STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 6, 2014

Ubaguzi! Mchezaji afungiwa kwa kubaguliwa Urusi

Kanga (kushoto) aliyefungiwa Russia kwa kutoa ishara za matusi baada ya kubaguliwa na mashabiki wa Spartak Moscow
KIUNGO wa kimataifa wa Gabon, Guelor Kanga amefungiwa mechi tatu na Shirikisho la Soka la Urusi, RFU baada ya kuonyeaha ishara ya matusi akikerwa na ubaguzi aliofanyiwa na mashabiki wa Spartak Moscow.
Kanga alionyesha ishara hiyo baada ya kuonyesha ishara ya matusi kwa mashabiki wa Spartak Moscow ambao walimfanyia vitendo vya ubaguzi wa rangi. 
Kiungo huyo wa klabu ya FC Rostov mwenye umri wa miaka 24 alikuwa akipigiwa kelele za nyani na mashabiki wa Spartak wakati wa mchezo wa Ligi Kuu nchini humo uliofanyika jijini Moscow.
Katika kujibu mapigo ya kejeli hizo nyota huyo alitoa ishara hizo hatua ambayo RFU ilibidi kuchukua hatua kwa kumtoza pia na faini ya paundi 600. 
Spartak nao walitozwa faini ya paundi 830 kutokana na mashabiki wao kuonyesha vitendo vya kibaguzi. 
Septemba mwaka huu beki wa Dynamo Moscow Christopher Samba alifungiwa mechi mbili kwa kufanya tukio kama hilo wakati mashabiki wa timu ya Torpedo Moscow walivyomfanyia vitendo vya kibaguzi.
KIUNGO wa kimataifa wa Gabon, Guelor Kanga amefungiwa mechi tatu na Shirikisho la Soka la Urusi-RFU kwa kuonyesha ishara ya matusi kwa mashabiki wa Spartak Moscow ambao walimfanyia vitendo vya ubaguzi wa rangi. Kiungo huyo wa klabu ya FC Rostov mwenye umri wa miaka 24 alikuwa akipigiwa kelele za nyani na mashabiki wa Spartak wakati wa mchezo wa Ligi Kuu nchini humo uliofanyika jijini Moscow jana. Nyota huyo naye alijibu mapigo hatua ambayo RFU ilibidi kuchukua hatua kwa kumtoza pia na faini ya paundi 600. Spartak nao walitozwa faini ya paundi 830 kutokana na mashabiki wao kuonyesha vitendo vya kibaguzi. Septemba mwaka huu beki wa Dynamo Moscow Christopher Samba alifungiwa mechi mbili kwa kufanya tukio kama hilo wakati mashabiki wa timu ya Torpedo Moscow walivyomfanyia vitendo vya kibaguzi.

Make Money

Arsenal yafa ugenini, Spurs, Liverpool zang'ang'aniwa

Stoke's Peter Crouch recreates the 'Cristiano Ronaldo' celebration for his goal
Crouch akishingalia bao lake la mapema dhidi ya Arsenal
Ryan Mason and Marouane Chamakh
Vita ya Spurs na Crystal ilikuwa hivi
Steven Gerrard
Nahodha Steven Gerrard akiipigiania LIverpool akitokea benchi bila ya mafanikio
Charlie Austin
QPR ilipotakata nyumbani
SAA chache baada ya vinara wa Ligi Kuu ya England Chelsea kunyukwa ugenini ikiwa ni kwa mara ya kwanza, Arsenal nayo imekumbana na aibu kama hiyo ugenini baada ya kulala mabao 3-2 kwa Stoke City.
Dalili mbaya kwa Arsenal zilianza mapema baada ya kufungwa bao la kushtukiza dakika moja tu tangu kuanza kwa pambano hilo wakati Peter Crouch alipoiandikia Stoke bao la kuongoza akimaliza kazi ya Mamme Diouf.
Dakika ya 35 Bojan aliiongezea wenyeji bao kabla ya kumegewa pande na Jonathan Walters, ambaye alifunga bao jingine la Stoke lililokuwa la tatu sekundu chache kabla ya mapumziko.
Vijana wa Arsene Wenger walirejea kwa kasi katika kipindi cha pili kwa kuanza kurejesha mabao hayo, baada ya Santi Cazorla kuandika bao dakika ya 68 kwa penati kabla ya Aaron Ramsey kuongeza dakika mbili baadaye akimalizia kazi ya Alexis Sanchez.
Arsenal ilijikuta ikimpoteza beki wake Calum Chembers baada ya kuonyesha kadi ya pili ya manjano iliyoambatana na nyekundu.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Liverpool ikiwa nyumbani iling'ang'aniwa na Sunderland na kutoka suluhu sawa na ilivyokuwa kwa Tottenham Hotspur iliyoshikiliwa na Crystal Palace na Hull City kushindwa kutoshana nguvu na Wes Bromwich Albion kwa kutoka pia suluhu huku QPR ikipata ushindi wake wa pili kati ya mechi zake tatu za karibuni.
Kwa hivi sasa mabaingwa watetezi Manchester City wapo dimbani kuumana na Everton katika pambano linalochezwa uwanja wa Etihad.
Jumatatu kutakuwa na pambano moja la kukata na shoka kati ya Southampton itakayoialika Manchester United ambayo inasaka kuingia kwenye Tatu Bora.

Yanga yaidonyoa Express, Maximo amficha Emerson

Emerson (wa pili kulia) akiwa na Hussen Javu, Kiiza na Coutinho
IKICHEZA bila kiungo mkabaji mpya toka Brazil, Yanga imetuma salamu kwa watani zao Simba baada ya kuifunga Express ya Uganda kwa bao 1-0 katika pambano la kirafiki la kimataifa lililochezwa uwanja wa Taifa.
Bao pekee lililoizamisha Express ambao jana walilazimishwa suluhu na Simba katika pambano jingine la kirafiki la kimataifa liliwekwa kimiani na Mganda, Hamis Kiiza 'Diego' katika dakika za lala salama na kuzima ndoto za Waganda wenzake kuambulia suluhu katika mchezo huo.
Kiiza aliyeingia uwanjani toka benchi alifunga bao hilo kwa shuti baada ya kuunganisha krosi ya Simon Msuvah, na mashabiki waliofurika uwanjani walikosa uhondo kwa kushindwa kumuona Emerson Oliveira ambaye kocha Marcio Maximo aliamua kutompanga kabisa ili kuficha makali yake kabla ya kuvaana na Simba Jumamosi ijayo kwenye mechi ya Bonanza ya Nani Mtani Jembe.

Newcastle United yaiadabisha Chelsea, Cisse shujaa

Newcastle striker Papiss Cisse puts his side in front against Chelsea
Cisse akimtungua kipa wa Chelsea
Papiss Cisse scores for Newcastle against Chelsea
Cisse alikuwa na kazi ya kufunga tu St James Park
MABAO mawili ya mtokea benchi, Demba Cisse yameiwezesha Newcastle United kusitisha rekodi ya ushindi mfululizo wa Vinara wa Ligi Kuu ya England Chelsea baada ya timu hiyo kucharazwa mabao 2-1.
Cisse aliyeingizwa dimbani kipindi cha pili alidhihirisha umuhimu wake katika timu hiyo baada ya kufunga mabao hayo akiunganisha korsi pasi za Mousa Sissoko katika dakika za 57 na 78  kabla ya Didier Drogba kuipatia Chelsea bao kwa kichwa akiunganisha mpira wa adhabu dakika ya 83.
Adabu hiyo ilitokana na Steven Taylor kucheza rafu iliyofanya aonyeshwe kadi ya pili ya njano na kuunganishiwa nyekundu dakika ya 81, hata hivyo pamoja na Chelsea kucharuka matokeo yalisalia kuwa 2-1.
Kipigo hicho ni cha kwanza kwa Chelsea kwa msimu huu na kuendeleza unyonge wake kwa Newcastle kwa mechi ya tatu mfululizo kila wanapoifuata nyumbani kwao St James Park.
Kabla ya klipigo hicho Chelsea ilikuwa imcheza mechi 23 bila kupoteza na 14 zikiwa za ligi na kukatisha ndoto za mashabiki wa klabu hiyo wakiifikia rekodi ya Arsenal iliyocheza mechi 49 katika msimu wa 2003-2005.