiwa na matatu akilingana na Arjen Robben, Robin van Persie wa Uholanzi, Enner Valencia wa Ecuador na Xherdan Shaqiri wa Uswisi.
Katika mechi itakayopigwa baadaye saa tano usiku, wenyeji Brazil ambayo awali kulikuwa na hofu ya kukosa huduma za nyota wao Neymar aliyekuwa akisumbuliwa na maumivu ya misuli, itashuka dimbani kuwakabili Colombia waliopo kwenye kiwango cha hali juu katika fainali hizo.
Colombia iliyoshinda mechi zake zote za makundi kwa asilimia 100 na kuing'oa Uruguay kwa mabao 2-0 katika muda wa kawaida, itawakabili wenyeji wakiwa wanafahamu wapo nyumbani na wakipewa sapoti na maelfu ya mashabiki vichaa wa soka wa taifa hilo lenye watu wanaokadiriwa Miliioni 200.
Wakimtegemea nyota wao mpya anayeongoza kwenye safu ya Ufungaji Bora wa Fainali hizo za Brazil, James Rodriguez, Colombia bila shaka itakuwa na kiu kubwa ya kutinga hatua hiyo ya Nusu fainali ili kuzidi kuboresha reklodi yao baada ya kipindi cha muda mrefu. Kwani haikuwahi kutinga hatua ya Riobo Fainali waliyopo sasa wala kunusa Nusu Fainali tangu ianze kushiriki michuano hiyo.
Hatua kubwa kwake ni kutinga 16 Bora katika fainali za mwaka 1990 zilipofanyika nchini Italia, na mara zote ilikuwa ikikwamia katika hatua ya makundi na kwa kasi waliyoonyesha msimu huu ni wazi Brazil inapaswa kujichunga la sivyo watashuhudia wakibaki kuwashangilia wageni na wao kuwa watazamaji.
Rodriguez aliyefunga mabao matano na kufunika kabisa pengo lililokuwa likitarajiwa kuiathiri nchini baada ya Radamel Falcao kuumia na kuondolewa kikosini, anatazamwa kama tumaini ya Colombia kuweka historia kubwa zaidi kwa nchi hiyo ambayo pia ina wakali kadha wanaotamba duniani kama Jackson Martinez, Adrian Ramos na kipa mkongwe aliyeweka rekodi mpya ya kuwa mchezaji mzee kucheza Fainali za Kombe la Dunia akimpiku Mcameroon, Roger Milla. Faryd Mondragon mwenye miaka 43.
Hata hivyo Brazil siyo rahisi kwao kukubali kufanywa daraja na majirani zao hao katika mchezo huo na nyota wake Neymar amenukuliwa kujiandaa kumfunika Rodriguez na Colombia kwa ujumla.
Neymar alisema Brazil imedhamiria kutinga nusu fainali ya Kombe la Dunia kwa ushindi dhidi ya Colombia mjini Fortaleza, licha ya kumsifu  James kwa kiwango chake katika michuano hiyo akimtaja kama 'Mchezaji Mkubwa', ila akisistiza kuwa yeye na wachezaji wenzake watahitimisha safari nzuri ya wapinzani wao hao katika michuano hiyo leo.
"Colombia ni timu nzuri, wamekuwa wakishinda sana, wameonyesha wana nguvu wakati wa mechi zao. James ni bonge lamchezaji: yeye ni nyota, ingawa ni mdogo sana, miaka 22 kama mimi. Amekuwa akionyesha namna alivyo mchezaji mkubwa na tunapaswa kumpongeza kwa kila anachokifanya.
"Lakini natumai safari yake katika Kombe la Dunia hili imefikia tamati sasa na Brazil iendelee – kwa heshima yote, hakika."
Mbali na Neymar, Brazil pia inatambia nyota kama Fred, Davud Luis, Oscar, na kipa aliyegeuzwa 'Mungu' kwa sasa akiabudiwa kwa kuivusha timu yao hatua hiyi kwa kudaka penati mbili za Chile, Julio Cesar.
Je ni Ujerumani au Ufaransa zitakazotangulia Nusu fainali ma vipi wenyeji Brazil watatibua rekodi ya Colombia ya kushinda mechi kwa asilimia 100? Tusubiri kuona hiyo usiku.