STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 29, 2014

PSG yazidi kupeta Ufaransa

Paris Saint Germain's Zlatan Ibrahimovic of Sweden, center, controls the ball past Nice's Mathieu Bodmer of France, left, during their French League One soccer match, in Nice stadium,southeastern France, Friday, March 28, 2014. (AP Photo/Lionel Cironneau)
Zlatan Ibrahimovic akichuana na wachezaji wa Nice wakati PSG ilipopata ushindi wa ugenini
BAO la kujifunga la Timothee Kolodziejczak wa Nice usiku wa jana liliisaidia mabingwa watetezi wa Ligue 1, PSG kuendeleza wimbi la ushindi katika ligi hiyo na kujichimbia kileleni.
Wenyeji walijifunga bao hilo katika dakika ya 52 wakati Kolodziejczak akiwa katika harakati za kuokoa mpira na kuisaidia PSG ambayo Jumatano itavaana na Chelsea katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa  Ulaya kujikita kileleni.
Timu hiyo kwa ushindi wa jana imefikisha jumla ya pointi 76 kutokana na michezo 31 na kuwaacha wanaowafukuzia Monaco kwa pointi 13 hata Monaco itakayoshuka dimbani leo dhidi ya Evian TG.

No comments:

Post a Comment