STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 17, 2013

Mhariri Mtendaji 'Jamhuri' mbaroni, kisa...!

IGP Said Mwema
 Wadau,

Safari ya kupambana na ufisadi katika nchi hii ni ngumu sana.

Leo kuanzia saa 5 hadi saa 8:30 mchana, Mhariri Mtendaji wa Jamhuri, Deo Balile, amehojiwa Makao Makuu ya Polisi kuhusu habari iliyochapishwa kwenye Jamhuri inayohusu “Ufisadi ujio wa marais 11”

Kwa bahati nzuri, habari nzima wanaikubali kwamba ni ya kweli! Kasoro pekee eti ni matumizi ya barua ya Ikulu iliyokuwa na neno “Secret” ambayo ilikuwa na majina tu.

Anashitakiwa kwa kosa la "Kuchapisha Nyaraka za Siri", jambo ambalo ni kinyume cha Sheria ya Usalama, kifungu 5(1). Nimemwekea dhamana hadi Ijumaa saa 4 asubuhi.

Angalizo: 
Huu ni mwendelezo wa Serikali kukwepa kuwashughulikia wezi na wafujaji wa fedha za umma zaidi ya Sh bilioni 8 kwenye Mkutano wa Smart Partnership, badala yake wameamua kuhangaika na neno moja tu “Secret”. Hivi kweli neno “secret” ni kero na hatari zaidi kuliko hoja yenyewe ya kile kilichoandikwa?

Nawasilisha.
Manyerere Jackton

No comments:

Post a Comment