STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 29, 2014

Bayern Munich bado haishikiki Bundesliga

http://thesoccerdesk.com/wp-content/uploads/2013/11/bayern-munich.jpg
MABINGWA wa Ligi Kuu ya Ujerumani, Bayern Munich, imeendelea kulinda rekodi yao ya kutopoteza mchezo wowote katika ligi hiyo baada ya jioni hii kulazimishwa sare ya 3-3 ma Hoffenheim.
Bavarians waliotetea taji hilo mwanzoni mwa wiki hii kwa kuifunga Hertha Berlin mabao 3-1, ilishutuliwa na wageni wao baada ya  Anthony Modeste alipofunga katika dakika yua 23.
Hata hivyo wenyeji walicharuka na kusawazisha bao kupitia kwa Claudio Pizarro katika dakika ya 31 kabla ya Xherdan Shaqiri kuongeza la pili katika dakika ya 34.
Pizarro aliongeza bao jingine dakika ya 40 na dakika moja kabla ya mapumziko Salihovic aliifungia Hoffenheim bao la pili na kufanya timu yao iende mapumziko wakiwa nyuma kwa mabao 3-2.
Kipindi cha pili wageni waliopo nafasi ya katikati waliendelea kuwasumbua wenyeji wao na kufanikiwa kusawazisha bao katika dakika ya 75 kupitia kwa Roberto Firmino.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Borussia Dotmund ikiwa ugenini ilipata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Stuttgart, Bayer Leverkusern ililazimishwa sare ya 1-1 na Eintracht Braunschweig.
Nayo timu ya Wolfsburg wakiitandika Eintracht Frankfurt 2-1 na Mainz 05 ikapata ushindi mnono nyumbani kwa kuizabua Augsburg kwa mabao 3-0.

No comments:

Post a Comment