STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 29, 2014

Samatta aivusha TP Mazembe 8 Bora

Shujaa Mbwana Samatta
TIMU ya TP Mazembe ya DR Congo imefanikiwa kuwa timu ya kwanza kutinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Sewe ya Ivory Coast.
Bao hjilo pekee lililoivusha Mazembe lilitupiwa kimiani na Mbwana Samatta  katika dakika ya 66, huku wakikosa pia penati baada ya Jonas Sakuwaha kushindwa kumtungia kipa wa Sewe Sylvain Gbohouo.
Ushindi huo uliopatikana mjini Lubumbashi, umeifanya Mazembe kufuzu kwa faida ya bao la ugenini kwani matokeo ya jumla yamekuwa 2-2 baada ya wiki iliyopita vijana hao wa Kongo kufungwa mabao 2-1 bao lililofungwa na Mbwana Samatta ambaye ni Mchezaji Bora wa Mwaka wa TP Mazembe kwa mwaka jana.

No comments:

Post a Comment