STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 29, 2014

Arsenal, Manchester City zashindwa kutambiana

Olivier Giroud and Mathieu FlaminiKLABU ya soka ya Arsenal imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Manchester City katika pambano la Ligi Kuu ya England.
Wageni wa walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 18 kupitia kwa David Silva na kudumu wakati wa mapumziko.
Hata hivyo wenyeji walifanikiwa kuchomoa bao hilo dakika chache baada ya kuanza kipindi cha pili kupitia kwa Mathieu Flamini akimalizia kazi nzuri ya Lucas Podolski.
Sare hiyo imeikwamisha Manchester City kukaa kileleni baada ya Chelsea kufungwa bao 1-0 na Crystal Palace kwani imefikisha pointi 67 kwa michezo 30 na kubakia nafasi ya tatu nyuma ya Liverpool yenye pointi 68 na itakayoshuka dimbani kesho Anfield kuumana na Tottenham Hotspur.
Arsenal yenyewe wamesalia kwenye nafasi ya nne ikiwa na pointi 64 na baada ya kushuka dimbani mara 32.

No comments:

Post a Comment