STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 14, 2014

HATARI! Watu 6 wafa kwa kuchinjwa kama Kuku Bukoba

Kanisani alipouawa mwalimu Ng"wandu
KWA kipindi cha miezi miwili tu, kuanzia Octoba 9 hadi Desemba 4 mwaka huu, ambapo jumla ya vijana  6 wameuawa katika mazingira ya kutatanisha,  watatu wamechinjwa katika kata ya Kitendaguro, 1 katika kata ya Rwamishenye, huku wawili wakichinjwa katika kata ya Kibeta ndani ya manispaa, huku wananchi wakishangaa ukimya wa mamlaka bila kuchukua hatua.

Tarehe 09 Oktoba, aliyeuawa mwalimu DIONIZ NGW’ANDU wa shule ya sekondari Kagemu, alipokuwa katika kanisa la PAGT, baada ya kukatwa kichwa na kitu chenye ncha kali, huku jamaa yake aliyekuwa mlinzi katika kanisa hilo siku hiyo akijulikana kwa jina mojala THEMISTOCRES akisalia na ulemavu wa maisha, kama alivyoeleza  mchungaji wa kanisa hilo FAUSTINE JOSEPH. 

Siku kati ya 5 au saba badaye, mwili wa kijana ambaye hakutambuliwa majina wala sura, ulikutwa umeharibiwa kwa kunyofolewa macho, huku ukitupwa kando mwa shamba la mmoja wa wakazi wa Kitendaguro, ambapo Anakret Laurent Kyaishozi miaka 30 alikuwa shuuda, aliueleza mtandao huu kuwa mwilihuoulichukuliwa na polisi mpaka sasa hawajajua ninikiliendelea.

Kando na hayo, familia ya kijana aliyekuwa na umri wa miaka 37 Erick Kashaga akiacha mjane Sofia Mozes miaka 32 na watoto saba, imesalia katika mvutano mkubwa,na familia ya bwana Levocatus , ambaye mpaka sasa yuko mikononi mwa jeshi la polisi, huku jamaa zake wakielezwa kuwa uchunguzi unaendelea.
Kaburi la Mozes Kashaga
 Levocatusi ni kijana  mwenye umri wa miaka 33 huku akiwa na watoto watatu wawili wakizaliwa na mke wake wa Katoma walieachana, na mmoja akizaliwa na mke anayeishi naye Kitendaguro, Bi Ajat au Betrida mwenye umri wa miaka 32, alikamatwa baada ya kutajwa kuwa alitambuliwa na kijana aliyekuwa na marehemu wakatiwa tukio .
Mzee Rumumba akionesha eneo alipochinjwa Mozes
Mzee SILIDION RUMUMBA mwenye umri wa miaka 73,  ndiye mmiliki wa kilabu cha pombe, ambacho dakika za mwisho marehemu aliondoka hapo muda wa saa tano usiku, akiwa na jamaa zake wawili.

Ndani ya dk kama mbili baadaye, liyetajwa kwa jina moja tu la Eriki alirudi nyumbani kwa mzee SILIDION RUMUMBA akiwaeleza kuwa wamevamiwa na mtu ambaye alimtaja jina, huku akisema kuwa hana hakika kama watamkuta hai Kashaga, ilhali akitoa taarifa hizo kimyakimya, pasi na kupiga kelele wakati wa tukio,jambo ambalo linawashangaza wengi, kwasababu marehemu ameuawa karibu kabisa na makaazi ya watu.
Mama mzazi wa Mozes
Kando na maelezo hayo, nimetaka kusikiliza ushuuda wa Erick aliyethibitisha kuwa alishuudia mauaji hayo, lakini nyumbani kwaojamaa zakewalisema kuwa huwezi kumwona sababau wamemficha sehemu baada ya kutishiwa na mkewa mtuhumiwa.

Hayo yamesalia katika familia hizo ndani ya kata ya Kitendaguro, huku katika kata ya kibeta, lawama kubwa zikiangushwa kwa mamlaka, kuwa hawajaonesha juhudi zozote  baada ya kuuawa kijana GOODRUCK FRANCIS aliyekuwa na umri wa miaka 38, ambapo  taarifa za awali zinaonesha kuwa aliuawa kwa kukatwa shingo na watu wasiojulikana, ikiwa ni kando kando mwa barabara ya mtaa wa Kibeta Amjuju.
Bi Stella Lenatus amesema amekata tama kwasababu tangu ahojiwe, ameenda kituoni kujua taarifa za mdodgo wake na kuambiwa asubiri walikuwa bize na kazi nyingine muhimu.
Hapo kustoto pichani ndipo aliuawa Gudrack eneo la Kibeta Anyama.
Sambamba na wanaouawa pasipo kutambulika majina na makwao ndani ya manispaa ya Bukoba, Ernest Kato ni kijana aliyeuawa mwezi novemba akiwa na miaka32,katika mtaa wa Bugezi kata Rwamishenye, majira ya usiku, na kutambulika asubuhi ya tarehe iliofuata kwa kukutwa amechinjwa, huku akiacha mjane na mtoto mmoja, ambaye hatahivyo  amekimbia kwa kuhofia naye kuawa.

Mmoja kati ya wanafamilia wa marehemu Ernest, ameomba jina lake lihifadhiwe, pamoja na kusema kuwa wanaishi kwa hofu kubwa kiasi cha kujipangia muda wa kurudi nyumbani mapema nyakati za usiku, na shughuli zimesimama.

Mauaji ya  mwisho hadi ninakamilisha makala haya, ni alivyouawa Joran Rutulaniisa, mkaazi wa Kibeta magoti, nilifika eneo la tukio muda mfupi tu baada ya polisi kuubeba mwili wake lakini taarifa za ndugu ambao hatahivyo wanahofu ya maisha yao, ni kuwa nduguyao  ameuawa kwa aina ile ile ya vifo vya kukatwa koromeo.
Marehemu Rutu enzi za uhai wake
Tetesi ambazo bado sijazithibisha, wananchi wanaofanya biashara ya senene, wamelazimika kuanza kujifunga vitu vigumu na tauro shingoni, kama taadhali watakapovamiwa.
Shangazi na mama mdogo wa marehemu kwenye kaburi la Rutu

Baba wa marehemu Rutulanisa
Mauaji nikitendo kisichokubalika kwa mwenyezi Mungu, jambo linalompa shekh mkuu wa mkoa wa Kagera Aruna Kichwabuta,kukemea hali hiyo katika mamlaka na wananchi.
Shekh mkuu wa mkoa, Haruna KICHWABUTA
Makala maalumu sehemu ya kwanza kuhusu mauaji hayo inaruka marudio leo saa moja jioni kupitia 88.5 Kasibante fm Bukoba.

 
Na Mwanaharakati

Hivi ndivyo Simba ilivyoinyoa Yanga mabao 2-0 Nani Mtani Jembe

 Kocha wa Simba, Patrick Phiri akisalimiana na kocha wa Yanga, Marcio Maximo kabla ya mchezo.
Katika pambano hilo lililokuwa kali na la kusisimua, Simba ilipata mabao yake katika kipindi cha kwanza kupitia Awadh Juma 'Maniche' na Elias 'Magoli' Maguli na kuifanya Yanga inyong'onyee kwa mwaka wa pili mbele ya Mnyama baada ya mwaka jana kucharazwa mabao 3-1 katika mchezo kama huo.
 (Picha zote: Francis Dande)
 Emmanuel Okwi akiomba dua wakati akiingia uwanjani.
 Mgeni rasmi Mh waziri wa michezo Dr Fenella Mukangala akisalimiana na wachezaji wa Yanga.
 Mgeni rasmi akisalimiana na wachezaji waSimba.
Kikosi cha Yanga.
Kikosi cha Simba.
Kocha wa Yanga akitafakari.
Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi akiwa amenyanyua juu
Kombe la Ubingwa wa mechi ya Nani Mtani Jembe msimu wa pili uliofanyika leo kwenye
Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Simba imeshinda 2-0. 
 Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Mchezo, Dk. Fenella Mukangala akimkabidhi nahodha wa Simba, Emmanuel Okwi Kombe la Ubingwa wa mechi ya Nani Mtani Jembe.
Wachezaji wa Simba wakishangilia ushindi wa timu yao.
 Umati wa mashabiki wa Yanga.
 Umati wa mashabiki wa Simba.
Mashabiki wa Simba wakiwa wamebeba mfano wa jeneza kuwakejeli watani zao.
 Beki wa Yanga, Nadir Haroub ‘Canavaro’
 Beki wa Yanga, Kelvin Yondan akimiliki mpira.
 Mwamuzi wa mchezi akimuonyesha kadi ya njano mshambuliaji wa Simba, Simo Serunkuma.
 Kpah Sherman akiokoa moja ya hatari langoni mwake huku Elius Maguri akimzonga.
 Mshambuliaji wa Simba Elius Maguri akichuana na beki wa Yanga, Nadir Haroub.
Wachezaji wa Simba wakishangilia bao lao la kwanza.
 Hassan Isihaka (kushoto) ana Ramadhani Singano ‘messi’ wakishangilia bao la kwanza la timu yao.
Beki wa Yanga, Oscar Joshua akimtoka Elius Maguri wa Simba.
Shabiki wa Yanga akipata msaada baada ya kuzimia jukwaani.
 Mashabiki wa Simba wakiwa na bango lenye idadi ya mabao waliyowahi kufungwa Yanga.
Leo ni 2-0…..
Burudani zikitolewa uwanjani.
 Mashabiki wakitolewa uwanjani baada ya kuzimia.
 Hali ilikuwa ngumu kwa mashabiki mpaka baadhi yao kuzimia.
Huduma ya kwanza kwa waliozimia ikitolewa.
 Beki wa Yanga, Kpah Sherman akichuana na beki wa Simba, Hassan Isihaka.
 Danny Mrwanda akiwa ameshika kichwa baada ya kukosa bao la wazi.
Ivo Mapunda akiokoa moja ya hatari langoni mwake.
 Simon Msuva akichuana na Issa Rashid.
Ivo Mapunda (katikati) akishangilia ushindi na wenzake.
Wachezaji wa Yanga wakiwa na huzuni baada ya kumalizika kwa mchezo.
Yanga wakiwa vichwa chini.
 Medali za washindi.

SHIME WATANZANIA TUKAPIGE KURA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6cywA_Xx-3NwoCS58CUsRmxx95Iy-9b2GXMUVGHbJTT8eltyJa55rwXPY-7khzoVNOhblSZSKnd1zwe6zsafqFkTqyJ4KuY7oHLCWlOyzO9MSnfWuJe_YKES3SHnSQYpyhd4sR_yzudg/s1600/IMG_0257.JPG
Shime watanzania changamkieni uchaguzi kama hivi, msije mkajilaumu baadaye weatakapochaguliwa viongozi wasiofaa katika eneo lako.
LEO Desemba 14 ni Siku ya Kupiga Kura kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa, Vitongoji, Tarafa na Vijiji.
Shime watanzania hii ni siku muhimu na ambayo yeyote hapaswi kuipoteza.
Hivyo yeyote ambaye amejiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika maeneo yao ni wajibu wao kutumia haki yao kwa kwenda kupiga kura kuchagua viongozi wanaowataka kutokana na wasifu wao.
Kitu cha muhimu mzingatie sifa na uwezo wa mtu badala ya kuangalia chama, jinsia, imani ya kidini, kabila au jambo lolote lisilo la tija kwa maendeleo ya eneo husika.
Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa tangu kuanzia saa 2 asubuhi mpaka jioni, hivyo yeyote anayetambua wajibu wake kwa maendeleo ya eneo lake na Taifa kwa ujumla aitumie nafasi hiyo adhimu kwa kwenda KUPIGA KURA kuchagua VIONGOZI wanaofaa.
MICHARAZO inawatakia kila la HERI katika zoezi hilo na MUNGU awaongoze kuwachagua WANAOSTAHILI.

FIFA kuipigia kura Ripoti ya Uchunguzi wa Rushwa

http://resources3.news.com.au/images/2010/12/09/1225968/118755-sepp-blatter-fifa_.jpgSHIRIKISHO la Soka Duniani, FIFA, linatarajia kupiga kura ili kuamua kuweka hadharani ripoti ya Uchunguzi wa Mgogoro wa Rushwa katika utoaji wa zabuni ya kuandaa fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2018 na 2011.
Zoezi hilo la upigaji wa kura unatrajiwa kufanywa wiki ijayo, ili kumaliza mzizi wa fitina ambayo umelighubika shirikisho hilo kwa siku za karibuni.
Mkutano huu utakaofanyika jijini Marrakesh, Morocco utatoa maamuzi ya kuweza kusambazwa ripoti ya uchunguzi wa kashfa ya rushwa katika kutoa nafasi ya wenyeji wa michuano ya kombe la dunia. 
Viongozi wa soka chini ya mapendekezo ya kamati ya maadili ya FIFA ilisisitiza siyo rahisi kutolewa kwa ripoti hiyo kwa sababu za kisheria. 
FIFA wamewapa nafasi Urusi kuwa wenyeji wa kombe la dunia mwaka 2018 na Qatar kwa mwaka 2022, uteuzi wa nchi hizi unaonekana umegubikwa na mazingira ya rushwa na kusababisha kumweka katika wakati mgumu Rais Sepp Blatter anayetarajiwa kuwania tena nafasi hiyo.
Hivi karibuni Rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya, UEFA, Michel Platini alimtaka Rais huyo wa FIFA, kupisha wengine na kuweka bayana hatampigia kura labda kama atajitokeza mgombea mwingine wa tatu.

Everton kumuongezea mkataba mpya Samuel Eto'o

http://cde.3.depor.pe/ima/0/0/1/4/2/142932.jpg
WAKALA wa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Cameroon, Samuel Eto’o anatarajiwa kuwa nchini Uingereza wakati wa krismasi ili kuzungumzia suala la kuongeza mkataba na klabu ya Everton.
Mkataba aliosaini mshambuliaji huyo wakati akitua Goodison Park kama mchezaji huru katika majira ya kiangazi una kipengele ambacho kinaruhusu mazungumzo kufanyika pindi mechi 15 zinazpokuwa zimechezwa.
Kutoka na umuhimu wa Eto,o katika klabu hiyo baada ya kufunga mabao manne na kusaidia mengine mawili katika mechi 15 za mashindano yote, Everton wanaonekana kuwa tayari na mazungumzo hayo.
Mara kadhaa kocha wa Everton, Roberto Martinez amekiri kuwa angependa kumbakisha Eto’o mwenye umri wa miaka 33 katika kikosi chake

Diamond, Ommy Dimpoz kuwania tuzo Uganda


WASANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond' na Omar Nyembo 'Ommy Dimpoz' wameteuliwa kuwania tuzo za HiPipo Music Awards (HMA-2015) za nchini Uganda.
Diamond aliyetoka kunyakua tuzo nne tofauti moja ya The Future ya Nigeria na tatu za Channel O, ameteuliwa kupitia wimbo wa 'Number One' alioimba pekee yake na Dimpoz kupitia 'Ndagushima'
Wasanii wameweka kwenye kundi moja la kipengele cha 'East Africa Super Hit' sambamba na Saul Soul kupitia wimbo wao wa "Nishike', Jaguar kupitia wimbo wake wa 'Kioo' na Knowless aliyewania kupitia wimbo wa 'Baramushaka'.
Wengine waliopo kwenye kipengele hicho ni Eddy Kenzo kupitia wimbo wake wa 'Sitya Loss', Urban Boys Ft Iyanya kupitia wimbo 'Tayali' na Bebe Cool aliyeteuliwa kupitia wimbo wa Love U Everyday'.
Tuzo hizo zinatarajiwa kutolewa rasmi wiki moja kabla ya 'Siku ya Wapendanao' yaani Februari 7 nchini humo.
Ebu cheki Orodha Kamili ya HMA-2015 hapo chini;

1. Artiste Of The Year
• Sheebah Karungi
• Radio & Weasel
• Jose Chameleone
• Irene Ntale
• Eddy Kenzo
• Bobi Wine
• Bebe Cool
2. Best Male Artiste• King Saha
• Jose Chameleone
• Eddy Kenzo
• David Lutalo
• Bobi Wine
• Bebe Cool
3. Best Female Artiste• Sheebah Karungi
• Rema
• Maureen Nantume
• Irene Ntale
• Irene Namatovu
4. Best Duo Group Artiste• Revival Band
• Radio And Weasel
• Pallaso & Sheebah
• New Eagles
• Golden Production Band
5. Best Male Breakthrough Artiste• Ziza Bafana
• Melody
• Lyto Boss
• Daxx Kartel
• A Pass
6. Best Female Breakthrough Artiste

• Zanie Brown
• Spice Diana
• Naira Ali
• Betina Namukasa
• Anita Da Diva
7. Best Use Of Social Media By Artiste

• Navio
• Maurice Kirya
• Hindu Asha
• Eddy Kenzo
• Bebe Cool
8. Best Concert Performance

• Teli Dogo – Gravity Omutujju
• Sitya Loss Concert – Eddy Kenzo
• Ekyikumi Physicaly Fit – Big Eye
• Best Of Bebe Cool
• Amasso Ntunga – Radio And Weasel
9. Best Artiste In Diaspora
• Sarah Musayimuto
• No1. Suspect Badman
• Mc Norman
• Fyonna Nsubuga
• Frank Rock
• Ang3lina (Angella Nabuufu)
10. Best Young/Teen Artiste• Triplets/Ghetto Kids
• M14 Omutugumbuzi
• Boys Of Destiny
• Aba Marcus Mayanja – Trex
11. Best Dj• Selector Jay
• DJ Slick Stuat
• DJ Shiru
• DJ Roja
• DJ Mark
• DJ Ivan
• DJ Hearts
• DJ Aludah
12. Album Of The Year• Pride By Navio
• Amaaso Ntunga By Radio And Weasel
• Akantu By David Lutalo
13. Video Of The Year• Wale Wale – Jose Chameleone
• Sitya Loss – Eddy Kenzo
• No Holding Back – Navio
• Love You Everyday – Bebe Cool
• Kuzala Kugyaganya – Irene Namatovu
• Fly Solo – Keko
14. Song Of The Year• Twesaana – Sheebah Karungi
• Sitya Loss – Eddy Kenzo
• Neera – Radio And Weasel
• Mulirwana – King Saha
• Love You Everyday – Bebe Cool
• Gyobela – Irene Ntale
15. Best Audio Producer• Nash Wonder
• Dr. Fizor
• Diggy Baur
• D.King (Buddies Studio)
• Crouch
16. Best Video Producer• Sasha Vbyz (Savy Films)
• Noltonmax & Georgeous Films
• Meddie Menz
• Jah Alive (Frank)
• Grate Make
17. Best Song Writer• Saxess
• Ray Signature
• Peter Nawe
• Nince Henry
• Jamie Culture
18. Best Hip Hop Song• No Holding Back – Navio
• Jajja Wo – Santana
• Ekyebeyi – Gravity Omutujju
• Akayimba Ka Maama – Gnl Zamba
• Ahh Ahh Ahh – Atlas Da African Dr. Jose Chameleone
19. Best Rnb Song• Olibeera Nange – Juliana
• Neera – Radio And Weasel
• Muchuzi Muchuzi – Rema
• Mubbi Bubbi – Maro Ft David Lutalo
• Kanzunzu – Lyto Boss
20. Best Ragga Dancehall Song• Zero Distance – Anita
• Tetubatya – Apass
• Pomini Pomini – Ziza Bafana
• Mundongo – Pallaso And Sheebah
• Kidandali – Ak47
21. Best Reggae Song• Ngolabye – Jamal
• Muntu Wange – Naira Ali
• Maze Okukwetegereza – Maro, Radio & Weasel
• Love You Everyday – Bebe Cool
• Equation – Desire Luzinda
• Dilema – Bobi Wine, Mr.G & Cindy
22. Best Religious Song• This Year – Dr Hilderman
• Sibiwulila – Wilson Bugembe
• List Ya Mukama – Julie Mutesasira
• Jungle – Levixone
• Amiina – Swahaba Kasumba
23. Best Band Song• Salute – Mary Bata
• Olweza – Geofrey Lutaaya
• Namakula – Meseach Semakula
• Nalalila – Catherine Kusasira
• Kisusunku – Maureen Nantume
• Akantu – David Lutalo
24. Best Kadongo Kamu/ Afro Folk Song• Muserebende – Gerald Kiwewa
• Kuzaala Kujagaana – Irene Namatovu
• Omugugu -Hassan Ndugga
• Etaaka – Kazibwe Kapo
• Agawalagana – Victor Kamenyo
25. Best Zouk Song• Nice And Lovely – Eddy Kenzo
• Neberela Eno – Chris Evans
• Gyobela – Irene Ntale
• Emikisa Gyabakazi – Betina Namukasa
• Bbaluwa – Rahma Ali
• Basusi Bamenvu – Nince Henry
26. Best Afrobeat Song• Twesana – Sheebah Karungi
• Size Yoo – Bobi Wine
• Nkoleki -Melody Ft Jose Chameleone
• Nkola Byafayo – Bebe Cool
• Mulirwana – King Saha
27. Best Afropop Song• Wale Wale – Jose Chameleone
• Sitya Loss – Eddy Kenzo
• Kitoobero – Viboyo Oweyo
• Go Down Low – Pallaso And Sheebah
• Evaluate – Jacki O Ft Andy Music
28. Best Western Region Song• Yanshobera – Dr Shaay
• Nankogu – Penny Patra
• Enshazi – Ray G
• Kaana Ka Maama – Dorrys Mutahunga
• Higher Level – Figo West
29. Best Eastern Region Song• Owakasanda Ke – Park U
• Nguwe Kumwoyo – Dr Denicris & Kmas
• Ngesi Ore – Genious Drey Ft 2gb
• Malizaa – Kmas Ft Sytrus
• Igwe Papa – Judith Akol
• Ekireta – Gazampa
30. Best Northern Region Song• Pingo – Pretty B
• Muko Kwany Dek – Bosmic Otim
• Mama – 2pee
• Latona – Nokkie Man
• Aol – Eddie Wizzie
31. Best Southern Region Song• Okuloga Ataffaa – Luwalira Dalausi
• Mu Part 2 – Kool Banti
• Jangu – Sk Brain Ft King Saha
• Eno Embaga – Tonny Rich
• Aliba Ani – Eng Wasswa
32. East Africa Super Hit• Tayali – Urban Boys Ft Iyanya
• Sitya Loss – Eddy Kenzo
• Ndagushima – Ommy Dimpoz
• Number One – Diamond Platnumz
• Nishike (Touch Me) – Sauti Sol
• Love You Everyday – Bebe Cool
• Kioo – Jaguar
• Baramushaka – Knowless
33. Most Active Fans Group• Team Radio & Weasel
• Team Juliana
• Team Jose Chameleone
• Gagamel Phamily
• Firebase Army
34. Lifetime Achievement

Wednesday, December 10, 2014

Arsenal yaua, Monaco Juve zapenya 16 Bora Ulaya

Wojciech Szczesny (left) looks on in shock as Arsenal players celebrate Ramsey's stunning strike
Wachezaji wa Arsenal wakishangilia bao lao kwa kumfuta kiatu Aaron Ramsey
Lukas Podolski fires past Galatasaray defender Semih Kaya to give Arsenal an early lead in the Group D clash
Podolski akifunga bao la kwanza la Arsenal
sare ya 1-1 dhidi ya Atletico Madrid ilitosha kuwavusha Juventus kwenye hatua ya 16 bora.
Wachezaji wa Juventus walifurahia baada ya timu yao kufuzu hatua ya 16 Bora
The Juventus squad couldn't hide their delight at progressing to the knockout stages of the Champions League on Tuesday evening
Hureeee!
Monaco nao walikuwa na furaha yao kama hivi

Bayer Leverkusen went through, but were disappointed at full-time after surrendering top spot to Monaco
Bayer Leverkusen naop wamefuzu 16 Bora
MABAO mawili ya kila mmoja toka kwa Aaron Ramsey na Lucas Podolski yaliiwezesha Arsenal ya Uingereza kupata ushindi mnono ugenini wa mabao 4-1 dhidi ya wenyeji wao Galatasaray ya Uturuki na kujihakikishia nafasi ya pili katika Kundi D la michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Podolski aliiandikia The Gunners bao la kuongoza dakika ya tatu tu tangu kuanza kwa pambano hilo kabla ya Ramsey kuongeza la pili dakika ya 11 na kisha kurudi tena kambani dakika ya 29.
Kipindi cha pili wenyeji walicharuka na kufanikiwa kupata bao la kufutia machozi lililofungwa na mkongwe Wesley Sneijder kwa mpira wa adhabu ndogo katika dakika ya 87.
Dakika tatu baadaye Ramsey alihitimisha karamu ya mabao kwa kufunga bao la nne na la pili kwake katika mchezo huo na kuifanya Arsenal ikitinga hatua ya 16 Bora nyuma ya Borussia Dortmund ya Ujerumani ambayo ililazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Anderlecht ya Ubelgiji.
Vijana hao wa Arsene Wenger wana hatari ya kukutana na moja ya timu mojawapo kati ya Real Madrid, Atletico Madrid, Barcelona, PSG, Bayern Munich, Porto au Monaco katika hatua ya mtoano.
Bao la Dortmund lilifungwa na Ciro Immobile katika dakika ya 58 kabla ya wageni kuchomoa dakika sita kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kupitia kwa Aleksandar Mitrovic  kwa njia ya kichwa.
Dortmund imeongoza kundi hilo kwa sare hiyo kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa, lixcha ya kulinga pointi 13 na Arsenal.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Juventus ikiwa nyumbani ililazmisha suluhu kwa Atletico Madrid na zote mbili kufuzu kwa hatua ya 16 Bora kutoka kundi A, licha ya Olympiakos Pirates kupata ushindi mnono wa mabao 4-2 djhidi ya Malmo ya Sweden.
Nayo timu ya Monaco ya Ufaransa ilifanikiwa kusonga mbele baada ya kuilaza Zenit St Petersburg ya Russia kwa mabao 2-0 na kuongoza kundi C ambalo lilishuhudia Bayer Leverkusen wakifuzu nao licha ya kung'ang'aniwa ugenini na Benfica ya Ureno.

ZILIFUZU 16 BORA
Kundi A: Atletico Madrid na Juventus
Kundi B: Real Madrid na Basle
Kundi C:Monaco na Bayer Leverkusen
Kundi D: Borussia Dortmund na Arsenal