STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 8, 2014

Breaking News: Ajali nyingine yaua zaidi ya watu 10 Gairo


ajali tabora 1
Baadhi ya waokozi wakiitoa miili ya abiria ndani ya gari hilo
AJALI za barabarani zimeendelea kupoteza uhai wa watanzania baada ya muda mfupi uliopita kudokezwa kuwa mapema leo asubuhi bao la Airbus lililokuwa likitoka Dar es Salaam kuelekea Tabora kupinduka ewneo la Kuegeya mjini Gairo na kusababisha vya watu kadhaa huku wengine wakiwa majeruhi.
MICHARAZO inafuatilia taarifa hizo na zitawafahamisha vyema na idaidi ya waliokufa katika ajali hiyo inayoelezwa kuwa ni mbaya kutokana na basi hilo kupinduka na kuwarusha baadhi ya abiria.
Hata hivyo taarifa za awali zinasema watu zaidi ya 10 wamekufa katika ajali hiyona Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro,Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi(SACP) Faustine Shilogile amethibitisha ajaliu hiyo akiwa eneo la tukio.
Kamanda Shilogile alisema angetoa taarifa baadaye kuhusu idadi kamili ya waliofariki na majeruhi, ila alikiri ni ajali mbaya.
Ajali imekuja ikiwa ni siku chache tangu watu zaidi ya 30 kufa katika ajali iliyohusisha magari matatu yakiwamo mabasi mawili ya J4 na Mwanza Coach kugongana mjini Musoma na kujeruhi wengine zaidi ya 70. 

No comments:

Post a Comment